Apr 9, 2010

UDOM Uchafu Kunuka



  • Wanafunzi wabaki yatima
  • Na Fita Lutonja
    CHUO kikuu cha Dodoma ni chuo kipya ambacho kimejaa misukosuko na mikasa ya kila aina. Kama wewe unaishi bali na huwa unakiona chuo hiki katika runinga basi huwezi jua mambo yaliyopo katika chuo hiki.

    Yawezekana pia huwa unakisikia kwenye vyombo vya habari mbalimbali vikisifiwa na viongozi wetu akiwemo rais wetu ambaye hachoki kukisifia kila anapoulizwa kuhusiana na serikali imeleta maendeleo gani hasa katika sekta ya elimu.

    Rais wangu mara nyingi amekuwa akionekana katika nyombo vya habari mbalimbali akiisifu serikali yake hasa katika kujenga chuo kikuu cha Dodoma.

    Hakika ni jambo zuri kukisifia kwani ni mojawapo ya kukitangaza ndani na nje ya nchi ili kiweze kujulikana zaidi ikiwa pamoja na serikali kupata sifa mbalimbali kwa kuamua kujenga chuo hicho.

    Lakini pamoja na kuangalia kwa umbo la nje basi wanatakiwa kuangalia na umbo la ndani ya chuo hicho, kwani chuo hicho kina kabiliwa na matatizo chungu nzima.

    Ukianzia tatizo la maji kwa wanafunzi hakika wanafunzi wanateseka sana nikiwemo na mimi mwandishi wa habari ambaye pia ni mojawapo wa wanafuzi wa chuo hiki.

    Katika chuo hiki maji huwa yanapatikana kwa shida wakati mwingine yanamaliza hata wiki mbili hadi tatu au zaidi bila maji na hapo chuo chote huwa kinanuka harufu mbaya kuanzia kwenye mabweni ya kulala mpaka majengo ya utawala.

    Wanafuzi wanaingia madarasani bila kuonga huku wengine wakikimbilia kijijini kwa wanakijiji kuomba maji angalu wapate ya kunawa usoni.

    Ni aibu kubwa sana kwa sisi tunaojivunia kuwa tumejenga chuo cha kimataifa wakati maji tu yametushinda kuyapeleka chuoni. Wanafunzi wanahangaika na maji wahadhili na wakufunzi wanahangaika na maji.

    Kwa upande wa wasomi wetu kuwatesa kiasi hicho cha kuwashindishi wiki mbili wakati mwingine wiki tatu bila maji tunajenga Taifa gani kwa vijana wetu? Au tunajenga Taifa la mateso? Kwa sababu tunajua kuwa vijana ndiyo Taifa la kesho.

    Mimi huwa nashindwa kujua hivi kweli uongozi wa chuo na wahusika wa maji tatizo hili hawalioni chuoni hapa? Kama maji Dodoma ni ya shida kunahaja gani ya kujenga chuo mahali ambapo hakuna maji kwa ajili ya wasomi wanaosoma hapo?

    Tusijenge chuo kwa kutafuta sifa bali tujenge chuo kwa kuangalia falsafa za mbele kwa kujiuliza. Je, hiki chuo kikiwa hakina maji kitazalisha wasomi wa aina gani? Je, iwapo kama wasomi wetu watasoma huku wakihangaika na kwenda kuomba maji kijijini watafaulu kwa kiwango kipi? Na je tunajenga chuo ili kije kilisaidieje Taifa kwa namna gani? Yatupasa tujilize maswali mengi na tukiyapatia ufumbuzi hakika hatuwezi kuwaacha wanafunzi waendelee kukoswa maji.

    Kitu kingine ambacho huwa kinanichanganya zaidi na kushindwa kujua kama kweli maji Dodoma hayapo ni pale viongozi wetu wanapokuja kutembelea chuoni.

    Siku hiyo ambayo kiongozi yeyote wa ngazi za juu kama anakuja chuoni maji huwa yanaanza kutoka kuanzia saa kumi usiku jambo ambalo huwa linaniacha kwenye dimbwi la fikra huku nikibaki na maswali ya kifalsafa; Kwanini yametoka?. Kwanini huwa wanakata maji kama hakuna kiongozi yeyeto ambaye anakuja chuoni? Kwanini sisi hawatudhamini wanatuona kama wanyama ambao hawaogi? Kwanini wanatutesa? Nk.

    Hivi karibuni wanafunzi tulikuwa tumechafuka kwa kukoswa maji lakini siku ambayo rais msitaafu ambaye pia ni mkuu wa chuo chetu Benjamin Mkapa alikuja chuoni tulipata nafuu kwani siku hiyo maji yalitoka siku nzima, lakini baada ya kuondoka tukaendelea na shida yetu ya kuishi bila maji huku tukivumilia harufu mbaya ya kila sehemu.

    Hapo sasa ndiyo tunajenga chuo cha kimataifa? Chuo bila maji wapi na wapi? Mzungu gani atakuja kusoma bila maji? Chuo bila kujali wanafunzi wapi na wapi? Chuo bila kujali wahadhili wake wapi na wapi? Tunajenga tu majengo lukuki lakini ndani hatuboreshi.

    Bila kuboresha ndani tutatoa wahitimu wanaokubalika kimataifa au tunataka kutoa wahitimu feki ambao wataenda kushindwa hata kufanya kazi ya taaluma walizozisomea na matokeo yake chuo chetu cha kimataifa kikaonekana na chenyewe feki?

    Siku ambayo alikuja Mkapa tulifurahi sana tukijua kwa kuwa yeye ni mkuu wa chuo basi tutamfikishia matatizo yetu ili ayapatie ufumbuzi ili nasi tupate nafuu ya kutulia chuoni kusoma badala ya kila siku kushinda tunahangaika vijijini kutafuta maji.


    Lakini siku hiyo cha kushangaza na kusikitisha ikiwa pamoja na kusitaabisha mkuu wetu wa chuo Mkapa hakuweza hata kuongea nasi, jambo ambalo lilituuma sana na kutuumiza roho zetu kwa kushindwa kufikisha shida zinazotukabili.

    Tukiangalia naye makamu mkuu wa chuo Prof. Idris Kikula naye hatupi nafasi hata ya kuonana naye ili angalau tuweze kumueleza shida zetu. Sasa sisi tutatatuliwa na nani matatizo yetu? Na tutaendelea na matatizo mpaka lini? Mbona munatudhulumu haki yetu? Mbona uhuru wetu munatunyima? Mbona munatuumiza kisaikolojia? Sasa iko wapi haki yetu? Kikula na Mkapa rais wagu mstafu na mkuu wangu wa chuo iko wapi haki na demokrasia yetu?

    Tangia nifike chuoni hapa yapata miaka miwili sasa lakini makamu mkuu wa chuo changu hajawahi hata siku moja kuongea na wanafuzi ili wamueleze matatizo mbalimbali yanayowaandama jambo ambalo huwa linatusikitisha.

    Yawezekana makamu wa chuo chetu katususia? Na kama katususia tumemukosea nini makamu wetu wa chuo Kikula? Tunamuomba sasa atuokoe na jahazi linalotukabili la mateso makubwa yanayotishia kutuharibia masomo yetu kwa kushinda nje ya chuo tukilandalanda kutafuta maji.

    Namkumbuka makamu mkuu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam Prof. Rwekeza Mukandara huwa anaongea na wanafuzi mara kwa mara ili kuweza kujua matatizo yao mbona Pro.Kikula wa chuo chetu haongei na sisi wanafunzi wake?

    Wakati sijaja hapa chuoni kusoma nilikuwa naitumia taaluma yangu kwa kuadika katika gazeti la Mwananchi nimeandika habari nyingi za Mkandara akiongea na wanafunzi mpaka nimeondoka kuja kusoma huku Dodoma Mkandara alikuwa na huo utaratibu wa kuongea na wanafunzi. Mbona Kikula ambaye anaonekana baba mpole mwenye hekima na busara hafanyi hivyo?

    Sasa sisi wanafunzi wa Udom tumekuwa yatima hatuna wa kutusaidia ili kuondokana na matatizo haya. Tumetelekezwa bila msaada wowote na sasa hatuoni uhuru wetu shahada zetu ziko hatarini. Ninaishia hapa ili niwahi kwenda kijijini kutafuata maji iusije ikala kwangu.

    Mwandishi wa makala haya anapatikana kwa simu: 0764 992264,niandikie:fitazi@hotmail.com Nitembelee: http://www.fitalutonja.blogspot.com/
    MWISHO













Jan 4, 2009

Mugabe: Kamwe sitamwamini Mzungu

Asema wazungu kwao si Afrika

Makala
Na Fita Lutonja

“KAMWE sitamwamini Mzungu hata siku moja, mweupe pekee wa kumwamini ni yule aliyekufa, wazungu kwao si Afrika, Afrika ni ya Waafrika hivyo basi Zimbanwe ni ya Wazimbabwe”

Huo ni usemi wa Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe (84) ambao amekuwa akinukuliwa na vyombo vya habari akiutumia kila wakati kuonyesha msimamo wake kwamba hababaishwi na mataifa ya Magharibi na hayaamini kama mataifa hayo yana nia nzuri na bara la Afrika.

Rais huyo amekuwa adui wa mataifa hayo kutokana na misimamo yake ya uongozi. Wanachokiona watu wa Magharibi ni kwamba rais Mugabe ni Mbale anayetumia madaraka vibaya kwa kutetea rasilimali za Wazimbabwe ili zisichuliwe na Mataifa hayo ya Magharibi.

Kwa msimamo wa Mugabe ni dhahili kuwa Rais huyo amedhamilia kutetea rasilimali za nchi yake ili zisichukuliwe na Mataifa ya Ughaibuni ambapo pia amenukuliwa akisisitiza kwa kusema kuwa “Ardhi ni yetu na wala si ya Ughaibuni tumeichukua na kuwapa watu wanaostahili”.

Rais huyo alisema hayo wakati alipoamru wazungu wapokonywe ardhi walikuwa wanaimiliki nchini Zimbabwe na wapewe wazawa wa nchi hiyo.

Msimamo wake daima amekuwa akionyesha kwamba si sahihi kwa mtu Mweupe kumiliki ardhi ya bara la Afrika huku wazawa wakihangaika hawana hata sehemu ya kulima.

Anachoamini Mugabe ni kwamba Afrika ni kwa ajili ya Waafrika, msimamo wa aina hiyo umekuwa ukimweka katika migogoro na mataifa ya Ulaya na Marekani.

Hata nchi yake ilipowekewa vikwazo vya kunyimwa misaada na mataifa hayo ya Ulaya na Marekani ambapo ilipelekea Zimbabwe kuwa na hali mbaya kiuchumi, rais Mugabe hakutishika na hilo bali aliendelea kutamba kwa kusisitiza “Kamwe hatutaanguka, acha ukame uje, umasikini nao uje, lakini asilan hatutaanguka daima”

Usemi wa Mugabe unaonyesha kuwa anamsimamo na fikra kubwa za kujua kuwa nchi yake haitajengwa kwa misaada kutoka ughaibuni bali itajengwa na Wazimbabwe wenyewe kwakutumia rasilimali zao.

Pia msimamo huo unaonyesha kuwa haitatokea hata siku moja wazimbabwe wakapiga makoti kwa mataifa ya uhgaibuni ili wapate misaada ambao ya kiunyonyaji kwa sababu misaada hiyo inalenga kuiibia Zimbabwe rasilimali zake. Kwa Mugabe hilo kamwe anasema halitatokea hata situ moja.

Mugabe hataki kuhusudu misaada kutoka ughaibuni wakati akijua kuma Mataifa mingine ya Afrika yanavyohusudu likiwemo Taifa laTanzania.

Nikifkria mpaka ninashindwa kujua huyu Mugabe ujasiri wa kuamua kutetea rasilimali za nchi hiyo ameutoa wapi? Huu ujasiri wa Mugabe huwa ninaufanananisha na ujasiri wa Julius kaisar ambapo na yeye kuna kipindi alidiliki kusema kuwa kamwe hawezi kumuogopa Mzungu mwenye kitambi na nywele ndefu bali anawaheshimu sana wanyonge na wanaodhulumiwa haki yao.


Kwa watu wenye mtazamo tofauti wanaweza wakauchukia msimamo wa Mugabe wa “kutokumwamini Mzungu”. Lakini msimamo huu ni wa kweli kabisa na unamantiki sana kwa Mataifa ya Afrika ambayo yanahusudu Wazungu kwa kuwapa ardhi na kila rasilimali, wakati Wazalendo wa mataifa hayo wakiendelea kuteseka na umasikini hohehahe.

Mataifa mengi ya kiafrika kuwapata viongozi kama Rais Mugabe wenye kuzilinda rasilimali za nchi zao zisiendelee kuchukuliwa na Wazungu ni wachache mno.

Labda Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na mfumo wa Azimio la Arusha, yeye ndiye anaweza kuwa mfano wa kuigwa katika kutetea rasilimali za Wazalendo kwa kuazisha mfumo wa utawala wa Azimio la Arusha ambalo lilikuwa na misingi ya kuhakikisha Watanzania wanafanyakazi bila kutegemea misaada kutoka kwa Mataifa mengine, Mwalimu aliwahi kusema “Tanzania daima itajengwa na Watanzania wenyewe na haiwezi kujengwa kwa misaada ya Mataifa mengine”

Mugabe kwa msimamo wake wa kutetea rasilimali za nchi yake zisiibiwe na Wazungu, ni dhahili kuwa kiongozi huyo sasa ametambua kuwa Afrika bado hajajikomboa na kupata uhuru wa kweli bali iko katika ukoloni wa kiunyonyaji ambao ni "Ukoloni Mamboleo"

Ukoloni huu unaimaliza Afrika taratibu bila viongozi wa nchi hizo kutambua kuwa nchi zao zinafirisiwa kiujanja na Mataifa hayo ya Ughaibuni.

Katika bara África Rais Mugabe peke yake ndiye anayeonekana kulinda rasilimali za nchi yake kwa manufaa ya wazalendo wa nchi hiyo, ambapo ni ishara kubwa ya kuonyesha anataka kuikomboa nchi yake kutoka katika ukoloni wa kiunyonyaji uchumi "Ukoloni mamboleo" ambao Mataifa yote ya afrika yanauhusudu na kuupigia magoti ndio maana yanaendelea kunyonywa kila kukicha huku yakiendelea kuwa masikini ya kutupwa.

Lengo kuu la Mugabe ni kutaka kuona Zimbabwe ikiwa huru na inajengwa na rasilimali zake na sio kutegemea misaada mbalimbali kutoka katika Mataifa yalioendelea ambayo lengo kuu la Mataifa hayo ni kutoa misaada ya kiunyonyaji ili wachukue rasilimali za Waafrika.

Hatukatai kuwa uchumi wa Zimbabwe umeyumba, katika kipindi hiki kutokama na mataifa hayo ya ughaibuni kusitisha kutoa misaada mbalimbali katika nchi hiyo, jambo hili la kunyimwa misaada Zimbabwe ni jambo ambalo Wazimbabwe wanatakiwa kuelewa kuwa wanachotakiwa sasa ni kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha Zimbabwe wanaitoa katika ndimbi la umasikini ni sio kutegemea misaada ya kiwiziwizi yenye mlengo wa kudidiniza uchumi wao.

Wazimbabwe wanatakiwa waondoe fikra ya kutawaliwa na kuwa tegemezi kama mataifa mengine ya Afrika, kwani sasa hivi wanachotakiwa kutambua kuwa wako huru na rasilimali zao katika kuzitumia tofauti na mataifa mengine ambayo bado yametawaliwa kiuchumi huku yakiendelea kunyonywa.

Jambo la Zimbabwe kujikomboa kutoka katika unyonyaji huu ni jambo la kufurahia kwa sababu uhuru huo ni Zimbabwe peke yake ambayo imeupata kati ya nchi zote za Afrika.

Ninaimani wazimbabwe mabadiliko ya ghafra ya kupata uhuru wenu yamewapa usumbufu mkubwa kutokana na kupandikizwa fikra tegemezi za Wazungu zilizowafanya kusahau kujitegemea mkahusudu misaada wakati rasilimali yenu inaibiwa bila kujitambua.

Kwa hiyo mabadiliko haya mnatakiwa mshangilie kwa kuwa uhuru wa nchi yenu umepatikana na mnatakiwa kuondoa fikra tegemezi mulizopandikizwa na wazungu na kuwapumbaza ili waendelee kuwanyonya rasilimali zenu, huku wenyewe Wazungu wakiendelea kiuchumi katika nchi zao na nyinyi munaendele kuwa na umaskini na fikra tegemezi.

Kumbukeni ya kwamba katika kitabu kitakatifu Bibria inatuambia kwamba wakati Mussa anawakomboa wana wa Israel kutoka katika utumwa wa nchi ya Misri, walilalamika huku wakimraumu Mussa wakisema, “Mussa amewatoa katika nchi ya neema nyenye asali na maziwa amewapeleka nchi ya Kanan ambayo ina njaa na mateso ya kila aina”.

Hawa wana wa Israel walikuwa wamezoea kunyonya na kutumikiswa na Wamisri kwahiyo mabadiliiko ya kutolewa Misri yaliwapa shida Wana wa Israel.

Lakini walipozoea waliona kuwa kumbe kweli walikuwa ndani ya utumwa bila wao kujua.

Na nyinyi Wazimbabwe yawapaswa musiendelee kulaumu na kulalamika ya kwamba Mugabe kawafukuza Wazungu kutoka katika nchi yenu kuwa amefanya makosa. La hasha! hajafanya makosa mbali ameamua kuwakomboa kutoka katika utumwa wa kizungu.

Msihudhunike na kufadhaika mioyoni mwenu ya kwamba Zimbabwe imekoswa misaada. Hiyo misaada ilikuwa ya kiunyonyaji kwa sababu ilikuwa inatumika kama ngao ya kuwatuliza msije kugundua wizi wa mchana wa Wazungu ambao wanaufanya katika Mataifa ya Afrika.

Kumbukeni ya kuwa uchumi wa Zimbabwe hauwezi kujengwa na Mataifa kutoka Ughaibuni hata siku moja haitatoke kamwe! Hivi ebu jiulizeni tangia lini nchi nyingine akajenga uchumi wa nchi nyingine?

Wazimbabwe wanachotakiwa ni kufanya kazi kwa kutumia rasilimali zao katika kuhakikisha wanaondokana na umasikini kwani bahati kubwa waliyoipata ya kujikomboa kutoka kwa wezi wa mchana wazungu ni bahati kubwa mno.

Afrika imefanywa kama kitega uchumi cha kuendeleza nchi za ughaibuni! Afrika imefanywa ndio sehemu ya kuchukua utajili na kuuhamishia katika Mataifa ya Ughaibuni! Afrika imefanywa kama mtaji wa kuendeleza uchumi wa nchi za Ughaibuni! rasilimali za afrika kama vile dhahabu, almas, ulanga, Tanzanite nk. zimekuwa mtaji wa kuendeleza na kukuza uchumi wa Wazungu. Kwa mtindo huu lini tutajikomboa kiuchumi?

Mbona hawa wazungu wanaione sana Afrika? Tangia enzi za zamani wanaidhulumu bila hata kutuhurumia! Walitufanya watumwa wakatuuza kwa mataifa ya mbali. Hawakulidhika na hilo wakaamua kututawala bila ruhusa huku wakaendelea kutunyonya.

Na baada ya kuondoka katika harakati za kudai uhuru wa bendera waliondoka huku wakiwa na kinyongo ndio maana tena wamekuja na njia nyingine ya kutunyonya ya ukoloni mamboleo.

Tukikataa huu ukoloni mamboleo wanatutishia kutunyima msaada? Hawa watu katu si wa kuwaamini hata siku moja!
Mwisho.
Nipigie: +255 764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com
Nitembee: http://www.fitalutonja.blogspot.com/

Dec 27, 2008

Aleyevunja azimio la Arusha alimusaliti baba wa Taifa Mwalim Jk. Nyerere


Anasitahili kulaaniwa na Watanzania wote

Na Fita Lutonja

ILIKUWA mwaka 1992 kipindi cha rais Ally Hassan Mwinyi ambapo watu wachache bila hata kumshirikisha Muasisi wa Taifa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere walikutana Zanzibar wakiwa na lengo la kuvunja mwongozi alioweka Mwalimu wa Azimio la Arusha.

Mwaka huo ulikuwa ni mwaka wa mapinduzi makubwa yaliyofanya na watu hao yakuondoa mfumo wa utawala wa Azimio la Arusha ambao ulikuwa unakataza dhuluma kwa kila mtu na kusisitiza kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kulikomboa taifa kutoka katika umasikini.


Hatukujua mfumo wenye asili ya kibepari waliutoa wapi? Na ulikuwana faida gani kwetu? Kwa sababu hawakutueleza faida za Mfumo huo kwa taifa letu na watanzania kwa ujumla.

Walidai kuwa wanaanzisha Azimio la Zanzimbar ambapo lengo lake hatukulijua lilikuwa ni nini? Au ilikuwa ni kuruhusu aina ya ufisadi ndani ya serikali hatukujua? au hilo Azimio la Zanzíbar lilikuwa na maana gani mpaka likasababisha mfumo wa baba wa taifa wa Azimio la Arusha kuonekana halifai? Jama hizo za kulivunja Azimio la Arusha mpaka leo watanzania hatujui zilikuwa na lengo gani?


Kama kweli walivunja Azimio la Arusha kwa lengo zuri mbona hawakutueleza faida za Azimio hilo la Zanzibar, kama alivyotueleza mwalimu faida za Azimio la Arusha?

Mwalimu alielezea faida za Azimio la Arusha kwa njia mbalimbali ikiwemo kupitia vyombo vya habari, vipeperushi, pia aliandika vitabu mbalimbali zinazoelezea faida za Azimio la Arusha lakini nyinyi na Azimio lenu la Zanzimbar hatujaona hata kitabu kimoja kinachoelezea faida za Azimio la Zanzimbar?


Tunakumbua ilikuwa mwaka 1967 ambapo Mwalimu alibaini dhuluma, matumizi mabaya ya madaraka , unyonyaji na ubinafsi wa viongozi ndani ya serikali yake, jambo ambalo aliona litaipeleka nchi katika hali mbaya kiuchumi na kuleta matabaka ya kiunyonyaji.

Mwalimu kwa kuona nchi itakuja kuwa mfalme wa unyonyaji aliamua kuanzisha mfumo mpya wa utawala wa Azimio la Arusha ambalo lilifanikiwa kukomesha fisikoko, unyonyaji na waliozoea kudhulu jasho la wananchi na kunufaisha matumbo yao pia nao walikomeshwa.

Fisikoko na kupe wanyonya jasho la wezao walikuwa wamezoea kudhulumu kutoka katika jasho la wanyonge walikomeshwa kwelikweli.

Mwalimu kwa kuhakikisha dhuluma, unyonyaji, wizi, matumizi ya madaraka vibaya na ukwapuaji wa pesa ovyo unathibitiwa aliamua kuazisha utawala bora wa Azimio jambo ambalo lilileta haki na usawa wa kumiliki mali ya umma.


Watanzania tuliposikia Azimio la Arusha limetangazwa huku likiwa na misingi ya utawala bora wa kuthibiti unyonyaji na dhuluma tulishangilia kwa fifijo na nderemo tukijua sasa saa ya ukombozi kwa taifa imefika.

Furaha yetu kweli ilileta matunda mema kwa taifa na wananchi kwa sababu Azimio la Arusha lilihakikisha kila mtumishi wa serikali anatumia madaraka yake vizuri huku akifanya kazi kwa bidii na kufuata maadili ya uongozi ili kujenga uchumi wa nchi.

Viongozi wote ndani ya utawala wa Azimio la Arusha hawakuruhusiwa kuiba mali ya umma na kujiongezea mapato yao, bali walitakiwa kutumia mishahara yao katika kuendesha maisha.

Lakini nyinyi muliona mafanikio haya yaliyoletwa na Mwalimu kwa kupitia Azimio la Arusha hayafai, kama hayafai kwanini munahubili utawala bora wa Mwalimu? Huwa munamaanisha nini mnaposema tumuenzi baba wa Taifa huku mkipingana naye kwa kuvunja misingi ya utawala bora wa Azimio la Arusha?

Azimio lilihakikisha mali ya umma inalindwa kwa ajili ya watanzania na iwapo kama kiongozi atatumia mali ya umma vibaya alihesabiwa kuwa amehujumu uchumi wa nchi na hukumu yake ilikuwa kali mno ili kutoa fundisho kwa kiongozi wengine kutotenda makosa ya aina hiyo.

Mwalimu alikuwa mkali sana akiona kiongozi yeyote amehujumu mali ya umma jambo ambalo linajithihilisha pale serikali yake kwa kuzingatia misingi ya maadili kwa kiongozi wa umma iliamua kumhukumu waziri mmoja wa sheria kwenda jera miezi 12 na kuchapya viboko 24 hadharani.

Tukiangalia katika utekelezaji wa maendeleo tuliona Azimio la Arusha lilianzisha siasa ya ujamaa na kujitegemea ili kuhakikisha taifa linajikomboa kutoka katika umasikini.

Katika mfumo wa ujamaa tunaona ujamaa wa Mwalimu ulisisitiza kufanya kazi kwa bidii na nguvu zote bila kutegeana ili kuongeza uzalishaji na kupelekea kuinua pato la taifa.

Ujamaa ulikataa dhuluma na matumizi mabaya ya pato la wajamaa huku ukisisitiza kuwa kila pato linamilikiwa na wajamaa wote na hakuna ubaguzi wowote.

Lakini sasa hivi dhuluma, utumiaji wa madaraka vibaya, unyonyaji, ubaguzi, mikataba mibovu ya Richmond, uchotaji wa pesa za malipo ya nje (EPA) umezidi na kupelekea watanzania kuhujumiwa mali yao hadhalani jambo ambalo Mwalimu alikuwa akilipinga sana ndani ya utawala wake wa Azimio la Arusha.


Vilevile ndani ya Azimio la Arusha, Ujamaa ulikuwa na misingi ya kutoa huduma kwa jamii bure, ikiwemo huduma ya elimu, jambo ambalo lilipelekea kupata wasomi wengi tofauti na tulivyoacha na wakoloni ambao waliicha Tanzania ikiwa na wasomi wenye taaluma wachache.

Katika utekelezaji wa jambo hili unadhihilisha kuwa Mwalimu hakupenda kabisa dhuluma zitokee hata kwenye sekta ya elimu kwani kumlipisha mtu aliona itajenga matabaka kwa wasomi wenye pesa, na masikini wasikuwa na elimu.


Na katika siasa ya kujitegemea Mwalimu alisisitiza kufanya kazi kwa bidii bila kutegemea misaada kutoka katika mataifa mengine kwa sababu alijua kuwa sisi ni matajiri wa rasilimari nyingi ambazo tukizitumia tunaweza kujikomboa kiuchumi.

Hakika Azimio lilifanikiwa kukomesha hali ya dhuluma, unyonyaji, ukupe, fisikoko, wezi wa mali ya umma, ukiritimba, ubeberu wa kujimilikisha mali ovyo kisa umebeba madaraka, yote haya ndani ya utawala wa Mwalimu yalikomeshwa.

Lakini sasa watanzania tunadhulumiwa haki yetu kabisa tunashuhudia viongozi wanatumia madaraka vibaya na kujimilikisha mali ya umma huku wakidai kuwa ujasiliamali? Tuelezeni kama mlivunja Azimio la Arusha ili muwe wajasiriamali?

Hii kweli inaingia akilini kuwa ujasiliamali unaufanyia kwenye sehemu ya uongozi? Mbona Mwalimu wakati akiwa kiongozi hakufanya huo ujasriamali? Kwa sababu alikuwa anaheshimu utawala bora wa Azimio la Arusha ambao nyinyi muliona haufai.

Haki yetu mbona munachukua bira kutuhurumia sisi watanzania masikini? Munahubiri maisha bora kwa kila mtanzania, tutapataje maisha bora wakati misingi ya kulinda mali ya umma mumeivunja iliyokuwa inatekelezwa na Azimio la Arusha?

Tunajua kuwa Azimio la Arusha lilileta usawa na kuondoa matabaka ya matajili na masikini. Lakini sasa hivi tunashudia matabaka ya walionacho na wasionacho yameongezeka huku hao matajiri wakitudhulumu nguvu kazi zetu kwa kututumikisha na kutulipa ujira finyu jambo ambalo Mwalimu alikuwa analipinga sana.

Mumevunja Azimio la Arusha ambalo lilikuwa na misingi ya maadili kwa kiongozi wa umma kutojimilikisha na kutumia madaraka vibaya kujinufaisha mwenyewe lakini sasa hivi watanzania tunashuhudia kila kiongozi aliyoko madarakani anamiliki mali nyingi, kila kiongozi aliyestafu tunaona ndio wale wanaomiliki makampuni, taasisi pamoja na vitega uchumi vingi.

Hizo mali mumezipataje? Kama sio kuthulumu mali ya watanzania wezenu? Kama kweli mumepata kwa uhali mbona munalindana zikitolewa hoja za kuchunguzwa?

Wakina Wilbroad Slaa wakipendekeza muchunguzwe ili kubaini mulikozipata hizo mali, munaanza kujikingia kifua na kujilinda wenyewe ili msifichunguzwe. Hakika tunawaambia kuwa Mwalimu alipoanzisha Azimio la Arusha hakutaka kabisa mambo mnayoyafanya yafanyike ndani ya nchi hii ya Tanzania.

Hakika kama Mwalimu angerudi angeshaanga kuona Tanzania aliyoiacha imebadilika, wawekezaji, mabepari, mabeberu wakiritimba na viongozi ndiyo wamekuwa wamiliki wa rasilimali za watanzania, pia angeshaagaa kuona mikataba mibovu kama ya Richmond inayosababisha kupotea kwa fedha za walipa kodi, ikisainiwa na viongozi wa Tanzania ya sasa.

Angesikitika kuona pesa ya malipo ya nje (EPA) inachotwa na viongozi huku wakishirikiana na wafanyabiashara maarufu wakati watanzania wanalala njaa.

Angeshaangaa sana, kuona viongozi wanatumia ofisi za umma kama ngao ya kufanyabiashara huku wakijiita wajasiriamali, jambo ambalo Azimio lake lilikuwa linakataza.

Angewasikitikia watanzania kwa kuzongwa na umasikini unaosababishwa na kuvunjwa kwa Azimio la Arusha na utawala bora.

Pia angeamua kungana na watanzania wote wanaodhulumiwa jasho lao kuamua kuikomboa upya Tanzania ili kulisimika tena Azimio la Arusha litokomeze dhuluma, unyonyaji, ubeberu, ubepari, ufisadi, ukupe na wizi wa pesa za umma.

Watanzania tungeshangilia kuiona tena saa ya ukombozi imefika kwani tumeteseka sana, tumeonewa sana, tumedhulumiwa sana, na tunatamani sana kujikomboa.

Makala haya yameandikwa na Mwananchi mwenye fikra za kimaendeleo anapatikana kwa simu: 0764 992264.

MWISHO.

Nov 24, 2008

Kunyongwa kwa Aleksander kaka yake Lenin ni hisia kubwa ya Lenin kutaka kuikomboa Urusi




Makala
KATIKA suala la kupigania haki za wanyonge kwa wakati mwengine linaweza kujitokeza kwa mtu kutamani kupigania haki za wanyonge kutokana na kuvutiwa na mtu furani ambaye anaonekana kuwa na harakati za kupigania haki ya wanyonge kwa nguvu zote.

Jambo hili lilitokea kwa mwanamapinduzi Mrusi mwenye fikra za kimaeneleo aliyejulikana kwa majina ya Vladimir IIyich Ulyanov (Lenin) ambaye kwa kiasi kikubwa aliathiriwa sana na kaka yake Aleksander ambaye alikuwa ni kijana mwenye nia imara mwenye kushirikilia maongozi mema ya kimaadili katika kuhakikisha wanyonge wanajikomboa.

Lenin alizaliwa Aprili 10 mwaka 1870, katika mji wa Simbirsk (sasa unaitwa Ulyanovsk) ulioko kwenye ng'ambo za mto Volga, na kukulia katika maeneo hayo ya wazi yaliyotanda sana ya mto huo mkuu wa Urusi, katika miji ya Simbirsk, Kazani na Samara.

Babu yake Lenini, N.V. Ulyanov alikuwa ni mkulima wa kitumwa wa Kirusi aliyekuwa akiishi katika Mkoa wa Nizhegorodsky, na katika mwaka 1791 alihamia katika Mkoa wa Astrakhan ambako aliandikiswa kama ni mtu wa tabaka la kati na alikufa katika hali ya umasikini hohehahe.

Baba yake Lenini, IIla Nikolayevich Ulyanov alikumbana na hali ya dhiki ya umasikini mapema sana maishani mwake, kaka yake ndiye aliyemsaidia mpaka akabahatika kupata elimu ya juu. Baada ya kuhitimu Chuo Kikuu cha Kazan baba yake Lenin alianza kufundisha katika shule za sekondari, na baadaye akawa Mkaguzi wa mashule na hatimaye kuwa Mkurugenzi wa shule za serikali katika mkoa wa Simbirsk. Alikuwa mtu mwenye fikra nzuri za kuleta maendeleo ya elimu kwa wananchi wa kawaida.

Mama yake Lenin, Maria Aleksandrovna, alitokana na ukoo wa daktari. Mama huyo alielimishwa nyumbani na akiwa mama hodari sana wa lugha nyingi za kigeni. alijua vyema fasihi na kupenda sana muziki. Alikuwa ni bibi Mwenye nia thabiti na tabia imara, mwenye akili, mtulivu na mwenye bashasha, alikuwa akijishughulisha sana katika kulea wanawe.

Katika ukoo wa Ulyanov kulikuwa na watoto sita ambao ni Anna, Aleksander, Vladimir, Olga, Dmitri na maria. Wazee wao walifanya wawezalo khakkisha watoto wao wanapata elimu ya fani mbalimbali, kuwalea wawe wapenda kazi, waaminifu, wenye adabu njama na wenye kuwafkiria watu wengine.

Kwahiyo Lenin alikulia katika ukoo huu ulioshikamana sana. Alikuwa ni mtoto mweye kuonekana wa furaha kila wakati huku akiwa mchangamfu, akipenda michezo ya hekaheka na ya makelele, kuogelea, kuteleza juu ya barafu na kwenda matembezini pamoja na marafiki wenzake.

Alijifunza kusoma alipokuwa na umri wa miaka mitano na alipotimiza miaka tisa aliingia darasala kwanza katika shule ya Simbirsk, wakati akiwa pale shuleni alisoma kwa hamu kuu akiwa na kipawa cha ajabu na kuyachukulia masomo yake bila mzaha wowote. Alikuwa kila mwaka akimaliza masomo anapata tuzo za hali juu kabisa.

Alikuwa tayari siku zote kuwasaidia wenzake pamoja na kuwafahamisha masomo magumu. katika madarasa ya mwisho ya sekondari aliwasaidia N. M. Okhotnikov, Mchuvash nk kujiandaa na mitihani yao ya kujipatia shahada ya kuhitimu shule.

Lenin mwanamapinduzi wa Urusi alikuwa akipenda sana kusoma na alivutiwa vizuri sana na vitabu vya A. Pushkin, M. Lermontonv, N. Gogol, I. Turgenev, N. Nekrasov, M. Saltykov-Shchedrin na L. Tolstoi. Sehamu kuu ya kisomo chake ilitawaliwa na vitabu vya wademokrati wa kimapinduzi, V Belinski, A. Herzen, N. Dobrolyubov na D .pisarev, pamoja na vitabu hivyo vilivyokuwa vimepigwa marufuku wakati huo. kitabu alichokuwa akikipenda zaidi ni cha N. Chernyshevski akiwa kama mwanchuoni mashuhuri na mpinzani mkali wa utawala wa mfalme na umwinyi.

Tabia na maoni ya Lenin ujanani mwake yalipatikana kutokana taathira ya malezi ya nyumbani, vitabu alivyosoma vya kimaendeleo pamoja na maisha yaliyokuwa yakimzunguka.

Wakati ule ubepari ulikuwa ikikua kwa kasi sana katika Urusi, makarakana na viwanda mbalimbali vilikuwa vikichipuka na kuajili wafanyakazi wengi ambao walikuwa wakinyonywa na kukandamizwa sana kitendo ambacho kilipelekea hali ya wafanyakazi hao kuwa mbaya sana kwani udhalimu wa serikali ya mfalme, mukandamizo wa makabaila, umasikini na unyonge wa wafanyakazi na wakulima yote haya yalimufanya lenin kuwa chukia wanyonyaji.

Lenin aliathiriwa sana na fikra za kaka yake, Aleksander ambaye alikuwa ni kijana mwenye nia imara ya kuhakikisha anaikomboa urusi kutoka katika tabaka wa wanyonyaji. "Mfano wa kaka yake kipenzi ulikuwa ni muhimu sana kwa Lenin," anasimulia Anna Ulyyanov dada yake Lenin, na kuongeza kuwa, tangu utotoni alijaribu kumwigiza kaka yake kwa kila jambo, aulizwapo atakuwa nani katika maisha yake, jibu lake lilikuwa: "Kama kaka yangu nimpendaye Aleksander"

Aleksander alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. Petersburg na alikuwa na lengo kuu katika maisha yake la kuendesha mapambano ya kimapinduzi dhidi ya utawala wa kinyonyaji wa mfalme na kuupigania umma upate maisha mazuri.

Aleksander alikuwa akielekea katika mfumo wa Mwanaharakati wa kijamaa Karl Marx katika kuhakikisha umma unajikomboa kutoka kwa utawala wa kiunyonyaji wa mfalme, ilikuwa ni kutokana na kaka yake Aleksander ndivyo Lenin alipotambua kwa mara yake ya kwanza juu ya maandishi yafuatayo maongozo ya Marx.

Lenin alikubwa na mikasa mikali ya maisha wakati akiwa kijana mdogo kutokana na kufiwa na baba yake ghafla mnamo mwaka 1886, na mara ukoo huo haujafarijika kutokana na pigo hilo mara ghafla tena msiba mwingine wa kaka yake Aleksander ukaanguka.

Msiba wa kaka yake Aleksander ulitokana na mnamo Marchi 1887 Aleksander alikamatwa mjini St. Petersgurg akikabiliwa na shtaka la kuhusika na jaribio la kutaka kumuua mfalme Aleksander III, na katika Mei, mwaka huo huo Aleksander alinyongwa katika Ngome ya Schelisselburg. "Aleksander Ulyaniov amekufa shahidi" aliandika Anna, dada yake na kuongeza kuwa "roho yake iliyotolewa mhanga imekuwa kama mwenge wa kimapinduzi uliomwangazia njia ndugu yake, Lenin."

Kunyongwa kwa kaka yake kulikuwa ni pigo kubwa sana kwa Lenin na kuthibitishia moyoni nia yake ya kuyatoa mhanga maisha yake kwa mapambano ya kimapinduzi katika kuhakikisha anaikomboa Urusi kutoka katika unyonyaji. Pamoja na hayo Lenin aliona fahari kubwa kwa kaka yake kujitoa mhanga kwa kupigania wanyonge hapo ndipo alijawa na fikra za kuhakikisha anaikomboa urusi kama kaka yake alivyodhamilia kufanya.

Kutokana na Machungu ya kaka yake lenin akaamua kutafuta njia ya kufuata fikra za kaka yake katika kuhakikisha anaikomboa urusi, katika kujitayalisha kwa mapinduzi hayo kijana huyo alikuwa na hamu sana ya kujifunza elimu za kijamii. Katika Agosti 1887, baada ya kuhitimu elimu ya sekondari pamoja na kutuzwa nishani ya dhahabu, aliingia katika Chuo kikuu cha Kazan akichukua fani ya sheria hiyo no mojawapo ya njia za kuelekea kuikomboa urusi kwa kufuata njia za kaka yake kipenzi Aleksander.

Katika Chuo Kikuu Lenin Ulynov akaaza kuingiliana na wanachuo wa kimaendeleo, wenye fikra za kimapinduzi. Mwanzoni mwa Desemba 1887 alifukuzwa katika Chuo hicho kwa kushiriki katika mkutano wa wanafunzi akisisitiza mapinduzi ya wanyonge. Baadaye Lenin alihadithia mazungumzo aliyokuwa akizungumza na afisa wa polisi aliyekuwa akimuongoza kwenda gerezani: "Ina maana gani kufanya uasi, kijana?" Afisa huyo alimuuliza na kuongeza: "Kwani huoni kuna ukuta mbele yako?" Ndiyo" Lenin alijibu na kuendelea: "lakini ukuta wenyewe umeoza kabisa, ukiusukuma kidogo tu unaanguka." Haya yalikuwa majibu ya Lenin kwa kujiamini ikijua kuwa ipo siku ukombozi wa wanyonge utaangusha ukuta wa unyonyaji.


Lenin alifungwa kifungo ambapo katika kifungo chake alikuwa anahamishiwa katika sehemu mbalimbali ambapo ilifikia hatua akahamishiwa katika kijiji cha Kokushkino (sasa unaitwa Lenino), Mkoa wa Kazan huku akiendelea kuwa chini ya ulinzi, wakati akiwa huko alitumia muda mwingi sana kumkumbuka mwongozo wa fikra za kaka yake za kukomboa wanyonge kutoka katika kunyonywa.

Vilevile alitumia muda wake kusoma na kujielimisha zaidi, alihathia "Nadhani sijawahi kusoma na kujielisha katika maisha yangu, hata wakati nilipokuwa gerezani St. Petersberg na huko Siberia, sijawahi kusoma kama nilivyosoma wakati nikiwa katika kijiji cha Kokushkino" alisimulia Lenin na kuongeza: "Nikiwa katika kijiji hicho nilisoma na kumbuka Aleksander kwa kwa kupania mno yaani kutoka alfajiri hadi usiku wa manane."

Basi katika umri wa miaka kumi na saba kijana Lenin alikuwa ameshashika njia ya kaka yake Aleksander ya mapambano ya kimapinduzi dhidi ya utawala wa mfalme.

Makala haya yameandaliwa kutoka katika mitandao na vyanzo vya habari mbalimbali.

Nipigie: +255 764 992264

Nov 2, 2008

Migomo na Maandamano siku hizi Tz hapakaliki




CHAMA cha Wafanyakazi ni umoja wajumuiya ya wafanyakazi katika sekta yoyote iliyohalali na inayofanya kazi kulingana na taratibu za nchi, kwahiyo chama ni kama raia nchini aliye na haki ya kujipatia mali au haki yake, vilevile kutetea haki zake mbele ya baraza na kulindwa na sheria ya nchi.
Vile vile Chama kinauwezo wa kugoma, kuishtaki serikali, kampuni, taasisi au mwajili yoyote iwapo kitafuata misingi inayokubalika katika kudai haki yake, vilevile chama kama chama kinaweza kushitakiwa kama kitavunja kanuni na sheria zinazotakiwa.
Huko wingereza vyama hivyo vilijulikana kwa jina la "Trade Unions" , katika miaka ya 1835 ndipo vyama vidogovidogo vilipojiunga huko kuko wingereza na kufanya umoja wa vyama uliojulika kama "Grand National Consolodated Trade Unions" vikiwa na lengo moja la kudai haki za wafanyakazi.
Kwahiyo umoja huo mkubwa uliwatisha sana Wamiliki wa viwanda, serikali pamoja na matajiri wa huko ambapo kwa kuhofia nao waliamua kukishambulia vyama hivyo katika Baraza Kuu, ili kuvidhofisha na waendelee kuwanyonya wafanyakazi pasipo kuwa na ngao yoyote ya kujilinda.

Katika mashambulizi hayo ambayo yalipelekea kudhofisha vyama hivyo na kukoswa nguvu mnamo mwaka 1865 hatimaye yalitokea matata ya watu katika miji ya Sheffield na Manchester kati ya wafanyakazi na matajiri wao, ambapo ilipelekea serikali kuchukua jukumu la kuchunguza juu ya mtafaruku huo ambapo serikali baada ya kumaliza uchunguzi wake ilitangaza sheria mpya mwaka 1875 ambayo ilijulikana kama Hati au Mkataba wa vyama vya wafanyakazi huko wingereza.

Huo ndio ukawa ndio msingi wa sheria wa vyama vya watu wa kazi huko wingereza na katika nchi zilizo kuwa chini ya Dola ya Kiingereza. Katika sheria hiyo ugomaji uliruhusiwa na wanachama wa vyama hivyo waliruhusiwa kuwashawishi wenzao nao wagome kwa kuzingatia sheria na kanuni za ugomaji.
Na sasa katika karne hii vyama vya wafanyakazi ni vyama vilivyo halali kabisa katika nchi zote zilizo huru na katika kila nchi vyama vya wafanyakazi vya sekta mbalimbali zinaendelea kutetea haki za wafanyakazi ili kuondokana na kuonewa au kunyanyaswa na waajiri wao.
Katika nchi yetu Tanzania tuna vyama vya wafanyakazi vingi sana na vimesajiliwa kihalali vikiwa na lengo la kutetea maslahi ya wafanyakazi wa sekta husika, lakini pamoja na haya vyama hivyo vimekuwa vikitekeleza majukumu yao ya kulinda haki, amani utulivu wa wanachama hapa nchini kama inavyotakiwa.

Pamoja na utekelezaji wa haki hizo hivi karibuni Chama Cha Walimu Tanzania (CCW) kilitangaza kugoma nchi zima na mgomo huo ungefanyika oktoba 15 mwaka huu lakini kutokana na serikali kuhofia kuwa mgomo huo ungeleta hasara kubwa kwa taifa iliamua kwenda mahakamani kupinga mgomo huo ambapo mahaka kweli iliupinga mgomo huo.
Lakini siku ambayo walimu walitangaziwa kuwa mgomo wao umesitiswa pale katika viwanja vya Karimujee walipandwa na hasira kubwa mno ninaimani kila mtu alisikiana na kuona kwenye vyombo vya habari vulugu viliyokuwepo hapo Karimjee ambapo siku hiyo ilikuwa pia ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha baba wa taifa kwa walimu siku hiyo ilikuwa ni siku ya majonzi na huzuni.
Baadhi ya walimu walilia kwa machungu makubwa utadhani ni watoto wadogo hakika mimi ambaye nilikuwa pale nikichukua habari nilipatwa na uchungu wa huruma kubwa sana kwa walimu wangu ambao walinifundisha mpaka kufikia hatua hii niliyonayo kuwaona wakilia hadhalani huku watoto wao wakiwaangalia.
Niliwahurumia walimu wangu kwa kukataliwa kufanya mgomo ambapo tunajua kabisa kuwa mgomo ni mojawapo wa njia ya kufikisha ujumbe ulidaiwa kwa siku nyingi bila mafanikio, lakimi baadhi ya walimu walitangaza kuwa wataendelea na mgomo baridi wa kutoingia madarasani na kama walimu wakuu watawalazimisha kuingia madarasani watawafundisha wanafunzi uongo.
Sasa serikali yetu mbona mpaka sasa hatujasikia kuwa walimu wetu wameshaanza kulipwa mafao yao? Si mulisema kuwa haichukui siku chache suala lao litakuwa limeshughulikiwa? Au munataka tena watangaze kugoma tena kwa kutokwenda shule tofauti na sasa ambapo wamefanya mgomo baridi wa kufundisha uongo.
Sisi watanzania bado tunajua kuwa hawa walimu bado wamegoma kwa kutumia mgomo baridi wa kufundisha uongo kwani serikali haijatueleza kama imefanya utafiti na kubaini kuwa walimu wetu sasa wanafundisha ukweli!
Tunajua watoto wetu bado wanafundishwa uongo kwa sababu walimu walisema watafundisha uongo mpaka hapo serikali itakapolipa mafao yao na serikali mpaka sasa haijalipa mafao yao.
Wazazi tunahofu kushindwa kufaulu kwa watoto wetu katika mitihani yao kwa sababu serikali haitaki kulipa mafao ya walimu ili watoto wetu wafundishi ukweli tunasikitika sana kwa kupuuzia suala zito kama hili au kwa sababu watoto wenu wako shule za kimataifa na wengine wako Marekani na Wingereza ndio maana hamjari watoto wetu sisi masikini. Munaona sawa tu waendelee kufundishwa uongo watoto wetu.
Kama Mwalimu mmoja aliyesema pale karimujee kuwa kama wakuu wao watawalazimisha kuingia madarasani watafundisha 1+1=0 na hesabu za mlinganyo watafundisha kama hesabu za majira ya nukita, hanuoni kuwa tunakoelekea ni kuua fikra za watoto na kuzalisha rasilimali watu ambao hawaendani na kazi wanazozifanya?

Si hayo tu hata walimu wanaweza kutafuta njia nyingine ya kudai haki yao kwani kule wingereza kipindi cha wafanyakazi kunyanyaswa kwa kunyimwa mafao yao, wafanyakazi hao walitafuta njia nyingine ya kudai haki yao ambapo wafanyakazi wa viwandani waliamua kuvunja vunja vifaa vya viwandani zikiwemo mashini na baadhi ya majengo na wengine waliamua kuweka chunvi katika mashine ili vioze ambapo mapambano haya yalijulikana kama “Luddism movement” 1811.Mapambano haya ya Luddism yalilitia hasa kubwa sanaTaifa la wingereza na kupelekea kushuka kiuchumi.
Sasa walimu wakiamua kutafuta haki yao kwa njia nyingine ambayo itakuwa ya hasara zaidi ya kugoma hapo mutasemaje? Wakiamua kufanya kama Luddism ya wingereza hapo mutasemaje?
Chondechonde tunawaomba walipeni walimu wetu mafao yao ili watoto wetu wasifundiswe uongo na kunusuru kutokea kwa mgomo mwengine wenye aina kama Luddism ya wingereza kwani hasara itakayopatika ni hasara ya watanzania wote kwani ndio walipa kodi ya maendeleo ya Taifa.
Ukipenda nipigie: +255 764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com

Taifa linaangamia taratibu chukua hatua




SALAAM Rais wangu Jakaya Mrisho Kikwete, nakusalimia ewe mtukuka mwenye nyingi rehema, mwenye upendo na nchi yako na watanzania wote hakika unaupendo mkubwa na nchi yako ndiyo maana huachi kufanya ziara kuizungukia nchi yakoTanzania kila sehemu ili kujua hari ya watu wako mlezi wa Tanzania na juzijuzi ulikuwa Mbeya, haya yote ni kutokana na kuipenda nchi yako.

Nchi yako Tanzania nayo Mungu ameijalia sana kwani rasilimali za kila aina vyote ameipatia, Tanzania tuna madini ya kila aina yakiwemo dhahabu, almasi, ulanga, Tanzanite n.k.

Vilevile ina maziwa na mito ya maji ya kila aina likiwemo ziwa vicktoria ambalo linazalisha samaki aina ya sangara kwa wingi ambao wakazi wa kanda ya ziwa wanapata Mapanki kwa ajili ya kutumia kama mboga kwani minofu yote huwa inachukuliwa na wawekezaji tuliowapa wachukue ili watupatie pesa za kigeni kwa maendeleo ya taifa letu.

Pamoja na hayo vilevile nchi yako Mheshimiwa Rais ina Milima mingi ukiwemo Mlima Kilimanjaro ambao ni Mlima mrefu kuzidi Milima yote Afrika, Mlima huu huwa unatuingizia pesa nyingi za kigeni yote haya ni kutokana na Mungu kuijalia nchi yako Tanzania.

Rais wangu Tanzania yako ina rasilimali nyingi sana ambazo na sisi watanzania tunazitumia ili kujiletea maendeleo pamoja na kwamba wawekezaji ndio wamechukua sehemu kubwa ya rasilimali zetu lakini yote haya ni kuhakikisha taifa linapiga hatua kimaendeleo.

Rais wangu Jakaya nakupa pole sana kwa Masaibu yaliyokukuta kwani tangia ukumbwe na kimbunga cha kuzomewa na kurushiwa mawe huko Mbeya sijakusalimia na kukupa pole baba mlenzi, mtetezi wa wanyonge.

Pole sana Mtukufu mlezi wa rasilimali za taifa kwa manufaa ya kizazi kijacho hakika wewe ni Mkombozi wa Tanzania ndio maana tulikupa kura kwa asilimia kubwa huku tukishangilia kuwa wewe ni chaguo la Mungu.

Yawezekana na Mungu alikujua kuwa wewe ndiye utakuja kuwatetea Watanzania kuondokana na dhuluma, unyonyaji, na kukomesha ufisadi ndani ya nchi yako mpaka kipindi cha miaka yako mitano itakapoisha ili kuingia tena uchaguzi mwingine wa hapo mwaka 2010 ambapo pia ungemalizia yaliyobakia.

Nakupa pole Rais wangu kutokana na matukio yanayoiandama serikali yako kwa sasa ni ya kusikitisha mno kwa sababu yanaashiria kuwa nchi yako Rais wangu ipo kwenye dimbi la hatari kuelekaea katika hari isiyo ya kawada kwani fikra za watu na hisia zao wameanza kuzionyesha hadharani sijui ni kwanini wanapata msukumu huu mpaka wa kuamua kukurushia mawe Rais wangu na kufanya Migomo ya kila aina?

Rais wangu yakupasa kufikiria kwa kina jambo hili la kurushiwa mawe wakati ukiwa katika ziara yako Mkoani Mbeya kwanini watu wa huko walidhubutu kukurushia mawe? Hapa kuna kitu ambacho unatakiwa kukitambua mapema ili kukipatia ufumbuzi kwa haraka zaidi kwani kitendo cha kukuzomea na kukurushia mawe ni nguvu ya fikra ya watu hao ya kufikria kuwa hujawatendea kitu fulani ambacho ulitakiwa kukitekeleza.

Sasa baada ya kuona kuwa haki yao hawapati japo kuwa ile haki wanaijua kuwa ni yao kihalali sasa ili kufikisha ujumbe wa hisia za fikra zao wakaamua kukuzomea na kurusha mawe ili ujue kuwa hujawapatia kile walichokuwa wanakitaka.

Nikiwa kule Mbeya kama kawaida yangu ya kuchukua habari ili nihabarishe umma wa Watanzania wenzagu wenye nia ya kujua matukio yanayotokea katika dunia hii nilibahatika kushuhudia kuzomewa kwa Rais Kikwete katika maeneo ya Mwanjelwa, katika maeneo hayo wananchi walipouona msafara wa wake walitanda barabarani kuuzuia msafara huo wa Rais wakimtaka azunguze nao.

Lakini alipojitokeza wananchi walianza kupiga kelele wakizungumzia ufisadi huku wakisema kwa nini Rais hashughulikii mafisadi mbalimbali wakiwemo wa EPA wakati aliapa kuwa atailinda na kuitetea katiba ya nchi? Na baadhi ya watu wakihoji kuhusiana ahadi alizotoa za kuwapatia ajira na maisha bora.

Na katika kijiji cha Kanga Wilayani Chunya tukio la kurushiwa mawe msafara wake ni jambo ambalo halisitahili na la kushangaza, lakini Rais wangu alichukulia kama jambo dogo na kumtaka Mkuu wa Mbeya John Mwakipesile ambaye alionekana kufadhisha sana na jambo hilo kwa kumwambia kuwa, asifadhaike sana kwani yeye Rais watu wa Mbeya wanampenda sana.

Rais jambo hili ni jambo zito kwani wananchi hawa kuamua kukurushia mawe huku wakidai ajira na maisha bora ni dhahili kuwa hujawaletea hayo maisha bora, ajira pamoja na kutekeleza kulitetea taifa lako kwa kushughulikia Mafisadi ili kuondoa umasikini iliokidhili kwa kila jamii.

Kwahiyo baada ya kuona maisha yao yanaendelea kudidimia huku wakiumia katika dimbi kubwa la umasikini wa kulala njaa na kuvaa nguo chakavu na zilizochanika kwa kukoswa pesa za kununua nguo mpya na chakula, wakamua kufanya jambo kama hilo ambalo halikutakiwa kutendeka.

Nakupa pole sana kwa misukosuko inayokupata katika uongozi wako Rais wangu, kwani uongozi wako umekuwa na misukosuko kila wakati tukiangalia misukosuko mingine tofauti na kurushiwa mawe na kuzomewa kule Mbeya.

Tunaona tangia watanzania tukukabidhi madaraka misukosuko imekuandama sana! Tulishuhudia kuvunjika kwa Baraza la Mawaziri kutokana na kujihudhuru kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowasa kwa kashifa ya Mkataba feki wa Richmond uliosababisha pesa ya walipa kodi kupotea bure.

Mara tu baada ya Richmond tukaona suala EPA nalo likaibuka ambalo lilisababisha pesa zetu kuchotwa pale benki kuu, Ndani ya utawala wako tu tumeshuhudia Zanzimbar iliyokuwa imara hapo zamani sasa inataka kujitenga.

Misukosuko inakuandama mara Madaktari kugoma wakidai nyongeza za mishahara, Wanafunzi wa vyuo vikuu kila wakati wanagoma wakidai hawatendewi haki mambo haya yote tumeyashuhudia, misukosuko inazidi kuendelea mara walimu kugoma wakidai malipo ya posho zao mpaka wanaamua kurusha mawe huku wakitoa machozi kama watoto wadogo kwa uchungu mkubwa.

Wazee wa walikuwa wa Wafanyakazi wa iliyokuwa Afirika Mashariki nao wanadai mafao yao ambayo bado wanaendelea kuzungushwa serikali yako, nao wanaamua kuzimalizia hisia zao kwa kumfungia Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi kwa hasira kali ya kuonyesha liwapo na liwe.
Jambo ambalo wazee hao wamelitoa juzijuzi katika viwanja vya Mnazi Mmoja Watanzania tunasononoka sana kwani katika viwanja hivyo wazee walisema kutokana na serika kushindwa kuwalipa mafao yao, sasa wamepanga kutoa pigo kali takatifu kwa serikali ambalo pigo hilo halitasahaulika daima! Japo kuwa hawa wazee walikataa kulitaja hilo pigo kwa waandishi wa habari wakidai kuwa serikali imekuwa ikipangua mipango yao wakiitaja, lakini hili pigo walisisitiza litakuwa la aina yake kwani serikali hata ifuatilie kwa aina gani haitagundua, bali itashutukia tu inapata pigo hilo takatifu.
Jamani watanzania tunashindwa kujua hili pigo takatifu ambalo serikali haitasahau litakuwa la namna gani? Lakini yote haya ni hasira ya wazee wale kunyimwa haki ya mafao yao wakati wakiona mafisadi wakiendelea kutanua na pesa za walipa kodi huku wakikumbatiwa na serikali kama vifaranga vya kuku.

Haya machache niliyoyatanja ni ishara tosha kabisa Rais wangu kuwa nchi yako inaelekea katika machafuko ambayo mwisho wake ni kuanguka kwa taifa la Tanzania.

Ukipenda nipigie: +255 764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com

Oct 20, 2008

Nani ataikomboa upya Tanzania?

SIKUTAKA kuandika juu ya Ujamaa tena katika maisha yangu lakini baada ya kukaa na kufikiria kwa kina zaidi nikaona nitakuwa siwatendei haki Watanzania wenzangu ambao walifaidika na ujamaa katika kipindi cha Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hasa katika kuondoa unyonyaji, dhuluma na ubaguzi yakiwemo mafisadi, katika kipindi hicho ujamaa ulitumia itikadi za kijamaa za kuunganisha watu kwa pamoja katika kufanyakazi na kama mtu ataonekan hafanyi kazi ujamaa ulimuona mtu huyo kama kupe anayeishi kwa kunyonya jasho la wengine.

Pia nikaona kama nitaacha kuzungumuzia Ujamaa nitakuwa simutendei haki Baba yetu wa Taifa ambaye alikuwa Mwazilishi wa huo Ujamaa ndani ya Azimio la Arusha. Ili kumuenzi Mwalimu baba wa Taifa aliyeondoa unyonyaji kwa kutumia hilo Azimio la Arusha ambalo lilikuwa na hiyo siasa ya Ujamaa sikuona sababau ya kuacha kabisa kulizungumzia Azimio la Arusha na siasa yake ya ujamaa.

Kitu ambacho kilitaka kunisababisha nisizungumzie Ujamaa tena ni ile kauli ya Rais wangu Jakaya Mrisho Kikwete niliyoisoma katika gazeti moja la kila siku toleo la jumapili kuwa Mheshimiwa Rais wangu wakati akifanyiwa mahojiano na shirika la habari moja, Mwandishi wa shirika hilo alimuuliza swali kuwa anaizungumuziaje kuhusiana na nchi yake ni ya kijamaa? na anazungumuziaje ujamaa katika nchi yake? katika jibu lake Rais wangu alisema Siasa ya ijamaa katika nchi yake iwapo mtu yoyote atazungumuzia ujamaa ataonekana kama Mwendawazimu!!

Siku hiyo niliposoma hiyo habari nilishutuka sana na nikaa kufikiria kama kweli Mheshimiwa anaweza kusema kitu kama hicho kuwa mtu akizungumzia ujamaa ataonekana Mwendawazimu! Baada ya kufikiria nikahoji mimi mwenyewe ataonekanaje mwendawazimu wakati huyo viongozi wetu akiwemo Mh. Rais wangu wanasisitiza kumuenzi baba wa Taifa na kazi alizozifanya ikiwemo na ujamaa?


Pamoja na kuhoji hivyo lakini hakiri yangu ikachukua jukumu la kuamua kuacha kabisa kulizungumuzia Azimio la Arusha na siasa yake ya Ujamaa na Kujitegemea kwani nilifikiri nikiendelea kuzungumuzia mambo haya nitaonekana kama Mwendawazimu!! na ili nionekane mimi ni Mwerevu basi nisizungumzie kabisa hili Azimio la Arusha na Utawala wake ambao ulituletea matumaini na faida kubwa sana Watanzania enzi za Mwalimu Nyerere kwa kuwa ulitokomeza na kudhibiti wanyonyaji,wadhulumaji na wahujumu ambapo sasa ni maarufu kwa jina mafisadi.

Lakini tangia niamue kuacha kuuzumgumuzia huu ujamaa nimekuwa nikijiouna ninazidi kuwa mjinga na ujinga ndio unaongezeka kwani nimekuwa nikisahau kabisa kumuenzi baba yetu wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pamoja na utawala wake ambao ulikuwa wa haki kwa kila Mtanzania.

Baada ya kukaa kimya huku nikifukria nikagundua kuwa kumbe kuzungumuzia ujamaa wa Mwalimu ni kujinyima haki yangu ya kumuenzi baba wa Taifa, hapo ndipo nikapata akiri kuwa kumbe nilipochukua jukumu la kuacha kuzungumuzia ujamaa ni sawa na kumunyima haki yake Mwalimu ya kumuenzi pia ni mojawapo ya kuwanyima haki watanzania wengine kujua mambo ambayo yalifanya na ujamaa kwa manufaa ya watanzania.

Baada ya kugundua hayo nikaamua hata kama waniite Mwendawazimu lazima kila sehemu ninapopita nitalizungumuza na kuhubiri misingi ya Azimio la Arusha na siasa zake za ujamaa na kujitegemea mbazo zilitusaidia watazania kufaidi raslimali zetu wenyewe kwani zilileta neema kubwa kwa watanzania wote.

Mwalimu bila hiana aliona kuwa mambo ya ya ufasadi yangetokea katika Taifa letu, aliona dhuluma ingetawala katika jamii, aliona unyonyaji ungekuwa ndio mfumo tawala katika taifa letu, aliona ubaguzi ungekuwa utamaduni ulitawala katika Taifa letu, aliona umma wa watanzania utakuja kushindwa kutumia raslimali zake kwa manufaa yao, hapo Mwalimu ndio aliona ili kujikinga na mambo haya aazishe Azimio la Arusha na misingi yake ya utawala bora.

Azimio hilo likawa na misingi madhubuti ya kutoruhusu kiongozi yoyote kujitwalia pesa ya umma kwa manufaa yake. Kwa leo nitaongelea zaidi faida za ujamaa ambao nilikuwa nimeamua nisiuhubiri kwa kuhofia kuitwa Mwendawazimu.

Tunajua kabisa ujamaa ulitokana na Azimio la Arusha ukiwa kama mojawapo ya siasa ambazo zilitakiwa kila mtanzania azifuate na kwa matendo na imani ili kujikomboa kiuchumi, kifikra, kiutumwa n.k.

Mwalimu aliweka kanuni za siasa ya ujamaa katika Azimio la Arusha ili kuweza kuwawezesha watanzania kuwa wajamaa, waishi kijamaa kwa kufanya kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo kwa pamoja pasipo kubaguana.

