Dec 27, 2008

Aleyevunja azimio la Arusha alimusaliti baba wa Taifa Mwalim Jk. Nyerere


Anasitahili kulaaniwa na Watanzania wote

Na Fita Lutonja

ILIKUWA mwaka 1992 kipindi cha rais Ally Hassan Mwinyi ambapo watu wachache bila hata kumshirikisha Muasisi wa Taifa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere walikutana Zanzibar wakiwa na lengo la kuvunja mwongozi alioweka Mwalimu wa Azimio la Arusha.

Mwaka huo ulikuwa ni mwaka wa mapinduzi makubwa yaliyofanya na watu hao yakuondoa mfumo wa utawala wa Azimio la Arusha ambao ulikuwa unakataza dhuluma kwa kila mtu na kusisitiza kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kulikomboa taifa kutoka katika umasikini.


Hatukujua mfumo wenye asili ya kibepari waliutoa wapi? Na ulikuwana faida gani kwetu? Kwa sababu hawakutueleza faida za Mfumo huo kwa taifa letu na watanzania kwa ujumla.

Walidai kuwa wanaanzisha Azimio la Zanzimbar ambapo lengo lake hatukulijua lilikuwa ni nini? Au ilikuwa ni kuruhusu aina ya ufisadi ndani ya serikali hatukujua? au hilo Azimio la ZanzĂ­bar lilikuwa na maana gani mpaka likasababisha mfumo wa baba wa taifa wa Azimio la Arusha kuonekana halifai? Jama hizo za kulivunja Azimio la Arusha mpaka leo watanzania hatujui zilikuwa na lengo gani?


Kama kweli walivunja Azimio la Arusha kwa lengo zuri mbona hawakutueleza faida za Azimio hilo la Zanzibar, kama alivyotueleza mwalimu faida za Azimio la Arusha?

Mwalimu alielezea faida za Azimio la Arusha kwa njia mbalimbali ikiwemo kupitia vyombo vya habari, vipeperushi, pia aliandika vitabu mbalimbali zinazoelezea faida za Azimio la Arusha lakini nyinyi na Azimio lenu la Zanzimbar hatujaona hata kitabu kimoja kinachoelezea faida za Azimio la Zanzimbar?


Tunakumbua ilikuwa mwaka 1967 ambapo Mwalimu alibaini dhuluma, matumizi mabaya ya madaraka , unyonyaji na ubinafsi wa viongozi ndani ya serikali yake, jambo ambalo aliona litaipeleka nchi katika hali mbaya kiuchumi na kuleta matabaka ya kiunyonyaji.

Mwalimu kwa kuona nchi itakuja kuwa mfalme wa unyonyaji aliamua kuanzisha mfumo mpya wa utawala wa Azimio la Arusha ambalo lilifanikiwa kukomesha fisikoko, unyonyaji na waliozoea kudhulu jasho la wananchi na kunufaisha matumbo yao pia nao walikomeshwa.

Fisikoko na kupe wanyonya jasho la wezao walikuwa wamezoea kudhulumu kutoka katika jasho la wanyonge walikomeshwa kwelikweli.

Mwalimu kwa kuhakikisha dhuluma, unyonyaji, wizi, matumizi ya madaraka vibaya na ukwapuaji wa pesa ovyo unathibitiwa aliamua kuazisha utawala bora wa Azimio jambo ambalo lilileta haki na usawa wa kumiliki mali ya umma.


Watanzania tuliposikia Azimio la Arusha limetangazwa huku likiwa na misingi ya utawala bora wa kuthibiti unyonyaji na dhuluma tulishangilia kwa fifijo na nderemo tukijua sasa saa ya ukombozi kwa taifa imefika.

Furaha yetu kweli ilileta matunda mema kwa taifa na wananchi kwa sababu Azimio la Arusha lilihakikisha kila mtumishi wa serikali anatumia madaraka yake vizuri huku akifanya kazi kwa bidii na kufuata maadili ya uongozi ili kujenga uchumi wa nchi.

Viongozi wote ndani ya utawala wa Azimio la Arusha hawakuruhusiwa kuiba mali ya umma na kujiongezea mapato yao, bali walitakiwa kutumia mishahara yao katika kuendesha maisha.

Lakini nyinyi muliona mafanikio haya yaliyoletwa na Mwalimu kwa kupitia Azimio la Arusha hayafai, kama hayafai kwanini munahubili utawala bora wa Mwalimu? Huwa munamaanisha nini mnaposema tumuenzi baba wa Taifa huku mkipingana naye kwa kuvunja misingi ya utawala bora wa Azimio la Arusha?

Azimio lilihakikisha mali ya umma inalindwa kwa ajili ya watanzania na iwapo kama kiongozi atatumia mali ya umma vibaya alihesabiwa kuwa amehujumu uchumi wa nchi na hukumu yake ilikuwa kali mno ili kutoa fundisho kwa kiongozi wengine kutotenda makosa ya aina hiyo.

Mwalimu alikuwa mkali sana akiona kiongozi yeyote amehujumu mali ya umma jambo ambalo linajithihilisha pale serikali yake kwa kuzingatia misingi ya maadili kwa kiongozi wa umma iliamua kumhukumu waziri mmoja wa sheria kwenda jera miezi 12 na kuchapya viboko 24 hadharani.

Tukiangalia katika utekelezaji wa maendeleo tuliona Azimio la Arusha lilianzisha siasa ya ujamaa na kujitegemea ili kuhakikisha taifa linajikomboa kutoka katika umasikini.

Katika mfumo wa ujamaa tunaona ujamaa wa Mwalimu ulisisitiza kufanya kazi kwa bidii na nguvu zote bila kutegeana ili kuongeza uzalishaji na kupelekea kuinua pato la taifa.

Ujamaa ulikataa dhuluma na matumizi mabaya ya pato la wajamaa huku ukisisitiza kuwa kila pato linamilikiwa na wajamaa wote na hakuna ubaguzi wowote.

Lakini sasa hivi dhuluma, utumiaji wa madaraka vibaya, unyonyaji, ubaguzi, mikataba mibovu ya Richmond, uchotaji wa pesa za malipo ya nje (EPA) umezidi na kupelekea watanzania kuhujumiwa mali yao hadhalani jambo ambalo Mwalimu alikuwa akilipinga sana ndani ya utawala wake wa Azimio la Arusha.


Vilevile ndani ya Azimio la Arusha, Ujamaa ulikuwa na misingi ya kutoa huduma kwa jamii bure, ikiwemo huduma ya elimu, jambo ambalo lilipelekea kupata wasomi wengi tofauti na tulivyoacha na wakoloni ambao waliicha Tanzania ikiwa na wasomi wenye taaluma wachache.

Katika utekelezaji wa jambo hili unadhihilisha kuwa Mwalimu hakupenda kabisa dhuluma zitokee hata kwenye sekta ya elimu kwani kumlipisha mtu aliona itajenga matabaka kwa wasomi wenye pesa, na masikini wasikuwa na elimu.


Na katika siasa ya kujitegemea Mwalimu alisisitiza kufanya kazi kwa bidii bila kutegemea misaada kutoka katika mataifa mengine kwa sababu alijua kuwa sisi ni matajiri wa rasilimari nyingi ambazo tukizitumia tunaweza kujikomboa kiuchumi.

Hakika Azimio lilifanikiwa kukomesha hali ya dhuluma, unyonyaji, ukupe, fisikoko, wezi wa mali ya umma, ukiritimba, ubeberu wa kujimilikisha mali ovyo kisa umebeba madaraka, yote haya ndani ya utawala wa Mwalimu yalikomeshwa.

Lakini sasa watanzania tunadhulumiwa haki yetu kabisa tunashuhudia viongozi wanatumia madaraka vibaya na kujimilikisha mali ya umma huku wakidai kuwa ujasiliamali? Tuelezeni kama mlivunja Azimio la Arusha ili muwe wajasiriamali?

Hii kweli inaingia akilini kuwa ujasiliamali unaufanyia kwenye sehemu ya uongozi? Mbona Mwalimu wakati akiwa kiongozi hakufanya huo ujasriamali? Kwa sababu alikuwa anaheshimu utawala bora wa Azimio la Arusha ambao nyinyi muliona haufai.

Haki yetu mbona munachukua bira kutuhurumia sisi watanzania masikini? Munahubiri maisha bora kwa kila mtanzania, tutapataje maisha bora wakati misingi ya kulinda mali ya umma mumeivunja iliyokuwa inatekelezwa na Azimio la Arusha?

Tunajua kuwa Azimio la Arusha lilileta usawa na kuondoa matabaka ya matajili na masikini. Lakini sasa hivi tunashudia matabaka ya walionacho na wasionacho yameongezeka huku hao matajiri wakitudhulumu nguvu kazi zetu kwa kututumikisha na kutulipa ujira finyu jambo ambalo Mwalimu alikuwa analipinga sana.

Mumevunja Azimio la Arusha ambalo lilikuwa na misingi ya maadili kwa kiongozi wa umma kutojimilikisha na kutumia madaraka vibaya kujinufaisha mwenyewe lakini sasa hivi watanzania tunashuhudia kila kiongozi aliyoko madarakani anamiliki mali nyingi, kila kiongozi aliyestafu tunaona ndio wale wanaomiliki makampuni, taasisi pamoja na vitega uchumi vingi.

Hizo mali mumezipataje? Kama sio kuthulumu mali ya watanzania wezenu? Kama kweli mumepata kwa uhali mbona munalindana zikitolewa hoja za kuchunguzwa?

Wakina Wilbroad Slaa wakipendekeza muchunguzwe ili kubaini mulikozipata hizo mali, munaanza kujikingia kifua na kujilinda wenyewe ili msifichunguzwe. Hakika tunawaambia kuwa Mwalimu alipoanzisha Azimio la Arusha hakutaka kabisa mambo mnayoyafanya yafanyike ndani ya nchi hii ya Tanzania.

Hakika kama Mwalimu angerudi angeshaanga kuona Tanzania aliyoiacha imebadilika, wawekezaji, mabepari, mabeberu wakiritimba na viongozi ndiyo wamekuwa wamiliki wa rasilimali za watanzania, pia angeshaagaa kuona mikataba mibovu kama ya Richmond inayosababisha kupotea kwa fedha za walipa kodi, ikisainiwa na viongozi wa Tanzania ya sasa.

Angesikitika kuona pesa ya malipo ya nje (EPA) inachotwa na viongozi huku wakishirikiana na wafanyabiashara maarufu wakati watanzania wanalala njaa.

Angeshaangaa sana, kuona viongozi wanatumia ofisi za umma kama ngao ya kufanyabiashara huku wakijiita wajasiriamali, jambo ambalo Azimio lake lilikuwa linakataza.

Angewasikitikia watanzania kwa kuzongwa na umasikini unaosababishwa na kuvunjwa kwa Azimio la Arusha na utawala bora.

Pia angeamua kungana na watanzania wote wanaodhulumiwa jasho lao kuamua kuikomboa upya Tanzania ili kulisimika tena Azimio la Arusha litokomeze dhuluma, unyonyaji, ubeberu, ubepari, ufisadi, ukupe na wizi wa pesa za umma.

Watanzania tungeshangilia kuiona tena saa ya ukombozi imefika kwani tumeteseka sana, tumeonewa sana, tumedhulumiwa sana, na tunatamani sana kujikomboa.

Makala haya yameandikwa na Mwananchi mwenye fikra za kimaendeleo anapatikana kwa simu: 0764 992264.

MWISHO.

Nov 24, 2008

Kunyongwa kwa Aleksander kaka yake Lenin ni hisia kubwa ya Lenin kutaka kuikomboa Urusi




Makala
KATIKA suala la kupigania haki za wanyonge kwa wakati mwengine linaweza kujitokeza kwa mtu kutamani kupigania haki za wanyonge kutokana na kuvutiwa na mtu furani ambaye anaonekana kuwa na harakati za kupigania haki ya wanyonge kwa nguvu zote.

Jambo hili lilitokea kwa mwanamapinduzi Mrusi mwenye fikra za kimaeneleo aliyejulikana kwa majina ya Vladimir IIyich Ulyanov (Lenin) ambaye kwa kiasi kikubwa aliathiriwa sana na kaka yake Aleksander ambaye alikuwa ni kijana mwenye nia imara mwenye kushirikilia maongozi mema ya kimaadili katika kuhakikisha wanyonge wanajikomboa.

Lenin alizaliwa Aprili 10 mwaka 1870, katika mji wa Simbirsk (sasa unaitwa Ulyanovsk) ulioko kwenye ng'ambo za mto Volga, na kukulia katika maeneo hayo ya wazi yaliyotanda sana ya mto huo mkuu wa Urusi, katika miji ya Simbirsk, Kazani na Samara.

Babu yake Lenini, N.V. Ulyanov alikuwa ni mkulima wa kitumwa wa Kirusi aliyekuwa akiishi katika Mkoa wa Nizhegorodsky, na katika mwaka 1791 alihamia katika Mkoa wa Astrakhan ambako aliandikiswa kama ni mtu wa tabaka la kati na alikufa katika hali ya umasikini hohehahe.

Baba yake Lenini, IIla Nikolayevich Ulyanov alikumbana na hali ya dhiki ya umasikini mapema sana maishani mwake, kaka yake ndiye aliyemsaidia mpaka akabahatika kupata elimu ya juu. Baada ya kuhitimu Chuo Kikuu cha Kazan baba yake Lenin alianza kufundisha katika shule za sekondari, na baadaye akawa Mkaguzi wa mashule na hatimaye kuwa Mkurugenzi wa shule za serikali katika mkoa wa Simbirsk. Alikuwa mtu mwenye fikra nzuri za kuleta maendeleo ya elimu kwa wananchi wa kawaida.

Mama yake Lenin, Maria Aleksandrovna, alitokana na ukoo wa daktari. Mama huyo alielimishwa nyumbani na akiwa mama hodari sana wa lugha nyingi za kigeni. alijua vyema fasihi na kupenda sana muziki. Alikuwa ni bibi Mwenye nia thabiti na tabia imara, mwenye akili, mtulivu na mwenye bashasha, alikuwa akijishughulisha sana katika kulea wanawe.

Katika ukoo wa Ulyanov kulikuwa na watoto sita ambao ni Anna, Aleksander, Vladimir, Olga, Dmitri na maria. Wazee wao walifanya wawezalo khakkisha watoto wao wanapata elimu ya fani mbalimbali, kuwalea wawe wapenda kazi, waaminifu, wenye adabu njama na wenye kuwafkiria watu wengine.

Kwahiyo Lenin alikulia katika ukoo huu ulioshikamana sana. Alikuwa ni mtoto mweye kuonekana wa furaha kila wakati huku akiwa mchangamfu, akipenda michezo ya hekaheka na ya makelele, kuogelea, kuteleza juu ya barafu na kwenda matembezini pamoja na marafiki wenzake.

Alijifunza kusoma alipokuwa na umri wa miaka mitano na alipotimiza miaka tisa aliingia darasala kwanza katika shule ya Simbirsk, wakati akiwa pale shuleni alisoma kwa hamu kuu akiwa na kipawa cha ajabu na kuyachukulia masomo yake bila mzaha wowote. Alikuwa kila mwaka akimaliza masomo anapata tuzo za hali juu kabisa.

Alikuwa tayari siku zote kuwasaidia wenzake pamoja na kuwafahamisha masomo magumu. katika madarasa ya mwisho ya sekondari aliwasaidia N. M. Okhotnikov, Mchuvash nk kujiandaa na mitihani yao ya kujipatia shahada ya kuhitimu shule.

Lenin mwanamapinduzi wa Urusi alikuwa akipenda sana kusoma na alivutiwa vizuri sana na vitabu vya A. Pushkin, M. Lermontonv, N. Gogol, I. Turgenev, N. Nekrasov, M. Saltykov-Shchedrin na L. Tolstoi. Sehamu kuu ya kisomo chake ilitawaliwa na vitabu vya wademokrati wa kimapinduzi, V Belinski, A. Herzen, N. Dobrolyubov na D .pisarev, pamoja na vitabu hivyo vilivyokuwa vimepigwa marufuku wakati huo. kitabu alichokuwa akikipenda zaidi ni cha N. Chernyshevski akiwa kama mwanchuoni mashuhuri na mpinzani mkali wa utawala wa mfalme na umwinyi.

Tabia na maoni ya Lenin ujanani mwake yalipatikana kutokana taathira ya malezi ya nyumbani, vitabu alivyosoma vya kimaendeleo pamoja na maisha yaliyokuwa yakimzunguka.

Wakati ule ubepari ulikuwa ikikua kwa kasi sana katika Urusi, makarakana na viwanda mbalimbali vilikuwa vikichipuka na kuajili wafanyakazi wengi ambao walikuwa wakinyonywa na kukandamizwa sana kitendo ambacho kilipelekea hali ya wafanyakazi hao kuwa mbaya sana kwani udhalimu wa serikali ya mfalme, mukandamizo wa makabaila, umasikini na unyonge wa wafanyakazi na wakulima yote haya yalimufanya lenin kuwa chukia wanyonyaji.

Lenin aliathiriwa sana na fikra za kaka yake, Aleksander ambaye alikuwa ni kijana mwenye nia imara ya kuhakikisha anaikomboa urusi kutoka katika tabaka wa wanyonyaji. "Mfano wa kaka yake kipenzi ulikuwa ni muhimu sana kwa Lenin," anasimulia Anna Ulyyanov dada yake Lenin, na kuongeza kuwa, tangu utotoni alijaribu kumwigiza kaka yake kwa kila jambo, aulizwapo atakuwa nani katika maisha yake, jibu lake lilikuwa: "Kama kaka yangu nimpendaye Aleksander"

Aleksander alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. Petersburg na alikuwa na lengo kuu katika maisha yake la kuendesha mapambano ya kimapinduzi dhidi ya utawala wa kinyonyaji wa mfalme na kuupigania umma upate maisha mazuri.

Aleksander alikuwa akielekea katika mfumo wa Mwanaharakati wa kijamaa Karl Marx katika kuhakikisha umma unajikomboa kutoka kwa utawala wa kiunyonyaji wa mfalme, ilikuwa ni kutokana na kaka yake Aleksander ndivyo Lenin alipotambua kwa mara yake ya kwanza juu ya maandishi yafuatayo maongozo ya Marx.

Lenin alikubwa na mikasa mikali ya maisha wakati akiwa kijana mdogo kutokana na kufiwa na baba yake ghafla mnamo mwaka 1886, na mara ukoo huo haujafarijika kutokana na pigo hilo mara ghafla tena msiba mwingine wa kaka yake Aleksander ukaanguka.

Msiba wa kaka yake Aleksander ulitokana na mnamo Marchi 1887 Aleksander alikamatwa mjini St. Petersgurg akikabiliwa na shtaka la kuhusika na jaribio la kutaka kumuua mfalme Aleksander III, na katika Mei, mwaka huo huo Aleksander alinyongwa katika Ngome ya Schelisselburg. "Aleksander Ulyaniov amekufa shahidi" aliandika Anna, dada yake na kuongeza kuwa "roho yake iliyotolewa mhanga imekuwa kama mwenge wa kimapinduzi uliomwangazia njia ndugu yake, Lenin."

Kunyongwa kwa kaka yake kulikuwa ni pigo kubwa sana kwa Lenin na kuthibitishia moyoni nia yake ya kuyatoa mhanga maisha yake kwa mapambano ya kimapinduzi katika kuhakikisha anaikomboa Urusi kutoka katika unyonyaji. Pamoja na hayo Lenin aliona fahari kubwa kwa kaka yake kujitoa mhanga kwa kupigania wanyonge hapo ndipo alijawa na fikra za kuhakikisha anaikomboa urusi kama kaka yake alivyodhamilia kufanya.

Kutokana na Machungu ya kaka yake lenin akaamua kutafuta njia ya kufuata fikra za kaka yake katika kuhakikisha anaikomboa urusi, katika kujitayalisha kwa mapinduzi hayo kijana huyo alikuwa na hamu sana ya kujifunza elimu za kijamii. Katika Agosti 1887, baada ya kuhitimu elimu ya sekondari pamoja na kutuzwa nishani ya dhahabu, aliingia katika Chuo kikuu cha Kazan akichukua fani ya sheria hiyo no mojawapo ya njia za kuelekea kuikomboa urusi kwa kufuata njia za kaka yake kipenzi Aleksander.

Katika Chuo Kikuu Lenin Ulynov akaaza kuingiliana na wanachuo wa kimaendeleo, wenye fikra za kimapinduzi. Mwanzoni mwa Desemba 1887 alifukuzwa katika Chuo hicho kwa kushiriki katika mkutano wa wanafunzi akisisitiza mapinduzi ya wanyonge. Baadaye Lenin alihadithia mazungumzo aliyokuwa akizungumza na afisa wa polisi aliyekuwa akimuongoza kwenda gerezani: "Ina maana gani kufanya uasi, kijana?" Afisa huyo alimuuliza na kuongeza: "Kwani huoni kuna ukuta mbele yako?" Ndiyo" Lenin alijibu na kuendelea: "lakini ukuta wenyewe umeoza kabisa, ukiusukuma kidogo tu unaanguka." Haya yalikuwa majibu ya Lenin kwa kujiamini ikijua kuwa ipo siku ukombozi wa wanyonge utaangusha ukuta wa unyonyaji.


Lenin alifungwa kifungo ambapo katika kifungo chake alikuwa anahamishiwa katika sehemu mbalimbali ambapo ilifikia hatua akahamishiwa katika kijiji cha Kokushkino (sasa unaitwa Lenino), Mkoa wa Kazan huku akiendelea kuwa chini ya ulinzi, wakati akiwa huko alitumia muda mwingi sana kumkumbuka mwongozo wa fikra za kaka yake za kukomboa wanyonge kutoka katika kunyonywa.

Vilevile alitumia muda wake kusoma na kujielimisha zaidi, alihathia "Nadhani sijawahi kusoma na kujielisha katika maisha yangu, hata wakati nilipokuwa gerezani St. Petersberg na huko Siberia, sijawahi kusoma kama nilivyosoma wakati nikiwa katika kijiji cha Kokushkino" alisimulia Lenin na kuongeza: "Nikiwa katika kijiji hicho nilisoma na kumbuka Aleksander kwa kwa kupania mno yaani kutoka alfajiri hadi usiku wa manane."

Basi katika umri wa miaka kumi na saba kijana Lenin alikuwa ameshashika njia ya kaka yake Aleksander ya mapambano ya kimapinduzi dhidi ya utawala wa mfalme.

Makala haya yameandaliwa kutoka katika mitandao na vyanzo vya habari mbalimbali.

Nipigie: +255 764 992264

Nov 2, 2008

Migomo na Maandamano siku hizi Tz hapakaliki




CHAMA cha Wafanyakazi ni umoja wajumuiya ya wafanyakazi katika sekta yoyote iliyohalali na inayofanya kazi kulingana na taratibu za nchi, kwahiyo chama ni kama raia nchini aliye na haki ya kujipatia mali au haki yake, vilevile kutetea haki zake mbele ya baraza na kulindwa na sheria ya nchi.
Vile vile Chama kinauwezo wa kugoma, kuishtaki serikali, kampuni, taasisi au mwajili yoyote iwapo kitafuata misingi inayokubalika katika kudai haki yake, vilevile chama kama chama kinaweza kushitakiwa kama kitavunja kanuni na sheria zinazotakiwa.
Huko wingereza vyama hivyo vilijulikana kwa jina la "Trade Unions" , katika miaka ya 1835 ndipo vyama vidogovidogo vilipojiunga huko kuko wingereza na kufanya umoja wa vyama uliojulika kama "Grand National Consolodated Trade Unions" vikiwa na lengo moja la kudai haki za wafanyakazi.
Kwahiyo umoja huo mkubwa uliwatisha sana Wamiliki wa viwanda, serikali pamoja na matajiri wa huko ambapo kwa kuhofia nao waliamua kukishambulia vyama hivyo katika Baraza Kuu, ili kuvidhofisha na waendelee kuwanyonya wafanyakazi pasipo kuwa na ngao yoyote ya kujilinda.

Katika mashambulizi hayo ambayo yalipelekea kudhofisha vyama hivyo na kukoswa nguvu mnamo mwaka 1865 hatimaye yalitokea matata ya watu katika miji ya Sheffield na Manchester kati ya wafanyakazi na matajiri wao, ambapo ilipelekea serikali kuchukua jukumu la kuchunguza juu ya mtafaruku huo ambapo serikali baada ya kumaliza uchunguzi wake ilitangaza sheria mpya mwaka 1875 ambayo ilijulikana kama Hati au Mkataba wa vyama vya wafanyakazi huko wingereza.

Huo ndio ukawa ndio msingi wa sheria wa vyama vya watu wa kazi huko wingereza na katika nchi zilizo kuwa chini ya Dola ya Kiingereza. Katika sheria hiyo ugomaji uliruhusiwa na wanachama wa vyama hivyo waliruhusiwa kuwashawishi wenzao nao wagome kwa kuzingatia sheria na kanuni za ugomaji.
Na sasa katika karne hii vyama vya wafanyakazi ni vyama vilivyo halali kabisa katika nchi zote zilizo huru na katika kila nchi vyama vya wafanyakazi vya sekta mbalimbali zinaendelea kutetea haki za wafanyakazi ili kuondokana na kuonewa au kunyanyaswa na waajiri wao.
Katika nchi yetu Tanzania tuna vyama vya wafanyakazi vingi sana na vimesajiliwa kihalali vikiwa na lengo la kutetea maslahi ya wafanyakazi wa sekta husika, lakini pamoja na haya vyama hivyo vimekuwa vikitekeleza majukumu yao ya kulinda haki, amani utulivu wa wanachama hapa nchini kama inavyotakiwa.

Pamoja na utekelezaji wa haki hizo hivi karibuni Chama Cha Walimu Tanzania (CCW) kilitangaza kugoma nchi zima na mgomo huo ungefanyika oktoba 15 mwaka huu lakini kutokana na serikali kuhofia kuwa mgomo huo ungeleta hasara kubwa kwa taifa iliamua kwenda mahakamani kupinga mgomo huo ambapo mahaka kweli iliupinga mgomo huo.
Lakini siku ambayo walimu walitangaziwa kuwa mgomo wao umesitiswa pale katika viwanja vya Karimujee walipandwa na hasira kubwa mno ninaimani kila mtu alisikiana na kuona kwenye vyombo vya habari vulugu viliyokuwepo hapo Karimjee ambapo siku hiyo ilikuwa pia ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha baba wa taifa kwa walimu siku hiyo ilikuwa ni siku ya majonzi na huzuni.
Baadhi ya walimu walilia kwa machungu makubwa utadhani ni watoto wadogo hakika mimi ambaye nilikuwa pale nikichukua habari nilipatwa na uchungu wa huruma kubwa sana kwa walimu wangu ambao walinifundisha mpaka kufikia hatua hii niliyonayo kuwaona wakilia hadhalani huku watoto wao wakiwaangalia.
Niliwahurumia walimu wangu kwa kukataliwa kufanya mgomo ambapo tunajua kabisa kuwa mgomo ni mojawapo wa njia ya kufikisha ujumbe ulidaiwa kwa siku nyingi bila mafanikio, lakimi baadhi ya walimu walitangaza kuwa wataendelea na mgomo baridi wa kutoingia madarasani na kama walimu wakuu watawalazimisha kuingia madarasani watawafundisha wanafunzi uongo.
Sasa serikali yetu mbona mpaka sasa hatujasikia kuwa walimu wetu wameshaanza kulipwa mafao yao? Si mulisema kuwa haichukui siku chache suala lao litakuwa limeshughulikiwa? Au munataka tena watangaze kugoma tena kwa kutokwenda shule tofauti na sasa ambapo wamefanya mgomo baridi wa kufundisha uongo.
Sisi watanzania bado tunajua kuwa hawa walimu bado wamegoma kwa kutumia mgomo baridi wa kufundisha uongo kwani serikali haijatueleza kama imefanya utafiti na kubaini kuwa walimu wetu sasa wanafundisha ukweli!
Tunajua watoto wetu bado wanafundishwa uongo kwa sababu walimu walisema watafundisha uongo mpaka hapo serikali itakapolipa mafao yao na serikali mpaka sasa haijalipa mafao yao.
Wazazi tunahofu kushindwa kufaulu kwa watoto wetu katika mitihani yao kwa sababu serikali haitaki kulipa mafao ya walimu ili watoto wetu wafundishi ukweli tunasikitika sana kwa kupuuzia suala zito kama hili au kwa sababu watoto wenu wako shule za kimataifa na wengine wako Marekani na Wingereza ndio maana hamjari watoto wetu sisi masikini. Munaona sawa tu waendelee kufundishwa uongo watoto wetu.
Kama Mwalimu mmoja aliyesema pale karimujee kuwa kama wakuu wao watawalazimisha kuingia madarasani watafundisha 1+1=0 na hesabu za mlinganyo watafundisha kama hesabu za majira ya nukita, hanuoni kuwa tunakoelekea ni kuua fikra za watoto na kuzalisha rasilimali watu ambao hawaendani na kazi wanazozifanya?

Si hayo tu hata walimu wanaweza kutafuta njia nyingine ya kudai haki yao kwani kule wingereza kipindi cha wafanyakazi kunyanyaswa kwa kunyimwa mafao yao, wafanyakazi hao walitafuta njia nyingine ya kudai haki yao ambapo wafanyakazi wa viwandani waliamua kuvunja vunja vifaa vya viwandani zikiwemo mashini na baadhi ya majengo na wengine waliamua kuweka chunvi katika mashine ili vioze ambapo mapambano haya yalijulikana kama “Luddism movement” 1811.Mapambano haya ya Luddism yalilitia hasa kubwa sanaTaifa la wingereza na kupelekea kushuka kiuchumi.
Sasa walimu wakiamua kutafuta haki yao kwa njia nyingine ambayo itakuwa ya hasara zaidi ya kugoma hapo mutasemaje? Wakiamua kufanya kama Luddism ya wingereza hapo mutasemaje?
Chondechonde tunawaomba walipeni walimu wetu mafao yao ili watoto wetu wasifundiswe uongo na kunusuru kutokea kwa mgomo mwengine wenye aina kama Luddism ya wingereza kwani hasara itakayopatika ni hasara ya watanzania wote kwani ndio walipa kodi ya maendeleo ya Taifa.
Ukipenda nipigie: +255 764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com

Taifa linaangamia taratibu chukua hatua




SALAAM Rais wangu Jakaya Mrisho Kikwete, nakusalimia ewe mtukuka mwenye nyingi rehema, mwenye upendo na nchi yako na watanzania wote hakika unaupendo mkubwa na nchi yako ndiyo maana huachi kufanya ziara kuizungukia nchi yakoTanzania kila sehemu ili kujua hari ya watu wako mlezi wa Tanzania na juzijuzi ulikuwa Mbeya, haya yote ni kutokana na kuipenda nchi yako.

Nchi yako Tanzania nayo Mungu ameijalia sana kwani rasilimali za kila aina vyote ameipatia, Tanzania tuna madini ya kila aina yakiwemo dhahabu, almasi, ulanga, Tanzanite n.k.

Vilevile ina maziwa na mito ya maji ya kila aina likiwemo ziwa vicktoria ambalo linazalisha samaki aina ya sangara kwa wingi ambao wakazi wa kanda ya ziwa wanapata Mapanki kwa ajili ya kutumia kama mboga kwani minofu yote huwa inachukuliwa na wawekezaji tuliowapa wachukue ili watupatie pesa za kigeni kwa maendeleo ya taifa letu.

Pamoja na hayo vilevile nchi yako Mheshimiwa Rais ina Milima mingi ukiwemo Mlima Kilimanjaro ambao ni Mlima mrefu kuzidi Milima yote Afrika, Mlima huu huwa unatuingizia pesa nyingi za kigeni yote haya ni kutokana na Mungu kuijalia nchi yako Tanzania.

Rais wangu Tanzania yako ina rasilimali nyingi sana ambazo na sisi watanzania tunazitumia ili kujiletea maendeleo pamoja na kwamba wawekezaji ndio wamechukua sehemu kubwa ya rasilimali zetu lakini yote haya ni kuhakikisha taifa linapiga hatua kimaendeleo.

Rais wangu Jakaya nakupa pole sana kwa Masaibu yaliyokukuta kwani tangia ukumbwe na kimbunga cha kuzomewa na kurushiwa mawe huko Mbeya sijakusalimia na kukupa pole baba mlenzi, mtetezi wa wanyonge.

Pole sana Mtukufu mlezi wa rasilimali za taifa kwa manufaa ya kizazi kijacho hakika wewe ni Mkombozi wa Tanzania ndio maana tulikupa kura kwa asilimia kubwa huku tukishangilia kuwa wewe ni chaguo la Mungu.

Yawezekana na Mungu alikujua kuwa wewe ndiye utakuja kuwatetea Watanzania kuondokana na dhuluma, unyonyaji, na kukomesha ufisadi ndani ya nchi yako mpaka kipindi cha miaka yako mitano itakapoisha ili kuingia tena uchaguzi mwingine wa hapo mwaka 2010 ambapo pia ungemalizia yaliyobakia.

Nakupa pole Rais wangu kutokana na matukio yanayoiandama serikali yako kwa sasa ni ya kusikitisha mno kwa sababu yanaashiria kuwa nchi yako Rais wangu ipo kwenye dimbi la hatari kuelekaea katika hari isiyo ya kawada kwani fikra za watu na hisia zao wameanza kuzionyesha hadharani sijui ni kwanini wanapata msukumu huu mpaka wa kuamua kukurushia mawe Rais wangu na kufanya Migomo ya kila aina?

Rais wangu yakupasa kufikiria kwa kina jambo hili la kurushiwa mawe wakati ukiwa katika ziara yako Mkoani Mbeya kwanini watu wa huko walidhubutu kukurushia mawe? Hapa kuna kitu ambacho unatakiwa kukitambua mapema ili kukipatia ufumbuzi kwa haraka zaidi kwani kitendo cha kukuzomea na kukurushia mawe ni nguvu ya fikra ya watu hao ya kufikria kuwa hujawatendea kitu fulani ambacho ulitakiwa kukitekeleza.

Sasa baada ya kuona kuwa haki yao hawapati japo kuwa ile haki wanaijua kuwa ni yao kihalali sasa ili kufikisha ujumbe wa hisia za fikra zao wakaamua kukuzomea na kurusha mawe ili ujue kuwa hujawapatia kile walichokuwa wanakitaka.

Nikiwa kule Mbeya kama kawaida yangu ya kuchukua habari ili nihabarishe umma wa Watanzania wenzagu wenye nia ya kujua matukio yanayotokea katika dunia hii nilibahatika kushuhudia kuzomewa kwa Rais Kikwete katika maeneo ya Mwanjelwa, katika maeneo hayo wananchi walipouona msafara wa wake walitanda barabarani kuuzuia msafara huo wa Rais wakimtaka azunguze nao.

Lakini alipojitokeza wananchi walianza kupiga kelele wakizungumzia ufisadi huku wakisema kwa nini Rais hashughulikii mafisadi mbalimbali wakiwemo wa EPA wakati aliapa kuwa atailinda na kuitetea katiba ya nchi? Na baadhi ya watu wakihoji kuhusiana ahadi alizotoa za kuwapatia ajira na maisha bora.

Na katika kijiji cha Kanga Wilayani Chunya tukio la kurushiwa mawe msafara wake ni jambo ambalo halisitahili na la kushangaza, lakini Rais wangu alichukulia kama jambo dogo na kumtaka Mkuu wa Mbeya John Mwakipesile ambaye alionekana kufadhisha sana na jambo hilo kwa kumwambia kuwa, asifadhaike sana kwani yeye Rais watu wa Mbeya wanampenda sana.

Rais jambo hili ni jambo zito kwani wananchi hawa kuamua kukurushia mawe huku wakidai ajira na maisha bora ni dhahili kuwa hujawaletea hayo maisha bora, ajira pamoja na kutekeleza kulitetea taifa lako kwa kushughulikia Mafisadi ili kuondoa umasikini iliokidhili kwa kila jamii.

Kwahiyo baada ya kuona maisha yao yanaendelea kudidimia huku wakiumia katika dimbi kubwa la umasikini wa kulala njaa na kuvaa nguo chakavu na zilizochanika kwa kukoswa pesa za kununua nguo mpya na chakula, wakamua kufanya jambo kama hilo ambalo halikutakiwa kutendeka.

Nakupa pole sana kwa misukosuko inayokupata katika uongozi wako Rais wangu, kwani uongozi wako umekuwa na misukosuko kila wakati tukiangalia misukosuko mingine tofauti na kurushiwa mawe na kuzomewa kule Mbeya.

Tunaona tangia watanzania tukukabidhi madaraka misukosuko imekuandama sana! Tulishuhudia kuvunjika kwa Baraza la Mawaziri kutokana na kujihudhuru kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowasa kwa kashifa ya Mkataba feki wa Richmond uliosababisha pesa ya walipa kodi kupotea bure.

Mara tu baada ya Richmond tukaona suala EPA nalo likaibuka ambalo lilisababisha pesa zetu kuchotwa pale benki kuu, Ndani ya utawala wako tu tumeshuhudia Zanzimbar iliyokuwa imara hapo zamani sasa inataka kujitenga.

Misukosuko inakuandama mara Madaktari kugoma wakidai nyongeza za mishahara, Wanafunzi wa vyuo vikuu kila wakati wanagoma wakidai hawatendewi haki mambo haya yote tumeyashuhudia, misukosuko inazidi kuendelea mara walimu kugoma wakidai malipo ya posho zao mpaka wanaamua kurusha mawe huku wakitoa machozi kama watoto wadogo kwa uchungu mkubwa.

Wazee wa walikuwa wa Wafanyakazi wa iliyokuwa Afirika Mashariki nao wanadai mafao yao ambayo bado wanaendelea kuzungushwa serikali yako, nao wanaamua kuzimalizia hisia zao kwa kumfungia Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi kwa hasira kali ya kuonyesha liwapo na liwe.
Jambo ambalo wazee hao wamelitoa juzijuzi katika viwanja vya Mnazi Mmoja Watanzania tunasononoka sana kwani katika viwanja hivyo wazee walisema kutokana na serika kushindwa kuwalipa mafao yao, sasa wamepanga kutoa pigo kali takatifu kwa serikali ambalo pigo hilo halitasahaulika daima! Japo kuwa hawa wazee walikataa kulitaja hilo pigo kwa waandishi wa habari wakidai kuwa serikali imekuwa ikipangua mipango yao wakiitaja, lakini hili pigo walisisitiza litakuwa la aina yake kwani serikali hata ifuatilie kwa aina gani haitagundua, bali itashutukia tu inapata pigo hilo takatifu.
Jamani watanzania tunashindwa kujua hili pigo takatifu ambalo serikali haitasahau litakuwa la namna gani? Lakini yote haya ni hasira ya wazee wale kunyimwa haki ya mafao yao wakati wakiona mafisadi wakiendelea kutanua na pesa za walipa kodi huku wakikumbatiwa na serikali kama vifaranga vya kuku.

Haya machache niliyoyatanja ni ishara tosha kabisa Rais wangu kuwa nchi yako inaelekea katika machafuko ambayo mwisho wake ni kuanguka kwa taifa la Tanzania.

Ukipenda nipigie: +255 764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com

Oct 20, 2008

Nani ataikomboa upya Tanzania?

SIKUTAKA kuandika juu ya Ujamaa tena katika maisha yangu lakini baada ya kukaa na kufikiria kwa kina zaidi nikaona nitakuwa siwatendei haki Watanzania wenzangu ambao walifaidika na ujamaa katika kipindi cha Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hasa katika kuondoa unyonyaji, dhuluma na ubaguzi yakiwemo mafisadi, katika kipindi hicho ujamaa ulitumia itikadi za kijamaa za kuunganisha watu kwa pamoja katika kufanyakazi na kama mtu ataonekan hafanyi kazi ujamaa ulimuona mtu huyo kama kupe anayeishi kwa kunyonya jasho la wengine.

Pia nikaona kama nitaacha kuzungumuzia Ujamaa nitakuwa simutendei haki Baba yetu wa Taifa ambaye alikuwa Mwazilishi wa huo Ujamaa ndani ya Azimio la Arusha. Ili kumuenzi Mwalimu baba wa Taifa aliyeondoa unyonyaji kwa kutumia hilo Azimio la Arusha ambalo lilikuwa na hiyo siasa ya Ujamaa sikuona sababau ya kuacha kabisa kulizungumzia Azimio la Arusha na siasa yake ya ujamaa.

Kitu ambacho kilitaka kunisababisha nisizungumzie Ujamaa tena ni ile kauli ya Rais wangu Jakaya Mrisho Kikwete niliyoisoma katika gazeti moja la kila siku toleo la jumapili kuwa Mheshimiwa Rais wangu wakati akifanyiwa mahojiano na shirika la habari moja, Mwandishi wa shirika hilo alimuuliza swali kuwa anaizungumuziaje kuhusiana na nchi yake ni ya kijamaa? na anazungumuziaje ujamaa katika nchi yake? katika jibu lake Rais wangu alisema Siasa ya ijamaa katika nchi yake iwapo mtu yoyote atazungumuzia ujamaa ataonekana kama Mwendawazimu!!

Siku hiyo niliposoma hiyo habari nilishutuka sana na nikaa kufikiria kama kweli Mheshimiwa anaweza kusema kitu kama hicho kuwa mtu akizungumzia ujamaa ataonekana Mwendawazimu! Baada ya kufikiria nikahoji mimi mwenyewe ataonekanaje mwendawazimu wakati huyo viongozi wetu akiwemo Mh. Rais wangu wanasisitiza kumuenzi baba wa Taifa na kazi alizozifanya ikiwemo na ujamaa?


Pamoja na kuhoji hivyo lakini hakiri yangu ikachukua jukumu la kuamua kuacha kabisa kulizungumuzia Azimio la Arusha na siasa yake ya Ujamaa na Kujitegemea kwani nilifikiri nikiendelea kuzungumuzia mambo haya nitaonekana kama Mwendawazimu!! na ili nionekane mimi ni Mwerevu basi nisizungumzie kabisa hili Azimio la Arusha na Utawala wake ambao ulituletea matumaini na faida kubwa sana Watanzania enzi za Mwalimu Nyerere kwa kuwa ulitokomeza na kudhibiti wanyonyaji,wadhulumaji na wahujumu ambapo sasa ni maarufu kwa jina mafisadi.

Lakini tangia niamue kuacha kuuzumgumuzia huu ujamaa nimekuwa nikijiouna ninazidi kuwa mjinga na ujinga ndio unaongezeka kwani nimekuwa nikisahau kabisa kumuenzi baba yetu wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pamoja na utawala wake ambao ulikuwa wa haki kwa kila Mtanzania.

Baada ya kukaa kimya huku nikifukria nikagundua kuwa kumbe kuzungumuzia ujamaa wa Mwalimu ni kujinyima haki yangu ya kumuenzi baba wa Taifa, hapo ndipo nikapata akiri kuwa kumbe nilipochukua jukumu la kuacha kuzungumuzia ujamaa ni sawa na kumunyima haki yake Mwalimu ya kumuenzi pia ni mojawapo ya kuwanyima haki watanzania wengine kujua mambo ambayo yalifanya na ujamaa kwa manufaa ya watanzania.

Baada ya kugundua hayo nikaamua hata kama waniite Mwendawazimu lazima kila sehemu ninapopita nitalizungumuza na kuhubiri misingi ya Azimio la Arusha na siasa zake za ujamaa na kujitegemea mbazo zilitusaidia watazania kufaidi raslimali zetu wenyewe kwani zilileta neema kubwa kwa watanzania wote.

Mwalimu bila hiana aliona kuwa mambo ya ya ufasadi yangetokea katika Taifa letu, aliona dhuluma ingetawala katika jamii, aliona unyonyaji ungekuwa ndio mfumo tawala katika taifa letu, aliona ubaguzi ungekuwa utamaduni ulitawala katika Taifa letu, aliona umma wa watanzania utakuja kushindwa kutumia raslimali zake kwa manufaa yao, hapo Mwalimu ndio aliona ili kujikinga na mambo haya aazishe Azimio la Arusha na misingi yake ya utawala bora.

Azimio hilo likawa na misingi madhubuti ya kutoruhusu kiongozi yoyote kujitwalia pesa ya umma kwa manufaa yake. Kwa leo nitaongelea zaidi faida za ujamaa ambao nilikuwa nimeamua nisiuhubiri kwa kuhofia kuitwa Mwendawazimu.

Tunajua kabisa ujamaa ulitokana na Azimio la Arusha ukiwa kama mojawapo ya siasa ambazo zilitakiwa kila mtanzania azifuate na kwa matendo na imani ili kujikomboa kiuchumi, kifikra, kiutumwa n.k.

Mwalimu aliweka kanuni za siasa ya ujamaa katika Azimio la Arusha ili kuweza kuwawezesha watanzania kuwa wajamaa, waishi kijamaa kwa kufanya kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo kwa pamoja pasipo kubaguana.

Ujamaa wa Mwalimu ulikataa ubaguzi wa mtu na mtu ndani ya jamii ukimanisha kuwa binadamu wote ni sawa na ndugu, kwahiyo hakuna binadamu ambaye yuko juu ya mwezake, hakuna binadamu ambayo anatakiwa kumiliki mali za Taifa na mwingine kutomiliki, ujamaa ulikuwa na na misingi ya kutokomeza unyonyaji kwa kuwafahamisha watanzania kuwa hakuna mtu ambaye anatakiwa kufanya kazi kwani ulibainisha kuwa misingi ya ujamaa ni kufanyakazi kwa pamoja na haukuruhusu kiongozi yoyote kujichotea pesa ya umma sehemu yoyote iwe benki kuu au sehemu yoyote kwani pesa hiyo ilihesabiuka kuwa ni pesa ya kila mtu yaani ya kijamaa kwa ajili ya maendeleo ya wajamaa.

Ujamaa haukuruhusu dhuluma katika sehemu yoyote kwani ulisisitiza kila mtu lazima afanye kazi kwa nguvu zake zote na nia yake yote, ili kuleta maendeleo ya Taifa, vilevile ndani ya siasa ya ujamaa dhuluma ilihesabika kama ni dhambi ambayo ilipaswa kukemewa na kila Mjamaa.

Ujamaa wa Mwalimu ulisisitiza watu kushikamana kwa pamoja bila kubaguana ndio maana ulikuwa ukiendana na maadamano mbalimbali ya mishikamano hasa watu wa kijijini bila shaka watakuwa wanayakumbuka maandamano hayo ambapo watu walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali zikiwemo za kujivunia ujamaa kuwezesha kuleta itikadi ya kukomesha unyonyaji, na kuondoa fisikoko waliozoea dhuluma bila kujishughulisha.

Ujamaa wa Mwalimu ulileta vijiji vya ujamaa ndani ya jamii watu waliondolewa katika makazi ya porini na kuhamishiwa katika sehemu moja na kuuda kijiji kimoja ulifanya hivyo ukiwa na lengo la kusisitiza mushikamano wa kuishi kijamaa na ulitaka huduma za kijamii zimufikie kila mtu kwa pamoja pasipo kumuhudumia wa sehemu moja na kuacha wa sehemu nyingine.

Katika kulitekeleza hili Mwalimu alihakikisha watu waliokuwa katika sehemu hiyo moja ya kijiji wanapata huduma za kijamii zikiwemo shule, zahanati, mpembejeo, ghara za kutunzia nafaka zao, sehemu ya karibu ya kuuzia mazao yao na huduma nyingine nyingi kwa pamoja.

Katika vijiji vya ujamaa ili kuinua zaidi kilimo Mwalimu aliamua kila kijiji cha ujamaa kipewe Makisai na majembe ya kukokotwa na Ng'ombe ambayo yalikuwa yakitumika kulimia katika mashamba yao ya ujamaa na wakipata mazao wanauza katika sehemu hizo husika.

Hakika katika ujamaa kulikuwa na faida nyingi sana ambazo zingine sitaweza hata kuzitaja kwani kitamaliza sehemu yote ya gazeti hili na kwa ajili ya faida hizi hata kama muniite Mwendawazimu kwa kuzungumuzia ujamaa wa Mwalimu niitine tu, na ninawahakikisheni ya kuwa sitaacha kumuenzi Mwalimu kwa kazi yake kubwa aliyoifanya kama hii ya kuanzisha siasa ya ujamaa wenye misingi ya kutoruhusu mtu kunyonywa jasho la nguvu zake.

Ninaimani kabisa ujamaa ulioleta fikra ya usawa ndani ya jamii mpaka leo hatuna ukabira hata kidogo ukikaa kwa wagogo wewe msukuma kama mimi unaoneka ni Mjamaa kama wao kwahiyo utapatiwa kila kitu, ikienda kwa kwa Wanyantuzu wewe ni Mkwele utapokelewa vizuri na wala hutabaguliwa hata kidogo kama huduma zote utapata yote haya ni kwa sababu ya fikra za Mwalimu za ujamaa za kumdhamini mtu hata kama katoka wapi kama unakitu mugawane sawa ndio fikra za kiujamaa ambazo zilikataa unafiki.

Na mpaka hapo mimi sione sababu za kuona kuwa ukizungumzia ujamaa utaonekana kama ni Mwedawazimu. Kama kweli ujamaa ni mwendawazimu kwani ulileta hasara gani kwa umma wa Watanzania? kwani kuwahamisha watu kutoka sehemu walizo kuwa wanaishi ili huduma za kijamii ziwafikie kwa pamoja ni jambo baya? Kuondoa ubaguzi kwa kuwaunganisha watu katika sehemu mbalimbali ili waishi kijamaa ni jambo baya? kusisitiza watu wafanye kazi kwa pamoja ni jambo ili kujikomboa kimaendeleo pasipokutegemea wawekezaji nalo ni jambo baya? Hakika sione hatia ya ujamaa! na sione kosa alilolifanya Mwalimu katika kuanzisha ujamaa!

Huu mfumo ambao umetawala wa ubepari faida zake kwa watanzania mbona hatuzijui? Sasa tunaona mali zetu watanzania zinamilikiwa na wachche huku watanzania walio wengi wanahangaika kwenye ndimbwi la umasikini kitendo ambacho mongozo wa ujamaa ulikuwa hautaki hata kidogo. Wachache wanaotumia nguvu ya pesa zao ndio wanaoendelea kujitwalia sehemu ya raslimali zetu huku watanzania masikini wakiendele kunyanyasika, kuteseka na kushinda njaa huku wakikumbuka mtetezi wa wanyonge Azimio la Arusha na siasa yake ya Ujamaa.

Wawekezaji nao wanachukua raslimali zetu kwa bei poa kwa mfano hayo madini yetu asilimia 97 yote wanachukuwa wao na kupeleka kwao ughaibuni huku sisi wazalendo wakitubakishia asilimia 3 tu ambayo ukilinganisha na udhamani wa madini yetu ni sawa na tunawapa bure.

Ujamaa ulipinga mtu kujimilikisha kitu au kumiliki kitu pekee yake kwa manufaa yake peke yake (binafsi) bali mtu alitakiwa kila kitu ni cha umma hakuna mwenye nacho lakini sasa umilikishaji binafisi umetufanya Watanzania wengi waliomasikini kukoswa haki yetu ya kumiliki, kama umma wa watanzania sasa uchumi wote wanamiliki wachache wenye pesa zao huku Watanzania masikini hawana kitu wanalia na umasikini wa kushinda njaa kila siku, kumbukeni hakuna kitu kibaya maishani kama kuishi kwenye nchi yako lakini uchumi wa nchi hiyo unakuwa siyo wako hii ni sawa na utumwa.

Kumbe sasa tumewagundua hila zao kwa Mwalimu za kulivunja Azimio la Arusha na misingi yake ya utawala bora! Hila hizi kumbe walikuwa hawautaki ujamaa kwa sababu ni Mwendawazimu. Sasa nianawauliza wakati Mwalimu yupo mbona hamukusema kuwa ujamaa ni uendawazimwi? Mbona Rais wangu Kikwete anamuzalilisha Mwalimu kwa kuita mfumo wake wa uongozi ni uendawazimu?
Hakika mimi ninapata hasira ninaposikia Mwalimu baba wa Taifa anaenziwa kwa matusi ya aina hiyo! Jamani hizi za kuita ujamaa uendawazimu si ni laana kubwa mno? Mbona munatuingiza kwenye laana kubwa namna hii? Acheni hizo kama mumechoka kutuongoza si bora mukajihudhulu kuliko kuanza kutoa matusi kwa Mwasisi wa Taifa letu! Tahadhali kuanzia sasa mukome kututukania Mwalimu wetu kama mulikuwa hamumupendi sisi tunampenda sana.
Na ninamalizia kwa kusema kuwa laiti kama Mwalimu Nyerere angekuja kuishi na Watanzania tena, angeamua kuikomboa Tanzania upya, kwani angesikitika kuona ujamaa wake aliouleta kwa ajili ya kuikomboa Tanzania na kutokomeza unyonyanyi ubaguzi na dhuluma unafananishwa na Mwendawazimu huku maisha aliyoyataka Watanania kuyafuata ili waishi kwa usawa na haki hayafutwi tena.

Angeikomboa upya Tanzania kwani asingevumilia kuona watanzania wanaendelea kuishi katika umasikini huku baadhi ya wachache wanaishi maisha ya kifahari kutokana na kuwawadhulumu haki ya rasilimali zao. Pia angeshangaa kuona ubepari ambao alikuwa anaupinga vita kali sana katika kanuni za Azimio la Arusha sasa ndio umekuwa Mfalme wa Tanzania.
Ni mimi mwendawazimu nipigie: 0764 992264
Niandikie: fitazi@hotmail.com
Kwa taarifa zaidi niblogu: http://www.fitalutonja.blogspot.com/

Oct 10, 2008

Uhuru wa habari ni haki ya kila mtu

Huyu hapa ni Mtangazaji mwanamke wa kwanza wa idhaa ya kiswahili BBC anaitwa Zayana Self, hapo akiwa na Watangazaji wengine wa idhaa hiyo, Mwanamke huyu alikuwa mojawapo wa watangazaji wanavuti katika idhaa hiyo.

Uhuru wa Habari ni haki ya kila mtu

Mtangazaji David wa idhaa ya kiswahili BBC enzi hizo alikuwa akitangaza kwa aina ya mvuti wa pekee kila mtu aliyemsikiliza hakutaka hata kuzima radio yake kwa kwa sauti yake ambayo ilikuwa ikimvutia kila mtu, lakini baada ya kufanya kazi huko Uingereza baadae aliamua kurudi Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo sasa hivi ni TBC Taifa.

Habari ni kioo cha Jamii

Habari ni kioo cha Jamii



Mtangazaji wa idhaa ya kiswahili BBC Hassan Mazoa akijiandaa katika kipindi cha muziki na burudani enzi hizo.

Habari ni kioo cha jamii

Huyu ni Oscar Kambona Mtangazaji wa aliyerusha matangazo kwa mara ya kwanza idhaa ya kiswahili BBC mnamo juni27 1951 hakika alifanya kazi ya habari kwa nguvu zote, alifariki huko nchini Uingereza akiwa na umri wa miaka 68. Haki ya habari daima idumu

Zidumu Fikra za Baba wa Taifa.

Rais msitaafu wa awamu ya pili Tanzania wa pili kutoka kushoto akishuhudia mchezo wa bao kati ya Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere wa pili kutoka kulia na mzee mmoja wa Butiama, na wa kwanza kutoka kulia ni mke wa baba wa Taifa mama Maria Nyerere na kaka yake Nyerere Chief Burito ni wa tatu kutoka kulia. Sasa ndugu zangu Kikwete anaweza kufanya hivyo? au Tanzania ya sasa ni tofauti ya zamani? lakini tukumbuke za kale dhahabu ipo siku tutazijutia: bonyeza kwenye sehemu ya toa maoni utoe maoni yako.

Oct 9, 2008

Fikra za Mwalimu

Mwalimu alikuwa anaipenda hata Familia kama alivyokuwa anawapenda Watanzania angalia katika picha hii hapa akiwa katikati na kushoto ni mama yake kulia mke wake Marry Nyerere. Picha hii lilipigwa Novemba10, 1985 baada ya Mwalimu kuamua kung`atuka madarakani.

Oct 8, 2008

Zidumu fikra za Mwalimu

Mwalimu atakumbukwa daima na watu wenye upendo na nchi yao mambo aliyafanya kwa Taifa letu ni fahari ya watanzania. Huwa napata hasira kubwa mno ninapoona viongozi wetu wakizidi kuvuruga utawala bora wa haki kwa kushindwa kumuenzi kwa utawala wake bora wa Azimio la Arusha lililokuwa na misingi ya haki huku likiwa linakataa dhuluma ya viongozi likitulinganisha viongozi na watu wengine ni sawa.

Natamani siku moja nirudishe heshima ya Mwalimu na ninandoto za kurudisha hii heshima ya Mwalimu kwa watanzani ili watanzania wenzangu waishi kwa amanipasina kunyonywa na Mabeberu yalituzunguka, na ninuhakika ipo sikunitairudisha heshima ya Mwalimu, ninaumia mno ninapoona viongozi wakivunja yale aliyoyakataa Mwalimu BlockquoteDaima zidumu fikra za Mwalimu

Oct 7, 2008

Fikra za Mwalimu


Fikra za Mwalimu baba wa Taifa zidumu, hakika Mwalimualikuwa na fikra za kimaendeleo, alikuwa mtu wa watu, alikuwa kiongozi anayestahili kuigwa na jamii ya viongo, sasa tunaelekea katika kuadhimisha kumbukumbu ya kifo chake huyu baba wetu wa Taifa nawaomba wananchi wenzangu tujitokeze kumuenzi Mwalimu.





Na walaaniwe wale wote waliovunja uongozi bora wa Mwalimu kwa kulizika Azimio la Arusha na misingi yake yote ya utawala bora, Watanzania tuungane wote kwa pamoja kumlaani huyoaliyevunja Azimio la baba kwani umaskini wetu wote huu ni chanzo chake yeye aliyevunja Azimio, lakini shida tunazozipata watanzania kwa ajiliya kuvunja utawala bora wa Azimio la Arusha ule wake kwa kutuletea hizi shida daima Mungu atamuhukumu kulingana na kutusababishia utawalawa dhuluma.

Sep 24, 2008

Ipo siku haki yetu itapatikana.


Aliyevunja Azimio la Arusha ana hatia kubwa

Makala

Fita Lutonja

NINAIKUMBUKA Februari 5, 1967 kama ni siku ya ukombozi wa wanyonge na changamoto ya kuongeza fikra za maendeleo miongoni mwa Watanzania, kwani siku hiyo kule Arusha, hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alitangaza kukomesha watu waliozoea kunyonya jasho la wanyonge bila huruma.

Hakika siku hiyo ilikuwa ya neema kwa Watanzania, kwani mfumo mpya wa utawala chini ya Azimio la Arusha, uliashiria nyota ya matumaini ya kujikomboa kwa wanyonge na waliokuwa wanadhulumiwa haki zao.

Baada ya Tanganyika kupata uhuru wake mwaka 1961 na kuwa Jamhuri mnamo mwaka 1962, na hatimaye kuungana na Zanzibar mnamo mwaka 1964 na kuunda Tanzania, hatukuwa na maendeleo makubwa.

Lakini Mwalimu kwa kuona baadhi ya viongozi kuwa bado wana fikra za kinyonyaji kama walizokuwa nazo wakoloni, akaamua kuanzisha Azimio la Arusha lililokuwa na misingi ya kulinda haki za wanyonge na kuondoa dhuluma ya tabaka la wanyonyaji.

Mwalimu aliona kipindi hicho umma wa Watanzania ukidhoofishwa kwa kudhulumiwa haki na tabaka la mabeberu na mabwanyenye ambao wengi wao walikuwa ni viongozi serikalini, kitendo hicho cha viongozi kuwanyonya wanyonge kilimkera sana.

Dhuluma haikuwa siri kipindi hicho, viongozi waliwadhulumu Watanzania waziwazi bila hata aibu, huku wakijiona wao ni bora zaidi ya wanyonge, wakiendelea kujikusanyia mirija mirefu ya kunyonya mali na haki za watu wengine. Waliendelea kuwakashifu walipa kodi kwa kuwanyonya jasho lao bila hata kuwahurumia.

Haikumchukua muda Nyerere kubaini kuwa ndani ya serikali yake changa, kuna wanyonyaji; mabepari na mabwanyenye ambao hawakuwahurumia wananchi wanyonge wa kawaida.

Alitambua kumbe ubepari na unyonyaji si rangi ya mtu tu. Ilionekana wazi kuwa hata watu weusi wanaweza kuwa wabaya kama walivyo Wazungu.

Baada ya kuona kuwa wanyonge wanadhulumiwa haki zao, tena hadharani, Nyerere aliamua kulinda haki yao ili isiendelee kudhulumiwa.

Aliunda Azimio la Arusha kama misingi ya kuhakikisha kuwa haki ya mnyonge inalindwa kama inavyolindwa haki ya mwenye nguvu. Aliliwekea Azimio kanuni za kuhakikisha hilo linatendeka.

Ni kweli kuwa Azimio lilisaidia kuleta usawa katika jamii. Kupitia Siasa ya Ujamaa, Azimio la Arusha lilifanikisha wanyonge nao kujiona kuwa wana fursa ya kufaidi matunda ya uhuru. Ujamaa na Azimio liliwataka viongozi kuwa wajamaa kweli, wakiwaona watu wanaowaongoza kama ndugu.

Hii ilisaidia kujenga utawala bora, unaoheshimu misingi ya utu badala ya unyonyaji. Hakukuwa na mtu dhalili na mtu bora. Unyonyaji ulionyeshwa kuwa ni mbaya.

Azimio la Arusha pamoja na misingi yake kwa watumishi wa umma, vilevile lilisisitiza ujamaa kuwa ni imani na njia pekee ya kuondokana na ubaguzi, ubinafsi na dhuluma, na kuwafaidisha wananchi wa aina zote nchini. Azimio, pamoja na Ujamaa viliamsha mori na ari ya kufanya kazi kiasi kwamba nchi ilifanikiwa kujijenga kwa kiasi kikubwa.

Watu walifanya kazi kwa kujitolea na kuanzisha vijiji vya ujamaa hadi viwanda. Tanzania ikageuka kuwa mzalishaji wa bidhaa zilizohitajika sana kwa ajili ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Azimio lilikuwa na siasa ya kujitegemea pia, ambayo iliboresha utumishi wa umma na uajibikaji wa viongozi na wananchi wa kawaida. Siasa hiyo ilimtaka kila mtu katika nafasi yake, kuhakikisha anazalisha kwa wingi, ili kuepuka kutegemea mtu mwingine.

Hii ilianzia kwa mtu mmoja mmoja mpaka kwa taifa. Taifa nalo lilitakiwa kujitegemea kwa mahitaji yake yote muhimu.

Watu walitakiwa kuwa na fikra kuwa wanaweza kuendesha maisha yao binafsi, au nchi bila hata kutegemea nchi nyingine. Tofauti na sasa, ambapo Azimio limeuawa, nchi imekuwa ni kama ombaomba. Jinsi ambavyo wanavyoongezeka ombaomba wa mitaani, na nchi nayo inazidi kuwa ombaomba na inakuwa kama inashindana na ombaomba wa mitaani.

Sasa hali imebadilika baada ya Azimio la Arusha kuuawa na kuzikwa. Hali imezidi kuwa mbaya na kwa hakika, aliyeliua Azimio la Arusha anastahili kubebeshwa lawama zote na hata ikibidi alaaniwe.

Mtu huyo anapaswa kubeba lawama zote kwa sababu amewasababishia mamilioni ya Watanzania maisha magumu.

Hivi sasa Watanzania wameshaanza kushuhudia unyonyaji na unyanyasaji ndani ya nchi yao wenyewe, licha ya kuwa walipata uhuru miaka zaidi ya 40 iliyopita.

Unyonyaji umerudi kwa kasi kwa njia ya uwekezaji.

Wawekezaji wamegeuka kuwa wanyonyaji ambao wanakamua mali za Watanzania bila huruma.

Watanzania, ambao nchi yao ina rasilimali zisizohesabika, leo wamekuwa wanyonge kama watu wanaoishi jangwani kusiko na kitu chochote.

Hadi hii leo sijaelewa nini ilikuwa misingi ya kuvunja Azimio la Arusha. Na misingi hiyo ilikuwa na masilahi gani kwa umma wa Watanzania?

Inashangaza kuwa wakati Azimio la Arusha lilipoundwa, wananchi walielimishwa maana na faida zake. Lakini walipoamua kulivunja, hawakutokea hadharani kueleza sababu za kufanya hivyo!

Mwalimu alifanya mikutano na kuchapisha vitabu na makala mbalimbali, yote akilenga kuwaelimisha wananchi wa kawaida kuhusiana na mfumo huu mpya wa maisha yao.

Lakini wenzetu hawakuona umuhimu wa kuwaeleza wananchi kwa nini waachane na mfumo wa maisha ambao wamekuwa wakiishi kwa miongo minne iliyopita.

Kimyakimya walikusanyika Zanzibar na kufanya maamuzi makubwa huku Watanzania wenyewe wakiachwa gizani. Kwa nini wananchi hatukuulizwa kabla ya kufikia uamuzi wa kuvunjwa kwa Azimio la Arusha? Au kwa nini mlipoamua kulivunja hamkurudi tena kwetu kutueleza ni kwa nini mmefikia uamuzi huo?

Au mlipoingia madarakani mliona hamupati nafasi ya kutuibia na kutunyonya haki yetu kwa sababu ya kanuni za Azimio la Arusha ziliwabana?

Kwani Azimio la Arusha lilikuwa na kasoro gani? Hivi kutetea haki za wanyonge nacho ni kitu kibaya? Mbona hamkutueleza hizo kasoro?

Azimio la Arusha, lililokataza viongozi kumiliki mali kupindukia limevunjwa na matokeo yake tumekuwa na viongozi mafisadi.

Au sijui ni mafisadi viongozi, maana ni vigumu kujua, kwa sababu wapo viongozi ambao walianza ufisadi kabla ya kupata uongozi na wakatumia mali zao kusaka uongozi, pia wapo viongzoi ambao walitumia nafasi zao kujilimbikizia mali na kuwa mafisadi.

Watu sasa wananyonywa na viongozi wao, dhambi ile ile ambayo Nyerere aliiona na kuiwekea kanuni za kuikataa.

Leo inakumbatiwa na wananchi wamekosa mtetezi kwa sababu viongozi ambao walipaswa kuwa watetezi wao, ndio wanaoongoza kundi linalowanyonya.

Azimio lenu la Zanzibar limeleta nini kwetu sisi Watanzania wa hali ya chini? Mbona limezidi kutuumiza na kutuletea maisha magumu na kutufanya tuwe wanyonge zaidi?

Sasa hivi masuala ya dhuluma, unyonyaji, umwinyi sanjari na ufisadi ndani ya serikali ni vitu vya kawaida.

Walidhani kuwa umaskini uliokuwepo ulikuwa unaletwa na Azimio la Arusha, wakaliua ili kutokomeza umasikini.

Lakini hali ya mambo imethibitisha kuwa hilo si kweli kwa sababu umaskini badala ya kutoweka, unaongezeka.

Na inavyoonekana ni vigumu sana kukuza uchumi wa nchi kwa mfumo walioukubali. Sana sana wanachofanya ni kujenga uchumi wa watu binafsi.

Tunatawaliwa kwa mfumo mpya wa ukoloni mamboleo. Tofauti yake na ukoloni tulioung’oa mwaka 1961 ni ndogo sana lakini madhara yake ni makubwa kuliko ya ule tulioukataa zamani.

Uhuru wetu sasa umegeuka kuwa wa bendera, jambo ambalo Azimio la Arusha lilikuwa linapiga vita kupitia kanuni zake.

Mwalimu katika mkutano wake wa kuelezea ubora wa Azimio la Arusha aliwaambia Watanzania ya kwamba jambo muhimu ni kujitegemea.

Aliwaambia Watanzania kuwa hawapaswi kumtegemea mtu mwingine yeyote. Tumeliua Azimio la Arusha na tumeingia katika mtego wa kuwategemea wafadhili na wahisani!

Azimio lenu la Zanzibar, ambalo kimsingi linatetea viongozi, limetuletea aibu ndani ya nchi yetu kwa viongozi wa umma kujimilikisha mali ya umma kwa kisingizio kuwa ni ujasiriamali.

Azimio lenu la Zanzibar tunalilaani kwa sababu limetuletea EPA, Richmond, unyonyaji, ubeberu, dhuluma, ufisadi, na matatizo chungu nzima ambayo yote haya tungekuwa na Azimio la Arusha yasingetokea kwani misingi yake ilikuwa hairuhusu.

Viongozi wanapswa kutambua kuwa wananchi wamechoka kweli na EPA, Richmond , unyonyaji, ubeberu, ubepari, ukupe, ukiritimba, umwinyi na wanachotaka ni Azimio la Arusha la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na misingi yake ya utawala bora, ili liunguze tena viongozi vikaragosi waliozoea dhuluma.

Idumu nguvu ya haki:
nipigie:0764 992264

Sep 20, 2008

Toa Maoni kwani ni uhuru wako


Huyu ni Sophia Kessy mtangazaji mahiri na mwenye sauti yenye kuvutia kwa kila msikilizaji. kwani katika kipindi chake cha Afikani mbambata ndani ya nyumba ya clouds Fm huwa anatisha, mwanadada kweli amejaliwa kipaji chake.

Sep 18, 2008

Toa Maoni

Hapa ni mimi siku hiyo nachukua picha hii nilikuwa na rafiki yangu Dora Sanga ambaye ni mfanyakazi mwenzanzu.

Haya:




Huyo naye anaitwa mic is just my friend naye and nampenda pia na yeye ananipenda japo kuwa hana ufikra wa kunishauri sana maana anapenda tuongelee masuala yasiyo na faida lakini mimi nimeshazoe kuongelea mabo muhimu kama wazungu wanavyodai kuwa non skilled people always talk about themselve, little skilled people talk about other peole and skilled and serius people talk about development and how to solve problem for progress achieve

Sep 15, 2008

Toa Maoni

Huyu ni rafiki yangu anaitwa Gloria anakaa Marekani ni mojawapo wa marafiki zangu niwapendao sana katika maisha yangu ila huyu ninampenda zaidi kwa sababu ana huruma kwa kila mtu, na sasa hivi ananitafutia visa ya kwenda Marekani kufanya kazi huko kulingana na kuniambia kwa muda mrefu nimeamua kumkubalia ombi lake kwenda kwa hiyo hivi karibuni akikamilisha kuwasilianasa na ubalozi wetu atanitumia hiyo visa ili niruke, ila sitaisahau Tanzania na mafisasadi wake nitahakikisha nikisitafu kazi yangu huku nije Tanzania kupambana na mafisadi ili kurudisha heshima ya wanyonge haya: BlockquoteMungu nibariki mimi mubariki rafiki yangu Gloria na mwisho Mungu ibariki Tanzania.

Sep 13, 2008

Toa Maoni yako





Anaitwa Markus Mpangala mwanafunzi chuo kikuu cha Dar rafiki yangu mkubwa sana na sijapata rafiki mwenye mawazo na fikra za maendeleo kama yeye hakika amenishauri mambo mengi sana katika maisha yangu na wmengi aliyonishauri leo hii yameniletea maendeleo katika maisha yangu.
Kwa sasa hivi mimi na yeye wote ni wandishi wa habari katika magazeti mbalimbali hapa nchini vilevile wote ni Wanablogu tunaohakikisha kila mtu dunia nzima anapata habari kupitia blogu zetu

Toa Maoni yako




Huyu ni rafiki yangu Habiba anakaa Dar ni rafiki yangu wa karibu sana kwani huwa ananishauri pale ninapokwanma kimawazo na kifikra hakika sitamusahau na wewe kama unamatatizo niombe contact zake ili upate ushauri daima huwa hatozi kitu chochote ni mjamaa wa kweli nas na fikra za kiujamaa. Basi ndugu toa maoni kuhusiana na ulivyomuona na maelezo yangu

Toa Maoni yako.


Huyu ni mwanaglogu mwenzangu je, unamonaje? toa maoni yako kuhusiana na unavyomuona hapo kwenye picha ila mimi huwa ninajifunza mambo mengi kutoka kwake. Muangalie hivyo tuni mwanadada nzuri kwanza anavutia na anaakili nyingi sana na ni mtu wa malengo na maisha yake.

Sep 11, 2008

Ukombozi wa haki ni uhuru wa habari

MAKALA

KWA misaada mbalimbali ya habari tunaona historia ya mawasiliano ya umma ilianza mwanzoni mwa utamaduni wa watu walipokuwa wanawasiliana na mfumo wa ishara baadaye wakawa wanawasilia kwa mdomo kipindi hicho kulikuwa hakuna lugha ya kuandika , kwahiyo mawasilia yalifanyika pale watu wanapoonana oso kwa uso

Kipindi hicho watu walikuwa wanaishi kwa kutegemeana lakini kulingana na muingiliano wa jamii mawasiliano yalihitajika sana mwingoni mwa jamiiambapo mawasiliano hayo kulingana watu kuhitaji kuwasiliana, mawasilano hayo hayo yalihitaji teknolojia zaidi ili kukidhi mahitaji ya jamii.

Miongoni mwa miaka ya 5,000 kabula ya Christo sehemu mbalimbali binadamu waligundua herufi mbalimbali kama kule Misri watu wa kule waligundua herufi za kutumia picha ambazo walikuwa wanatumia katika kufikishana ujumbe. Huko China watu wa kule waligundua herufi mbalimbali ambazo walitumia katika mawasiliano yao, hii yote inatudhihilishia kuwa watu walihitaji sana kuwasiliana na inatuonyesha kuwa mawasiliano ni ya muhimu katika jamii hayapaswi kupuuzwa hata kidogo kama yanavyopuuzwa Tanzania.

Halikadhalika siku zilivyozidi kwenda ndio watu walivyokuwa wanahitaji zaidi mawasiliano miongonui mwao hapo ikaja pale Mwanamapinduzi Mhunzi wa vyuma Johannes Guernberg alipokundua mashine ya kuchapisha herufi ambayo ilisaidia sana watu katika kuwasilia kwa kuandika hizi ni changamoto zilizojitokeza ili kuhakikisha binadamu anapata mawasiliano.

Ugunduzi wa Guternberg ilivuta hisia kubwa sana miongoni mwa jamii ambapo watu wengi walikubali ugunduzi wake. Mitandao mbalimbali inatuambia miongoni mwa watu waliokubali kazi ya Guternberg ni Mwanaharakati Marshall McLuhan ambaye alielezea kuhusiana na kazi ya Guternberg katika kitabu alichokiandika mnamo 1962 huku akikiita kw jina la “The Guternberg Galaxy” katika kitabu hiki McLuhan alielezea kiundani zaidi umuhimu wa ugunduzi wa Guternberg katika mfumo mzima wa mawasiliano.

Mitandao inaendelea kutuhabarisha kuwa uvumbuzi wa Guterberg ulipelekea kujitokeza kwa uandishi wa habari ambapo ilipelekea kuanzishwa kwa machapishi mbalimbali, kuko Kaisari Roma kulianzishwa gazeti la Acta Diurna na sehemu mbalimbail kama huko Holland mwaka 1920 kulianzishwa gazeti la Corantos. Hii yote ilikuwa ni kupanuka kwa mawasiliano kutokana na mahitaji ya binadamu, ambapo ilipelekea baada ya muda kujitokeza kwa uandishi wa habari na vyuo mbalimbali za uandishi wa habali zikaanzishwa, ilikuweka mbele umuhimu wa mawasiliano na kuwawezeshha waandishi kuwa makini na kazi yao.

Kulingana na kupanuka kwa mawasilano ya habari kwa kutumia vyombo vya habari na vyuo vya uandishi wa habari kuongezeka Taaluma hii ya habari ilipata umuhimu zaidi na kuleta changamoto kubwa sana miongoni mwa jamii. Huko marekani taaluma ya habari ilitiliwa maanani sana, siyo tu Marekani hata nchi zingine ziliona umuhimu wa taaluma hii yenye kutumia hakili na busara, kuwa ni miongoni mwa taaluma ya muhimu sana katika jamii. Baada ya kuelezea hayo hapo juu kama nilivyokufahamisha hapo mwazo kwamba nimetumia vyanzo vya habari mbalimbali ikiwemo mitandao.

Ninakuja sasa Tanzania. Je, hii taaluma tunaidhamini kama nchi zingine? Tunaipa heshima kama taaluma zingine kama vile udaktari, ualimu, uchumi, uongozi, Uanasiasa, utaalamu wa miamba, uiginia, nk? Tanzania hii taaluma ya habari haidhaminiwi, inatukanwa, inadharauliwa, inanyongwa hadharani, kudharauliwa hivyo ndio inapelekea taaluma hii kuonekana dampo kwa kila Mtanzania, ninaposema dampo musinielewe vibaya mbali ninamaana ya kuvamiwa na kila mtu na kujiita Mwandishi wa habari. Ninarudia tena kusema kuwa taaluma hii Tanzania ni dampo, kweli hii taaluma ni dampo kabisa, tena lile dampo lenye kila aina ya takataka mbalimbali zikiwemo zile zinazonuka vibaya sana.

Hii inashangaza sana kwa nchi kama Tanzania kutothamini taauma ya habari ambayo ni taaluma muhimu sana ndani ya jamii kwani taaluma hii ndio mfanisi mkuu wa kuhabarisha Taifa katika nyanja mbalimbali kama vile za kijamii, kiuchumi, kisiasa, kisaikulojia, kijeshi nk. Inashangaza sana kwa taaluma hii nyeti hapa Tanzania kuingiliwa na kila mtu kuanzia mtu wa darasa la saba utakuta ni Mwandishi wa habari na tena kaajiliwa na chombo cha habari. Huyu mtu darasa la saba hana taaluma ya habari atawezaje kuandika habari zenye kuelimisha jamii kama siyo kuidhalilisha taaluma ya habari na kuliweka Taifa katika hari ngumu? Huyu mtu darasa la saba hana upeo na suala zima la habari atawezaje hata kumuuliza maswali Waziri au Mkurugenzi yoyote ili apate habari yenye kuelimisha jamii? Ataanzia wapi kuuliza maswali wakati hajui namna ya kuuliza maswali yenye kupelekea kuandika habari yakinifu yenye faida kwa wananchi na Taifa kwa ujumla? Tunapofanya hivi siku za mbele Taifa litakuwa katika hari gani? Je litaelimishwa au litahatarishwa?

Tanzania kuna mambo ya ajabu kabisa utakuta hata mtu amesoma taaluma nyingine lakini mtu huyo akikoswa kazi katika fani yake anakimbilia uandishi wa habari, huyu atafanyaje kazi ya uandishi wa habari wakati fani yake ni Ualimu au Uasikari kama siyo kupeleka Taifa shimoni na kudidimiza uhuru wa wananchi katika kupata habari za kuelimisha ambazo ni haki yao ya msingi? Wanapokosea hawa watu ambao hawana taaluma hii ya habari si Taifa na Watanzania wote wanadanganywa? Tanzani tusifanye mchezo kwa mambao muhimu katika Taifa kama haya. Kwa nchi kama tanzania si ajabu kukuta chombo kama redio hakina Mwanataaluma wa fani hiyo hata mmoja, hivi vyombo vipo tena vingi!!!!! na vimesajiliwa na serikali yetu ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Serikali inasajiri vipi hivi vyombo vya habari bila hata mwandishi na mtangazaji wa habari hizo kama siyo ufisadi ndani ya serikali na vyombo vya habari kwa ujumla? Hii si kufanya taaluma hii kama dampo la kukimbilia watu wa aina mbalimbali na matokeo yake kupata habari za uongo zenye madhara katika jamii. Serikali ninawaomba muangalie vizuri taaluma hii ya habari kwani musipoangalia mutajikuta munawaandihi wegine kutoka Milembe Dodoma!!!!! Maana uandishi wa habari umezidi kuvaniwa na kila mtu.

Tanzania hii taaluma imekuwa kimbilio la kila mtu (dampo) kwani hata mtu alikuwa anagombania ukisura (usura) akishinda huo usura basi anakuwa mwandishi wa habari na anaajiliwa na chombo cha habari. Hivi kushinda huo usura ndio kamaliza chuo cha uandishi na utangazaji wa habari? Mbona watu hawa wanadhalilisha taaluma ya habari? mbona hawakibilii uhakimu, ualimu au upolisi? Taaluma hii ya habari tunaididimiza wenyewe kwa kutoipa chamgamoto za kutosha na kuidhamini kama taaluma zingime, hii ndio inapelekea kudharauliwa kwa Waandishi wa habari wetu na kudharauliwa huko kunawalenga wanahabari wote kumbe wachafuzi wa taaluma ni wengine ambao hawajasomea taaluma ya habari na hawafuati maadili ya uandishi wa habari.

Kulingana na taaluma hii kuonekana ni taaluma ambayo inavamiwa na kila mtu serikali kwa kushirikiana na vyombo vya habari nchini waweke mikakati ya kudhibiti kuwa na waandishi wasio na taaluma ya habari katika vyombo mbalimbali vya habari hapo ndio tutalinda heshima ya kazi ya uandishi wa habari na wananchi tutawapa haki yao ya kupata habari zinazotakiwa lakini sasa Wananchi tunawnyima haki yao ya kupata habari zenye kuelimisha zilizoandikwa na kutangazwa na waandishi wenye ujuzi na taaluma yao. Tukifanya hivi hakika laana tutazimaliza zak kila siku kutukanwa kwa waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya habari, utamatuni na michezo mwaka 2008/2009 iliyowasirisha bugeni inaonyesha dhahiri katika vyombo vya habari kuwa watatekeleza mambo mengi sana likiwemo la kulinda maadili ya uandshi wahabari hili linatakiwa liende sanjari na kuondoa waandishi wachafuzi wa maadili ya uandishi wa habari ili kuwatendea haki yao wananchi ya kupata habari zenye kukidhi mahitaji yao. Musituambie kuwa kazi ya uandishi wa habari inaweza kufanywa na kila mtu, hilo hatukubaliani nanyi hata siku moja, anayesema hivyo daima tutamuona haitakii mema Tanzania au hajui undani wa kazi hii, ama hajasoma uandishi wa habari ndiyo maana inataka kuingiza nchi katika janga ambalo watoto wetu watakuja kulijutia na kulaani kwa nini tulifanya hivyo? daima hii laana tutatembea nayo.

Pamoja na bajeti hii kuwa nzuri ili waandishi wa Tanzania waweze kuheshimika miongoni mwa jamii, serikali kwa kupitia wizara husika inatakiwa kuweka mipaka katika vyombo vya habari kuajili watu wenye taaluma ya habari na kuondoa fikra za kuamini kuwa kazi ya uandishi inaweza kufanya na kila mtu kwani tunapoamini hivyo tunakuwa hatuwatendei haki yao wananchi ambayo wanatakiwa kuipata kupitia vyombo vya habari.. Serikali iwajari wananchi wake kwa kuweka mikakati ya kuwapatia habari zenye mantiki ya kuelimisha, kuwafahamisha, kuwajenga kwa kuweka mikakati dhabiti kwa kuajiri watu wenye taaluma ya habari, kwani hao watu watakuwa wanaujuzi na kazi yao, wanajiamini na kuheshimu taaluma yao, hapa ndipo wananchi watapata habari zenye kuaminika na hii itapelekea kujenga heshima kwa waandishi wa habari .

Bila hivyo waandishi wa habari wataendelea kutukanwa, kunyimwa haki yao, kulaaniwa, kuwekwa kitanzini, kufukuzwa ofisini, kunyimwa uhuru, kudhalilishwa, pamija na kuitwa majina mengi ya kejeli na dhihaka kama vile makanjanja, wachovu, watu wa mishiko, waandishi njaa, chakupewa na mengine mengi wanayoitwa sasa hivi. Kejeli hizi zinawanyima haki yao waandishi wenye taaluma ya habari vilevile zinavunja misingi ya utawala bora Tanzania.

Toa maoni yako kwa kubonyeza sehemu ya maoni chini au nipigie 0764 992264

Aug 29, 2008

Saa ya ukombozi

Wakati umefika wa kujiuliza, kujitafiti, kujinasua na kujikomboa kutoka kwa hawa wanyonyaji makupe wanaotumia jasho letu kutunyonya ili wao waendelee kuwa matajiri, yatupasa kujiuliza kwa kina na fikra za kimaendeleo sasa tufanyeje? Kwani wa kutukomboa sasa hayupo tena kwani Azimio la Arusha mtetezi wa haki halipo tena!!! Wale makupe ngunguni wamelihujumu ili watunyonye kweli na sisi tunakubari Azimio la baba wetu Hayati Mwalimu JK Nyerere liondoke kwa sababu Mwalimu hayupo?

Tusikubari yatupasa kushika kila kitu kurudisha Mkombozi wetu Kipenzi Azimio la Arusha kwani alikuwa analinda maslahi yetuna jasho letu lisitumiwe na Wanyonyaji wa nguvu za umma, yatupasa kujiuliza ni lini tutajikomboa na kutoka katika Utumwa wa hawa Mabeberu wanyonyaji?

Sisi wenyewe ndio tunaweza kujikomboa kwa Azimio lilitufundisha Ujamaa na Kujitegemea kwahiyo tusisubili watu wengine watukomboe hayupo wa kutuhurumia tupambane ili tulirudisha Azimio la Arusha liunguze tena vikaragosi na kuleta ujamaa wa kweli. Ndugu wanaharakati, mashika ya dini, mashikaka mengine malimbali, na watanzania wote tupiganieni azimio la baba wa Taifa tuhakikishe tunalirudisha na kanuni zake za kukata milija kwa Mabwanyenye.

Tusiposimama imara kwa hili wataendelea kumdhalilisha baba wetu wa Taifa kwa kuvunja haki za utawala bora wenye kujali kila masilahi ya umma

Aug 27, 2008

Nguvu ya Fikra ni Ukombozi Daima



Watanzania wanadhulumiwa haki yao
Fita Lutonja


TANZANIA ni nchi yenye kila aina ya rasilimali. Ina madini, misitu, mbunga za wanyama, maziwa mbalimbali kama vile Victoria, Nyasa, Tanganyika n.k.

Vile vile ina Mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu kupita milima yote barani Afrika. Sifa nyingine ya nchi yangu Tanzania ni nchi ya amani kuzidi nchi nyingine ulimwengu kote. Ama kweli mimi ninajivunia kuwa Mtanzania.

Ndiyo maana namwomba Mungu aibariki Tanzania. Tanzania ina sifa nyigi sana tangu zamani enzi za hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Nyerere aliitakia mema Tanzania, alitaka Tanzania yenye neema, Tanzania yenye kukua kiuchumi, kisaikolojia, kiutamaduni, kijamii na kisiasa.

Lakini sasa hivi mbona mambo yamebadilika? Tanzania ya leo ipo tofauti sana na ile niliyoielezea hapo juu.

Sasa hivi Tanzania inazizima, inawayawaya, inavunjika sana, inatumbukia shimoni, inanuka kila aina ya mabaya; kuna ufisadi, kuna EPA, kuna mpasuko wa kisiasa Zanzibar, kuna Richmond, kuna suala la Zanzibar ni nchi au si nchi, kuna suala la vijisenti vimefichwa Uingereza, kuna suala la Mkapa na mke wake kufanya biashara Ikulu ya Tanzania, na mengine mengi. Yote haya mbona Tanzania mnatuchanganya?

Au mumeamua kufanya hivyo kwa sababu Baba wa Taifa hayupo? Au kwa sababu mlivunja Azimio la Arusha ambalo lilikuwa linabana na kudhibiti ufisadi?

Mwalimu aliona mbali sana. Mlipovunja Azimio la Arusha ninawauliza mlitaka kila mtu ajichukulie chake? Kwa sababu ya nani haya yanatokea sasa? Tumlaumu nani kwa haya yote? Sasa mnatupeleka wapi, mbona sisi wananchi wa kawaida hatuwaelewi, mnaendelea kutuumiza!

Sasa Watanzania wanalikumbuka Azimio la Arusha. Mwalimu aliona mbali sana kipindi cha utawala wake ndiyo maana alianzisha Azimio la Arusha.

Aliona kuwa kunaweza kutokea watu wasiojali masilahi ya Watanzania wengine; walafi, mabepari, mabwenyenye, wenye fikra mbaya kwa wengine, wenye kutafuna taifa kwa kutumia dhamana ya uongozi na kusababisha Tanzania kuyumbayumba.

Watanzania sasa wanamkumbuka Baba wa Taifa kwani wanaamini angekuwepo asingevumilia mambo kama haya ya ufisadi, ambayo alikuwa anayapiga vita sana kwa nguvu zake zote.

Ninakumbuka Mwalimu baada ya kuona mambo kama haya ya ufisadi, unyonyaji n.k. yatatokea, bila ajizi aliitisha mkutano Arusha na kuanzisha Azimio la Arusha mwaka 1967.

Lilipotangazwa, wananchi wanyonge wa nchi hii, walirukaruka na kushangilia. Wananchi hao walishangilia kwa sababu waliposikia misingi ya Azimio hilo, walifahamu fika kuwa ndio ukombozi wao.

Walikuwa bado wana machungu kutokana na kunyonywa, kundamizwa, kunyanyaswa na kudhulumiwa ndani ya nchi yao wenyewe.

Walikuwa bado wana kumbukumbu za ubeberu na ukoloni ambao ulikuwa umeota mizizi na pamoja na kuwa nchi ilikuwa huru, lakini watu wengi walikuwa bado hawajaanza kufaidi matunda ya uhuru, hasa katika nyanja ya uchumi, kwa sababu yalikuwa bado mikononi mwa watu wachache.

Watanzania wanakumbuka Azimio lilisababisha kuzaliwa kwa siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Itikadi hii iliwawezesha Watanzania kushirikiana kwa kila jambo na hivyo kujenga udugu uliowafanya Watanzania wajione kuwa kama watu wa familia moja. Vilevile kujitegemea kulisababisha Watanzania kuishi kwa kujiona wao ni wao. Dhamira yao kubwa ilikuwa ni kujenga uwezo wao, ili waachane na utegemezi wa nchi nyingine. Walifahamu kuwa huo ndio uhuru wa kweli.

Ili kuhakikisha kuwa linaondoa kabisa chembe chembe za unyonyaji, Azimio la Arusha liliweka kanuni zilizokuja kujulikana kama maadili ya uongozi kwa watumishi wa umma. Kanuni hizi zilitaja mambo ambayo mtumishi wa umma, hasa kiongozi, haruhusiwi kuyafanya.

Hii ililenga kuhakikisha kuwa viongozi hawatumii nafasi walizonazo kujigeuza mabeberu, wakiritimba na wanyonyaji. Jamii iliwahakikishia viongozi kutunzwa kupitia mishahara yao. Pia dhana ya Ujamaa na Kujitegemea iliwahakikishia viongozi kuwa watakuwa sawa na wananchi wengine wanawaongoza. Azimio la Arusha lilizuia kujengeka kwa matabaka katika jamii ya walionacho na wasio nacho.

Lakini hivi sasa nchi inayumbishwa na ufisadi, unyonyaji, ukandamizaji. Watu wameshaanza kumkumbuka Baba wa Taifa. Tunajiuliza tumekosea wapi? Inaleta hisia mbaya zaidi pale ambapo wanaoonekana kuwa vinara wa ufisadi na unyonyaji ni viongozi ambao tuliwakabidhi dhamana ya kutuongoza.

Mwalimu ndani ya Azimio la Arusha na kanuni zake aliamini kuwa Watanzania wataishi kijamaa kwa kushirikiana kwa kila kitu. Alilenga kujenga umoja chini ya upendo wa kidugu. Katika mazingira kama hayo, kwenye dhamira ya dhati kabisa, isingekuwa rahisi kwa viongozi kuwageuka watu wao na kuanza kuwa wajasiriamali zaidi ya viongozi.

Azimio la Arusha la Baba wa Taifa lilikataa ubaguzi wa mtu na mtu. Lilipinga unyonyaji wa mtu na mtu. Kitu hiki kilisababisha Watanzania kipindi hicho kuwa na amani katika maisha yao, huku wakiishi kwa kupinga aina zote za dhuluma.

Lakini hivi sasa, amani hiyo ipo mashakani. Wananchi wa kawaida waliotopea katika umaskini wanapowaona viongozi wao wakiogelea katika ukwasi wa hali ya juu, huku wakihubiri umaskini, wanachanganyikiwa. Lakini viongozi wanapaswa kushikwa na hofu kwamba amani imeshaanza kutoweka.

Unapoona watu wanamwadhibu kibaka aliyeiba kuku mtaani kiasi cha kufikia kumuua kwa kumchoma moto, ujue siku itafika ambapo watafanya hivyo kwa wezi wakubwa wakubwa na wala rushwa wakubwa wakubwa. Kwani lengo lao si ni kutoa adhabu kwa wahalifu?

Viongozi wanatakiwa waanze kukaa chonjo hivi sasa. Vita dhidi ya ufisadi iliyoanza, haitakoma mpaka wananchi wa takaporidhika kuwa ushindi umepatikana kiasi cha kutosha.

Salama ya viongozi ni kujiuliza nani alivunja hili Azimio la Arusha? Wanatakiwa kueleza kinagaubaga kwa nini Azimio lilivunjwa? Huyo aliyelivunja alikuwa anawatakia nini Watanzania?

Aliyevunja azimio letu jema atuambie alikuwa ana makusudi gani kufanya hivyo? Hivi alikuwa anatutakia ufisadi, ubepari, ubeberu na mambo ya EPA? Au alitaka kuona Tanzania inawayawaya na kufikia hatua ya viongozi kuanza kufanya biashara Ikulu?

Ndiyo. Haya yote yanatokea hivi sasa kwa sababu ya kuvunjwa kwa Azimio la Arusha kwani Azimio lilikuwa halitaki mambo haya yote.

Hakika Mwalimu alikuwa anaipenda Tanzania, mbona hamkumuenzi Mwalimu?

Mnataka kutuambia kumuenzi Mwalimu ni kufanya biashara lkulu na kumiliki migodi? Mbona Azimio la Arusha lilikuwa halitaki hivyo?

Baada ya Mwalimu kung’atuka madarakani, tumeona yale ambayo alikuwa anayapiga vita yakianza kujitokeza taratibu na alipofariki yakashika kasi. Kasi ya mambo aliyoyachukia Mwalimu iliongezeka zaidi pale walipoamua kulivunja Azimio la Arusha. Wakati azimio hili lilitangazwa kwa mbwembwe zote mwaka 1967 wakati linazaliwa, lilipofutwa hata haikutangazwa!

Walikutana kimya kimya wakasema Azimio linasababisha watumishi wa serikali wakose nyumba pindi wanapostaafu. Sasa tunagundua kuwa walikuwa na nia ya kuweka misingi ya kuiba mali ya umma wakati wakiwa kazini!

Hao watu eti nao wanajiita wazalendo? Kutuvunjia misingi ya utawala bora ili muibe na kuwa mabepari, ndio uzalendo? Kuficha pesa katika benki za nje ndio uzalendo? Kujenga majumba makubwa kama mahekalu na kusomesha watoto wenu nchi za nje kwa pesa za walipa kodi ndio uzalendo? Tuelezeni Watanzania, huo ndio uzalendo wenye itikadi ya kufia nchi yako kwa kuitetea?

Kwa mimi ninavyoamini uzalendo ni ile hali ya kuwa tayari kuifia nchi yako. Kwani katika Tanzania hii hamuoni wazalendo? Hamuwaoni kina Dk. Willibrod Slaa kuwa hao ndio wazalendo?

Hamuoni kuwa wako mbele kutetea maslahi ya nchi yao? Hamuoni Baba wa Taifa kwa kuanzisha Azimio la Arusha kuwa alikuwa mzalendo? Hamuoni Edward Sokoine na kazi aliyoifanya kuwa ni mzalendo?

Kwakweli mmetufikisha pabaya sana na tunasema hatutaki kuendelea kusikia mambo ya ubepari, unyonyaji, ufisadi, EPA, biashara za Ikulu, mpasuko wa kisiasa Zanzibar na matatizo chungu nzima.

Makala hii imeandaliwa na mwananchi mwenye fikra za maendeleo. Anapatikana kwa simu: 0764 992264

Aug 23, 2008

Muda ni mali

Muda ni mali na heshima kwa watumia vizuri muda wao, hakika ukitumia muda wako vizuri utapata mafanikio na ukikata tamaa na kuaanza kulalamika hakika utabaki hivyohivyo tu yatupasa kuutumia muda wetu vizuri na hasa katika suala kujinasua katika umaskini sijalishi umaskini wa mtu mmoja pekee, hakuna bali ni umaskini wa Tanzania.

Tuijenge nchi yetu kwa kujituma kila sehemu kuhakikisha kunaijenga hata katika nyanja za kuhakikisha wanyonyaji tunawafutilia mbali, unyonyaji huu wa mabeberu yatupasa kuupinga kwa nguvu zote kwani hawa ndio chanzo cha umasikini wetu.

Sisi wazalendo tunabaki maskini huku wao wanatunyonya kila kona huku wakitutumikisha kwa malipo duni, sasa yatupasa kujikomboa kwa kudai Azimio la Arusha la baba wetu wa Taifa hayati Mwalimu J.K. Nyerere kwani hili lilikuwa mzingiti wa kukomesha unyonyaji wa mapepari na waliovunja hili Azimio yatupasa na wenyewe kuwazomea hadharani ili waone aibu ya kuvunja utawala bora wa kijamaa huku wakitupigilia kichwani mwetu bila huruma, misumari ya wapepari sijui walikuwa na ajenda gani na hawa mapepari au na wao ni mabepari?