Aug 21, 2008

Lenin na Marx

Huwa ninalia ninapowakumbuka wapigania haki za wanyonge kama Lenin, Fredrick Angle, Dk.Carl Marx, Josef Stalen na wengine wegi huwa ninawakumbuka sana japo sitakufahamisha ni kitu gani walikifanya katika kupigania haki za binadamu kutoka kwa Mabepari ninajua bila shaka unawajua umuhimu wao katika jamii.

Lenin aliweza kupambana na mabrpari wa Urusi kwa mantiki ya kuondoa unyonyaji katika harakati zake aliwahi kuwekwa zizuizini, kufukuzwa chuo alikokuwa anasomea shahada ya sheria na kudhalilisha sana, naye Dk.Carl Marx alikuwa kama Lenin mpaka aliwahi kuandika kitabu cha kilichokuwa kinapinga unyonyaji wa Mabepari. Daima huwa ninafarijika sana ninapokumbua watu hawa muhimu katika historia ya haki za binadamu na huwa ninapata nguvu na msukumu wa kwamba kumbe hata sisi tunaweza kukomesha unyonyaji.

Habari njema

Habari zenu ndugu zangu popote pale mulipo mimi ni mzima na ninaendelea na pilikapilika za kuhakikisha haki inapatikana kutoka kwa wanyonyaji wetu wanajiita Miungu watu na kijiona wao ndio Mungu amewajalia na kuwaona na kutuona sisi kama Mungu hatupendi kumbe wanajidanganya wao wenyewe kwani Mungu wetu aliyembinguni anatupenda wote ndio maana akatupa kila kitu wote lakini wao kwa kumuuzi wakaamua kutunyang`anya na sisi haki yetu.

Watu hawa sasa wanafurahia katika dunia hii hawajui kuwa dunia hii ni ya kupita tu na makao yetu ya kudumu yako mbinguni kwa baba yetu Mungu, kule mbinguni ndio kutakuwa hakuna tena unyonyaji kama wanavyotufanyia sasa hivi huku wakitoa meno yote 36 nje kwa kujiona wao ndio wajaja kuzidi wote katika dunia hii.

Chama ni moyo

Ili kujikomboa na wanyonyaji yatupasa kuwa na umoja wenye mshikamano wa dhati umoja huo unakuja kwa kuunda chama kwahiyo wanaharakati wenzangu yatupasa sasa kuunda chama chetu cha kudai masilahi yetu wanayoyatumia kama sisi hatupo katika dunia hii kwani kimya chetu kimewafanya watuone hatuna haki.

Lakini katika maono yangu ninaona haki a wanyonge inakuja kwa nguvu zote ninaona uhuru wa kutoa maoni umekalibia watu watajikomboa kutoka kwa mabeberu makiritimba, manyonyaji, mabepari na wapinga haki yetu tuliyopewa na Hayati Mwalimu JK nyerere baba wetu wa Taifa mwenye kila aina ya sifa za kuitwa kiongozi bora Afrika. Je ninawauliza hao wabepari na wabeberu wa nchi hii huu ndio usawa wa binadamu? Mbona wenzetu mnadhurumu huku tunawaona?

uhuru na haki: Machozi yetu yasamani

uhuru na haki: Machozi yetu yasamani

uhuru na haki: Machozi yetu yasamani

uhuru na haki: Machozi yetu yasamani