Oct 10, 2008

Uhuru wa habari ni haki ya kila mtu

Huyu hapa ni Mtangazaji mwanamke wa kwanza wa idhaa ya kiswahili BBC anaitwa Zayana Self, hapo akiwa na Watangazaji wengine wa idhaa hiyo, Mwanamke huyu alikuwa mojawapo wa watangazaji wanavuti katika idhaa hiyo.

Uhuru wa Habari ni haki ya kila mtu

Mtangazaji David wa idhaa ya kiswahili BBC enzi hizo alikuwa akitangaza kwa aina ya mvuti wa pekee kila mtu aliyemsikiliza hakutaka hata kuzima radio yake kwa kwa sauti yake ambayo ilikuwa ikimvutia kila mtu, lakini baada ya kufanya kazi huko Uingereza baadae aliamua kurudi Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo sasa hivi ni TBC Taifa.

Habari ni kioo cha Jamii

Habari ni kioo cha Jamii



Mtangazaji wa idhaa ya kiswahili BBC Hassan Mazoa akijiandaa katika kipindi cha muziki na burudani enzi hizo.

Habari ni kioo cha jamii

Huyu ni Oscar Kambona Mtangazaji wa aliyerusha matangazo kwa mara ya kwanza idhaa ya kiswahili BBC mnamo juni27 1951 hakika alifanya kazi ya habari kwa nguvu zote, alifariki huko nchini Uingereza akiwa na umri wa miaka 68. Haki ya habari daima idumu

Zidumu Fikra za Baba wa Taifa.

Rais msitaafu wa awamu ya pili Tanzania wa pili kutoka kushoto akishuhudia mchezo wa bao kati ya Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere wa pili kutoka kulia na mzee mmoja wa Butiama, na wa kwanza kutoka kulia ni mke wa baba wa Taifa mama Maria Nyerere na kaka yake Nyerere Chief Burito ni wa tatu kutoka kulia. Sasa ndugu zangu Kikwete anaweza kufanya hivyo? au Tanzania ya sasa ni tofauti ya zamani? lakini tukumbuke za kale dhahabu ipo siku tutazijutia: bonyeza kwenye sehemu ya toa maoni utoe maoni yako.