Ujamaa wa Mwalimu ulikataa ubaguzi wa mtu na mtu ndani ya jamii ukimanisha kuwa binadamu wote ni sawa na ndugu, kwahiyo hakuna binadamu ambaye yuko juu ya mwezake, hakuna binadamu ambayo anatakiwa kumiliki mali za Taifa na mwingine kutomiliki, ujamaa ulikuwa na na misingi ya kutokomeza unyonyaji kwa kuwafahamisha watanzania kuwa hakuna mtu ambaye anatakiwa kufanya kazi kwani ulibainisha kuwa misingi ya ujamaa ni kufanyakazi kwa pamoja na haukuruhusu kiongozi yoyote kujichotea pesa ya umma sehemu yoyote iwe benki kuu au sehemu yoyote kwani pesa hiyo ilihesabiuka kuwa ni pesa ya kila mtu yaani ya kijamaa kwa ajili ya maendeleo ya wajamaa.

Ujamaa haukuruhusu dhuluma katika sehemu yoyote kwani ulisisitiza kila mtu lazima afanye kazi kwa nguvu zake zote na nia yake yote, ili kuleta maendeleo ya Taifa, vilevile ndani ya siasa ya ujamaa dhuluma ilihesabika kama ni dhambi ambayo ilipaswa kukemewa na kila Mjamaa.

Ujamaa wa Mwalimu ulisisitiza watu kushikamana kwa pamoja bila kubaguana ndio maana ulikuwa ukiendana na maadamano mbalimbali ya mishikamano hasa watu wa kijijini bila shaka watakuwa wanayakumbuka maandamano hayo ambapo watu walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali zikiwemo za kujivunia ujamaa kuwezesha kuleta itikadi ya kukomesha unyonyaji, na kuondoa fisikoko waliozoea dhuluma bila kujishughulisha.

Ujamaa wa Mwalimu ulileta vijiji vya ujamaa ndani ya jamii watu waliondolewa katika makazi ya porini na kuhamishiwa katika sehemu moja na kuuda kijiji kimoja ulifanya hivyo ukiwa na lengo la kusisitiza mushikamano wa kuishi kijamaa na ulitaka huduma za kijamii zimufikie kila mtu kwa pamoja pasipo kumuhudumia wa sehemu moja na kuacha wa sehemu nyingine.

Katika kulitekeleza hili Mwalimu alihakikisha watu waliokuwa katika sehemu hiyo moja ya kijiji wanapata huduma za kijamii zikiwemo shule, zahanati, mpembejeo, ghara za kutunzia nafaka zao, sehemu ya karibu ya kuuzia mazao yao na huduma nyingine nyingi kwa pamoja.

Katika vijiji vya ujamaa ili kuinua zaidi kilimo Mwalimu aliamua kila kijiji cha ujamaa kipewe Makisai na majembe ya kukokotwa na Ng'ombe ambayo yalikuwa yakitumika kulimia katika mashamba yao ya ujamaa na wakipata mazao wanauza katika sehemu hizo husika.

Hakika katika ujamaa kulikuwa na faida nyingi sana ambazo zingine sitaweza hata kuzitaja kwani kitamaliza sehemu yote ya gazeti hili na kwa ajili ya faida hizi hata kama muniite Mwendawazimu kwa kuzungumuzia ujamaa wa Mwalimu niitine tu, na ninawahakikisheni ya kuwa sitaacha kumuenzi Mwalimu kwa kazi yake kubwa aliyoifanya kama hii ya kuanzisha siasa ya ujamaa wenye misingi ya kutoruhusu mtu kunyonywa jasho la nguvu zake.

Ninaimani kabisa ujamaa ulioleta fikra ya usawa ndani ya jamii mpaka leo hatuna ukabira hata kidogo ukikaa kwa wagogo wewe msukuma kama mimi unaoneka ni Mjamaa kama wao kwahiyo utapatiwa kila kitu, ikienda kwa kwa Wanyantuzu wewe ni Mkwele utapokelewa vizuri na wala hutabaguliwa hata kidogo kama huduma zote utapata yote haya ni kwa sababu ya fikra za Mwalimu za ujamaa za kumdhamini mtu hata kama katoka wapi kama unakitu mugawane sawa ndio fikra za kiujamaa ambazo zilikataa unafiki.

Na mpaka hapo mimi sione sababu za kuona kuwa ukizungumzia ujamaa utaonekana kama ni Mwedawazimu. Kama kweli ujamaa ni mwendawazimu kwani ulileta hasara gani kwa umma wa Watanzania? kwani kuwahamisha watu kutoka sehemu walizo kuwa wanaishi ili huduma za kijamii ziwafikie kwa pamoja ni jambo baya? Kuondoa ubaguzi kwa kuwaunganisha watu katika sehemu mbalimbali ili waishi kijamaa ni jambo baya? kusisitiza watu wafanye kazi kwa pamoja ni jambo ili kujikomboa kimaendeleo pasipokutegemea wawekezaji nalo ni jambo baya? Hakika sione hatia ya ujamaa! na sione kosa alilolifanya Mwalimu katika kuanzisha ujamaa!

Huu mfumo ambao umetawala wa ubepari faida zake kwa watanzania mbona hatuzijui? Sasa tunaona mali zetu watanzania zinamilikiwa na wachche huku watanzania walio wengi wanahangaika kwenye ndimbwi la umasikini kitendo ambacho mongozo wa ujamaa ulikuwa hautaki hata kidogo. Wachache wanaotumia nguvu ya pesa zao ndio wanaoendelea kujitwalia sehemu ya raslimali zetu huku watanzania masikini wakiendele kunyanyasika, kuteseka na kushinda njaa huku wakikumbuka mtetezi wa wanyonge Azimio la Arusha na siasa yake ya Ujamaa.

Wawekezaji nao wanachukua raslimali zetu kwa bei poa kwa mfano hayo madini yetu asilimia 97 yote wanachukuwa wao na kupeleka kwao ughaibuni huku sisi wazalendo wakitubakishia asilimia 3 tu ambayo ukilinganisha na udhamani wa madini yetu ni sawa na tunawapa bure.

Ujamaa ulipinga mtu kujimilikisha kitu au kumiliki kitu pekee yake kwa manufaa yake peke yake (binafsi) bali mtu alitakiwa kila kitu ni cha umma hakuna mwenye nacho lakini sasa umilikishaji binafisi umetufanya Watanzania wengi waliomasikini kukoswa haki yetu ya kumiliki, kama umma wa watanzania sasa uchumi wote wanamiliki wachache wenye pesa zao huku Watanzania masikini hawana kitu wanalia na umasikini wa kushinda njaa kila siku, kumbukeni hakuna kitu kibaya maishani kama kuishi kwenye nchi yako lakini uchumi wa nchi hiyo unakuwa siyo wako hii ni sawa na utumwa.

Kumbe sasa tumewagundua hila zao kwa Mwalimu za kulivunja Azimio la Arusha na misingi yake ya utawala bora! Hila hizi kumbe walikuwa hawautaki ujamaa kwa sababu ni Mwendawazimu. Sasa nianawauliza wakati Mwalimu yupo mbona hamukusema kuwa ujamaa ni uendawazimwi? Mbona Rais wangu Kikwete anamuzalilisha Mwalimu kwa kuita mfumo wake wa uongozi ni uendawazimu?
Hakika mimi ninapata hasira ninaposikia Mwalimu baba wa Taifa anaenziwa kwa matusi ya aina hiyo! Jamani hizi za kuita ujamaa uendawazimu si ni laana kubwa mno? Mbona munatuingiza kwenye laana kubwa namna hii? Acheni hizo kama mumechoka kutuongoza si bora mukajihudhulu kuliko kuanza kutoa matusi kwa Mwasisi wa Taifa letu! Tahadhali kuanzia sasa mukome kututukania Mwalimu wetu kama mulikuwa hamumupendi sisi tunampenda sana.
Na ninamalizia kwa kusema kuwa laiti kama Mwalimu Nyerere angekuja kuishi na Watanzania tena, angeamua kuikomboa Tanzania upya, kwani angesikitika kuona ujamaa wake aliouleta kwa ajili ya kuikomboa Tanzania na kutokomeza unyonyanyi ubaguzi na dhuluma unafananishwa na Mwendawazimu huku maisha aliyoyataka Watanania kuyafuata ili waishi kwa usawa na haki hayafutwi tena.

Angeikomboa upya Tanzania kwani asingevumilia kuona watanzania wanaendelea kuishi katika umasikini huku baadhi ya wachache wanaishi maisha ya kifahari kutokana na kuwawadhulumu haki ya rasilimali zao. Pia angeshangaa kuona ubepari ambao alikuwa anaupinga vita kali sana katika kanuni za Azimio la Arusha sasa ndio umekuwa Mfalme wa Tanzania.
Ni mimi mwendawazimu nipigie: 0764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com
Kwa taarifa zaidi niblogu: http://www.fitalutonja.blogspot.com/

Oct 10, 2008

Uhuru wa habari ni haki ya kila mtu

Huyu hapa ni Mtangazaji mwanamke wa kwanza wa idhaa ya kiswahili BBC anaitwa Zayana Self, hapo akiwa na Watangazaji wengine wa idhaa hiyo, Mwanamke huyu alikuwa mojawapo wa watangazaji wanavuti katika idhaa hiyo.

Uhuru wa Habari ni haki ya kila mtu

Mtangazaji David wa idhaa ya kiswahili BBC enzi hizo alikuwa akitangaza kwa aina ya mvuti wa pekee kila mtu aliyemsikiliza hakutaka hata kuzima radio yake kwa kwa sauti yake ambayo ilikuwa ikimvutia kila mtu, lakini baada ya kufanya kazi huko Uingereza baadae aliamua kurudi Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo sasa hivi ni TBC Taifa.

Habari ni kioo cha Jamii