Aug 20, 2008

Dhambi ya ubaguzi

Rasilimali zetu wao wanaona kama Mungu aliwapa wenyewe na sio Watanzania wote. Wanajiamulia katika rasilimali zetu bila hata sisi kuwaruhusu wenyewe wanachukua huku wakituona sisi kama hatuna haki nazo, wakati Mungu alipotupaeia alitupa sote watanzania bila kubagua. Sasa wanaleta utawala wa kibaguzi kwa kutubagua wajili wao wakuu wakiwa na fikra za kuwa sisi ni wajinga hatujui haki zetu kumbe tunajua kila kitu, haya sasa Mungu ameshawalaani kwa kosa la kutubagua katika mali zetu, utawala wo umejaa fitna na unanuka ubaguzi kila sehemu.

Waonini sasa wamemukufuru hata Mwasisi wetu Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Watanzania kwa kushindwa kumuenzi kwa kila kitu, nakumbuka Mwalimu katika utawala wake alikuwa anapinga sana utawala wa kibaguzi, alimchukia kila mtu atakayeonekana mubaguzi kwani aliamini binadamu wote ni sawa,nakumbuka aliwahi kusema kuwa dhambi ya ubaguzi ni kubwa mno kwani ni sawa na mtu kula nyama ya mtu ambaye akiisha ila hataiacha katu.Hii ni kweli kabisa viongozi wetu mumezoea ubaguzi munatubagua sisi na hamtaacha kutubaguaa mpaka tujikomboe hapo ndio haki yetu itatimia

Hakika tunaweza

Ninaimani kubwa sana Watanzania tunaweza kujikomboa na kuwa huru kifikra, kimawzo, kiuchumi, kisansi, kijamii, kisaikoloa nk, ili tujikomboe yatupasa kufikria ni viongozi gani wanatufaa? ambao watasimama kutetea haki zetu na rasilimali zetu? hakika tukijua hilo hapo ndipo tutajikomboa na kuwa huru katika haki zetu, lakini tusipojua hilo daima tutaendelea kudhulumiwa haki zetu kwani viongozi wetu hawana na huruma nasisi pamoja na watoto wetu.

Lakini hawa wanyonyaji ninawaambia siku zao zinahesabika hazikawii ukombozi wetu unakuja mbio sana kwani hata wao wenyewe wanajua sehemu walivyotukosea sasa wanawayawaya hawana imani na sisi wameanza kutuhofia kuwa hueda tukafanya mapinduzi ya kura mwaka wa uchaguzi unaofuata.

Tumechoka kudhulumiwa

Tanzania ina kila kitu Mungu kaijalia kuwa na kila kitu ina mito na maziwa wa maji nyenye kila aina ya samaki, madini ya kila aina almasi, tanzanite, dhahabu, ulanga, makaa ya mawe,shaba, rubi nk vilevile ina milima mingi kama vile mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu kupita milima yote Afrika, mbuga za wanyma nk, vyote hivi ni mali za watanzania lakini ninashindwa kujua umasikini wetu umetoka wapi? Nani mchawi wa umasikini wetu? kwangu mimi ninavyoona mchawi anayesababisha umasini ni wale viongozi wetu hawafuati misingi ya utawala bora wenye kulinda mali hya umma bali wanauza mali zetu na kusingizia uwekezaji. uwekezaji huku munaliingizia Taifa hasara kwa mikataba mibovu lakini tunawatahadhalisha ole wenu nyinyi wanafiki ipo siku Mungu atawaadhibu kwa niaba ya watanzania, hapo ndio mtakoma na kujuta kwanini mlizaliwa Tz, lakini sasa munachekelea huku mukiendesha magari yenu ya kifisadi na kutaka kutugonga huku mukitutukana iti sie washezi, washamba hatujui hata kukwepa magari.