Nov 2, 2008

Migomo na Maandamano siku hizi Tz hapakaliki




CHAMA cha Wafanyakazi ni umoja wajumuiya ya wafanyakazi katika sekta yoyote iliyohalali na inayofanya kazi kulingana na taratibu za nchi, kwahiyo chama ni kama raia nchini aliye na haki ya kujipatia mali au haki yake, vilevile kutetea haki zake mbele ya baraza na kulindwa na sheria ya nchi.
Vile vile Chama kinauwezo wa kugoma, kuishtaki serikali, kampuni, taasisi au mwajili yoyote iwapo kitafuata misingi inayokubalika katika kudai haki yake, vilevile chama kama chama kinaweza kushitakiwa kama kitavunja kanuni na sheria zinazotakiwa.
Huko wingereza vyama hivyo vilijulikana kwa jina la "Trade Unions" , katika miaka ya 1835 ndipo vyama vidogovidogo vilipojiunga huko kuko wingereza na kufanya umoja wa vyama uliojulika kama "Grand National Consolodated Trade Unions" vikiwa na lengo moja la kudai haki za wafanyakazi.
Kwahiyo umoja huo mkubwa uliwatisha sana Wamiliki wa viwanda, serikali pamoja na matajiri wa huko ambapo kwa kuhofia nao waliamua kukishambulia vyama hivyo katika Baraza Kuu, ili kuvidhofisha na waendelee kuwanyonya wafanyakazi pasipo kuwa na ngao yoyote ya kujilinda.

Katika mashambulizi hayo ambayo yalipelekea kudhofisha vyama hivyo na kukoswa nguvu mnamo mwaka 1865 hatimaye yalitokea matata ya watu katika miji ya Sheffield na Manchester kati ya wafanyakazi na matajiri wao, ambapo ilipelekea serikali kuchukua jukumu la kuchunguza juu ya mtafaruku huo ambapo serikali baada ya kumaliza uchunguzi wake ilitangaza sheria mpya mwaka 1875 ambayo ilijulikana kama Hati au Mkataba wa vyama vya wafanyakazi huko wingereza.

Huo ndio ukawa ndio msingi wa sheria wa vyama vya watu wa kazi huko wingereza na katika nchi zilizo kuwa chini ya Dola ya Kiingereza. Katika sheria hiyo ugomaji uliruhusiwa na wanachama wa vyama hivyo waliruhusiwa kuwashawishi wenzao nao wagome kwa kuzingatia sheria na kanuni za ugomaji.
Na sasa katika karne hii vyama vya wafanyakazi ni vyama vilivyo halali kabisa katika nchi zote zilizo huru na katika kila nchi vyama vya wafanyakazi vya sekta mbalimbali zinaendelea kutetea haki za wafanyakazi ili kuondokana na kuonewa au kunyanyaswa na waajiri wao.
Katika nchi yetu Tanzania tuna vyama vya wafanyakazi vingi sana na vimesajiliwa kihalali vikiwa na lengo la kutetea maslahi ya wafanyakazi wa sekta husika, lakini pamoja na haya vyama hivyo vimekuwa vikitekeleza majukumu yao ya kulinda haki, amani utulivu wa wanachama hapa nchini kama inavyotakiwa.

Pamoja na utekelezaji wa haki hizo hivi karibuni Chama Cha Walimu Tanzania (CCW) kilitangaza kugoma nchi zima na mgomo huo ungefanyika oktoba 15 mwaka huu lakini kutokana na serikali kuhofia kuwa mgomo huo ungeleta hasara kubwa kwa taifa iliamua kwenda mahakamani kupinga mgomo huo ambapo mahaka kweli iliupinga mgomo huo.
Lakini siku ambayo walimu walitangaziwa kuwa mgomo wao umesitiswa pale katika viwanja vya Karimujee walipandwa na hasira kubwa mno ninaimani kila mtu alisikiana na kuona kwenye vyombo vya habari vulugu viliyokuwepo hapo Karimjee ambapo siku hiyo ilikuwa pia ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha baba wa taifa kwa walimu siku hiyo ilikuwa ni siku ya majonzi na huzuni.
Baadhi ya walimu walilia kwa machungu makubwa utadhani ni watoto wadogo hakika mimi ambaye nilikuwa pale nikichukua habari nilipatwa na uchungu wa huruma kubwa sana kwa walimu wangu ambao walinifundisha mpaka kufikia hatua hii niliyonayo kuwaona wakilia hadhalani huku watoto wao wakiwaangalia.
Niliwahurumia walimu wangu kwa kukataliwa kufanya mgomo ambapo tunajua kabisa kuwa mgomo ni mojawapo wa njia ya kufikisha ujumbe ulidaiwa kwa siku nyingi bila mafanikio, lakimi baadhi ya walimu walitangaza kuwa wataendelea na mgomo baridi wa kutoingia madarasani na kama walimu wakuu watawalazimisha kuingia madarasani watawafundisha wanafunzi uongo.
Sasa serikali yetu mbona mpaka sasa hatujasikia kuwa walimu wetu wameshaanza kulipwa mafao yao? Si mulisema kuwa haichukui siku chache suala lao litakuwa limeshughulikiwa? Au munataka tena watangaze kugoma tena kwa kutokwenda shule tofauti na sasa ambapo wamefanya mgomo baridi wa kufundisha uongo.
Sisi watanzania bado tunajua kuwa hawa walimu bado wamegoma kwa kutumia mgomo baridi wa kufundisha uongo kwani serikali haijatueleza kama imefanya utafiti na kubaini kuwa walimu wetu sasa wanafundisha ukweli!
Tunajua watoto wetu bado wanafundishwa uongo kwa sababu walimu walisema watafundisha uongo mpaka hapo serikali itakapolipa mafao yao na serikali mpaka sasa haijalipa mafao yao.
Wazazi tunahofu kushindwa kufaulu kwa watoto wetu katika mitihani yao kwa sababu serikali haitaki kulipa mafao ya walimu ili watoto wetu wafundishi ukweli tunasikitika sana kwa kupuuzia suala zito kama hili au kwa sababu watoto wenu wako shule za kimataifa na wengine wako Marekani na Wingereza ndio maana hamjari watoto wetu sisi masikini. Munaona sawa tu waendelee kufundishwa uongo watoto wetu.
Kama Mwalimu mmoja aliyesema pale karimujee kuwa kama wakuu wao watawalazimisha kuingia madarasani watafundisha 1+1=0 na hesabu za mlinganyo watafundisha kama hesabu za majira ya nukita, hanuoni kuwa tunakoelekea ni kuua fikra za watoto na kuzalisha rasilimali watu ambao hawaendani na kazi wanazozifanya?

Si hayo tu hata walimu wanaweza kutafuta njia nyingine ya kudai haki yao kwani kule wingereza kipindi cha wafanyakazi kunyanyaswa kwa kunyimwa mafao yao, wafanyakazi hao walitafuta njia nyingine ya kudai haki yao ambapo wafanyakazi wa viwandani waliamua kuvunja vunja vifaa vya viwandani zikiwemo mashini na baadhi ya majengo na wengine waliamua kuweka chunvi katika mashine ili vioze ambapo mapambano haya yalijulikana kama “Luddism movement” 1811.Mapambano haya ya Luddism yalilitia hasa kubwa sanaTaifa la wingereza na kupelekea kushuka kiuchumi.
Sasa walimu wakiamua kutafuta haki yao kwa njia nyingine ambayo itakuwa ya hasara zaidi ya kugoma hapo mutasemaje? Wakiamua kufanya kama Luddism ya wingereza hapo mutasemaje?
Chondechonde tunawaomba walipeni walimu wetu mafao yao ili watoto wetu wasifundiswe uongo na kunusuru kutokea kwa mgomo mwengine wenye aina kama Luddism ya wingereza kwani hasara itakayopatika ni hasara ya watanzania wote kwani ndio walipa kodi ya maendeleo ya Taifa.
Ukipenda nipigie: +255 764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com

No comments: