Nov 24, 2008

Kunyongwa kwa Aleksander kaka yake Lenin ni hisia kubwa ya Lenin kutaka kuikomboa Urusi




Makala
KATIKA suala la kupigania haki za wanyonge kwa wakati mwengine linaweza kujitokeza kwa mtu kutamani kupigania haki za wanyonge kutokana na kuvutiwa na mtu furani ambaye anaonekana kuwa na harakati za kupigania haki ya wanyonge kwa nguvu zote.

Jambo hili lilitokea kwa mwanamapinduzi Mrusi mwenye fikra za kimaeneleo aliyejulikana kwa majina ya Vladimir IIyich Ulyanov (Lenin) ambaye kwa kiasi kikubwa aliathiriwa sana na kaka yake Aleksander ambaye alikuwa ni kijana mwenye nia imara mwenye kushirikilia maongozi mema ya kimaadili katika kuhakikisha wanyonge wanajikomboa.

Lenin alizaliwa Aprili 10 mwaka 1870, katika mji wa Simbirsk (sasa unaitwa Ulyanovsk) ulioko kwenye ng'ambo za mto Volga, na kukulia katika maeneo hayo ya wazi yaliyotanda sana ya mto huo mkuu wa Urusi, katika miji ya Simbirsk, Kazani na Samara.

Babu yake Lenini, N.V. Ulyanov alikuwa ni mkulima wa kitumwa wa Kirusi aliyekuwa akiishi katika Mkoa wa Nizhegorodsky, na katika mwaka 1791 alihamia katika Mkoa wa Astrakhan ambako aliandikiswa kama ni mtu wa tabaka la kati na alikufa katika hali ya umasikini hohehahe.

Baba yake Lenini, IIla Nikolayevich Ulyanov alikumbana na hali ya dhiki ya umasikini mapema sana maishani mwake, kaka yake ndiye aliyemsaidia mpaka akabahatika kupata elimu ya juu. Baada ya kuhitimu Chuo Kikuu cha Kazan baba yake Lenin alianza kufundisha katika shule za sekondari, na baadaye akawa Mkaguzi wa mashule na hatimaye kuwa Mkurugenzi wa shule za serikali katika mkoa wa Simbirsk. Alikuwa mtu mwenye fikra nzuri za kuleta maendeleo ya elimu kwa wananchi wa kawaida.

Mama yake Lenin, Maria Aleksandrovna, alitokana na ukoo wa daktari. Mama huyo alielimishwa nyumbani na akiwa mama hodari sana wa lugha nyingi za kigeni. alijua vyema fasihi na kupenda sana muziki. Alikuwa ni bibi Mwenye nia thabiti na tabia imara, mwenye akili, mtulivu na mwenye bashasha, alikuwa akijishughulisha sana katika kulea wanawe.

Katika ukoo wa Ulyanov kulikuwa na watoto sita ambao ni Anna, Aleksander, Vladimir, Olga, Dmitri na maria. Wazee wao walifanya wawezalo khakkisha watoto wao wanapata elimu ya fani mbalimbali, kuwalea wawe wapenda kazi, waaminifu, wenye adabu njama na wenye kuwafkiria watu wengine.

Kwahiyo Lenin alikulia katika ukoo huu ulioshikamana sana. Alikuwa ni mtoto mweye kuonekana wa furaha kila wakati huku akiwa mchangamfu, akipenda michezo ya hekaheka na ya makelele, kuogelea, kuteleza juu ya barafu na kwenda matembezini pamoja na marafiki wenzake.

Alijifunza kusoma alipokuwa na umri wa miaka mitano na alipotimiza miaka tisa aliingia darasala kwanza katika shule ya Simbirsk, wakati akiwa pale shuleni alisoma kwa hamu kuu akiwa na kipawa cha ajabu na kuyachukulia masomo yake bila mzaha wowote. Alikuwa kila mwaka akimaliza masomo anapata tuzo za hali juu kabisa.

Alikuwa tayari siku zote kuwasaidia wenzake pamoja na kuwafahamisha masomo magumu. katika madarasa ya mwisho ya sekondari aliwasaidia N. M. Okhotnikov, Mchuvash nk kujiandaa na mitihani yao ya kujipatia shahada ya kuhitimu shule.

Lenin mwanamapinduzi wa Urusi alikuwa akipenda sana kusoma na alivutiwa vizuri sana na vitabu vya A. Pushkin, M. Lermontonv, N. Gogol, I. Turgenev, N. Nekrasov, M. Saltykov-Shchedrin na L. Tolstoi. Sehamu kuu ya kisomo chake ilitawaliwa na vitabu vya wademokrati wa kimapinduzi, V Belinski, A. Herzen, N. Dobrolyubov na D .pisarev, pamoja na vitabu hivyo vilivyokuwa vimepigwa marufuku wakati huo. kitabu alichokuwa akikipenda zaidi ni cha N. Chernyshevski akiwa kama mwanchuoni mashuhuri na mpinzani mkali wa utawala wa mfalme na umwinyi.

Tabia na maoni ya Lenin ujanani mwake yalipatikana kutokana taathira ya malezi ya nyumbani, vitabu alivyosoma vya kimaendeleo pamoja na maisha yaliyokuwa yakimzunguka.

Wakati ule ubepari ulikuwa ikikua kwa kasi sana katika Urusi, makarakana na viwanda mbalimbali vilikuwa vikichipuka na kuajili wafanyakazi wengi ambao walikuwa wakinyonywa na kukandamizwa sana kitendo ambacho kilipelekea hali ya wafanyakazi hao kuwa mbaya sana kwani udhalimu wa serikali ya mfalme, mukandamizo wa makabaila, umasikini na unyonge wa wafanyakazi na wakulima yote haya yalimufanya lenin kuwa chukia wanyonyaji.

Lenin aliathiriwa sana na fikra za kaka yake, Aleksander ambaye alikuwa ni kijana mwenye nia imara ya kuhakikisha anaikomboa urusi kutoka katika tabaka wa wanyonyaji. "Mfano wa kaka yake kipenzi ulikuwa ni muhimu sana kwa Lenin," anasimulia Anna Ulyyanov dada yake Lenin, na kuongeza kuwa, tangu utotoni alijaribu kumwigiza kaka yake kwa kila jambo, aulizwapo atakuwa nani katika maisha yake, jibu lake lilikuwa: "Kama kaka yangu nimpendaye Aleksander"

Aleksander alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. Petersburg na alikuwa na lengo kuu katika maisha yake la kuendesha mapambano ya kimapinduzi dhidi ya utawala wa kinyonyaji wa mfalme na kuupigania umma upate maisha mazuri.

Aleksander alikuwa akielekea katika mfumo wa Mwanaharakati wa kijamaa Karl Marx katika kuhakikisha umma unajikomboa kutoka kwa utawala wa kiunyonyaji wa mfalme, ilikuwa ni kutokana na kaka yake Aleksander ndivyo Lenin alipotambua kwa mara yake ya kwanza juu ya maandishi yafuatayo maongozo ya Marx.

Lenin alikubwa na mikasa mikali ya maisha wakati akiwa kijana mdogo kutokana na kufiwa na baba yake ghafla mnamo mwaka 1886, na mara ukoo huo haujafarijika kutokana na pigo hilo mara ghafla tena msiba mwingine wa kaka yake Aleksander ukaanguka.

Msiba wa kaka yake Aleksander ulitokana na mnamo Marchi 1887 Aleksander alikamatwa mjini St. Petersgurg akikabiliwa na shtaka la kuhusika na jaribio la kutaka kumuua mfalme Aleksander III, na katika Mei, mwaka huo huo Aleksander alinyongwa katika Ngome ya Schelisselburg. "Aleksander Ulyaniov amekufa shahidi" aliandika Anna, dada yake na kuongeza kuwa "roho yake iliyotolewa mhanga imekuwa kama mwenge wa kimapinduzi uliomwangazia njia ndugu yake, Lenin."

Kunyongwa kwa kaka yake kulikuwa ni pigo kubwa sana kwa Lenin na kuthibitishia moyoni nia yake ya kuyatoa mhanga maisha yake kwa mapambano ya kimapinduzi katika kuhakikisha anaikomboa Urusi kutoka katika unyonyaji. Pamoja na hayo Lenin aliona fahari kubwa kwa kaka yake kujitoa mhanga kwa kupigania wanyonge hapo ndipo alijawa na fikra za kuhakikisha anaikomboa urusi kama kaka yake alivyodhamilia kufanya.

Kutokana na Machungu ya kaka yake lenin akaamua kutafuta njia ya kufuata fikra za kaka yake katika kuhakikisha anaikomboa urusi, katika kujitayalisha kwa mapinduzi hayo kijana huyo alikuwa na hamu sana ya kujifunza elimu za kijamii. Katika Agosti 1887, baada ya kuhitimu elimu ya sekondari pamoja na kutuzwa nishani ya dhahabu, aliingia katika Chuo kikuu cha Kazan akichukua fani ya sheria hiyo no mojawapo ya njia za kuelekea kuikomboa urusi kwa kufuata njia za kaka yake kipenzi Aleksander.

Katika Chuo Kikuu Lenin Ulynov akaaza kuingiliana na wanachuo wa kimaendeleo, wenye fikra za kimapinduzi. Mwanzoni mwa Desemba 1887 alifukuzwa katika Chuo hicho kwa kushiriki katika mkutano wa wanafunzi akisisitiza mapinduzi ya wanyonge. Baadaye Lenin alihadithia mazungumzo aliyokuwa akizungumza na afisa wa polisi aliyekuwa akimuongoza kwenda gerezani: "Ina maana gani kufanya uasi, kijana?" Afisa huyo alimuuliza na kuongeza: "Kwani huoni kuna ukuta mbele yako?" Ndiyo" Lenin alijibu na kuendelea: "lakini ukuta wenyewe umeoza kabisa, ukiusukuma kidogo tu unaanguka." Haya yalikuwa majibu ya Lenin kwa kujiamini ikijua kuwa ipo siku ukombozi wa wanyonge utaangusha ukuta wa unyonyaji.


Lenin alifungwa kifungo ambapo katika kifungo chake alikuwa anahamishiwa katika sehemu mbalimbali ambapo ilifikia hatua akahamishiwa katika kijiji cha Kokushkino (sasa unaitwa Lenino), Mkoa wa Kazan huku akiendelea kuwa chini ya ulinzi, wakati akiwa huko alitumia muda mwingi sana kumkumbuka mwongozo wa fikra za kaka yake za kukomboa wanyonge kutoka katika kunyonywa.

Vilevile alitumia muda wake kusoma na kujielimisha zaidi, alihathia "Nadhani sijawahi kusoma na kujielisha katika maisha yangu, hata wakati nilipokuwa gerezani St. Petersberg na huko Siberia, sijawahi kusoma kama nilivyosoma wakati nikiwa katika kijiji cha Kokushkino" alisimulia Lenin na kuongeza: "Nikiwa katika kijiji hicho nilisoma na kumbuka Aleksander kwa kwa kupania mno yaani kutoka alfajiri hadi usiku wa manane."

Basi katika umri wa miaka kumi na saba kijana Lenin alikuwa ameshashika njia ya kaka yake Aleksander ya mapambano ya kimapinduzi dhidi ya utawala wa mfalme.

Makala haya yameandaliwa kutoka katika mitandao na vyanzo vya habari mbalimbali.

Nipigie: +255 764 992264

No comments: