Aug 21, 2008

Chama ni moyo

Ili kujikomboa na wanyonyaji yatupasa kuwa na umoja wenye mshikamano wa dhati umoja huo unakuja kwa kuunda chama kwahiyo wanaharakati wenzangu yatupasa sasa kuunda chama chetu cha kudai masilahi yetu wanayoyatumia kama sisi hatupo katika dunia hii kwani kimya chetu kimewafanya watuone hatuna haki.

Lakini katika maono yangu ninaona haki a wanyonge inakuja kwa nguvu zote ninaona uhuru wa kutoa maoni umekalibia watu watajikomboa kutoka kwa mabeberu makiritimba, manyonyaji, mabepari na wapinga haki yetu tuliyopewa na Hayati Mwalimu JK nyerere baba wetu wa Taifa mwenye kila aina ya sifa za kuitwa kiongozi bora Afrika. Je ninawauliza hao wabepari na wabeberu wa nchi hii huu ndio usawa wa binadamu? Mbona wenzetu mnadhurumu huku tunawaona?

No comments: