Aug 23, 2008

Muda ni mali

Muda ni mali na heshima kwa watumia vizuri muda wao, hakika ukitumia muda wako vizuri utapata mafanikio na ukikata tamaa na kuaanza kulalamika hakika utabaki hivyohivyo tu yatupasa kuutumia muda wetu vizuri na hasa katika suala kujinasua katika umaskini sijalishi umaskini wa mtu mmoja pekee, hakuna bali ni umaskini wa Tanzania.

Tuijenge nchi yetu kwa kujituma kila sehemu kuhakikisha kunaijenga hata katika nyanja za kuhakikisha wanyonyaji tunawafutilia mbali, unyonyaji huu wa mabeberu yatupasa kuupinga kwa nguvu zote kwani hawa ndio chanzo cha umasikini wetu.

Sisi wazalendo tunabaki maskini huku wao wanatunyonya kila kona huku wakitutumikisha kwa malipo duni, sasa yatupasa kujikomboa kwa kudai Azimio la Arusha la baba wetu wa Taifa hayati Mwalimu J.K. Nyerere kwani hili lilikuwa mzingiti wa kukomesha unyonyaji wa mapepari na waliovunja hili Azimio yatupasa na wenyewe kuwazomea hadharani ili waone aibu ya kuvunja utawala bora wa kijamaa huku wakitupigilia kichwani mwetu bila huruma, misumari ya wapepari sijui walikuwa na ajenda gani na hawa mapepari au na wao ni mabepari?

Wajibu wa kijana

Kwanini kijana unakaa vichochoroni, unalala mitaroni, unabeba zege na magunia, unasukuma matololi, unakimbizwa na migambo wa mji, unatembea kwa miguu bila kupanda daladala, unashinda kutwa nzima hujatia kitu tumboni huku tumbo linakuuma na huku nguvu zinakuishia taratibu unaelekea guanguka??? Yote haya ni mfumo mbaya ndio unaokutesa kijana wangu na sioni pa kijikomboa!!!!!!

Kijana wangu inaniuma sana ninapokuona unanyanyaswa na hawa fisikoko hawayani, wezi wakubwa wa raslimali zetu ambazo Mungu alitupatia wao wanazitumia bila kukuhurumia wewe kijana na wanataka wakumalize kwa njaa ili wajitwalie raslimali zetu bila kipingamizi, sasa tuwazomee haoooooooooo weziiiiiiii wakubwaaaaa tumewashutukiaaaa sasa hatutaki kuibiwa kwani hawa ni wabaya sana wanatudanganya kwa mikataba mibovu huku wakiendelea kutufirisi mali yetu, ukienda Buzwagi wanaiba, Bulwanhgulu wapo, Geita wanaendelea kusafirisha dhahabu zetu, Mlima Ngasamo na Mererani wamejaa huku sisi tunakufa na umaskini.


Sasa kijana simama imara uitetee haki yako, wote vijanawa kike na wakiume pambaneni na mafisadi na wizi wa madini yenu hapo ndio hadhi yenu itarudi na mtakula haki yenu, ninasema we kijana acha kusinzia, acha kudhurura, acha kukaa, acha kujiona huwezi kutetea haki yako daima pambana kwa nguvu zote kurudisha heshima na uhai wako hakika utajikomboa.