Aug 21, 2008

Habari njema

Habari zenu ndugu zangu popote pale mulipo mimi ni mzima na ninaendelea na pilikapilika za kuhakikisha haki inapatikana kutoka kwa wanyonyaji wetu wanajiita Miungu watu na kijiona wao ndio Mungu amewajalia na kuwaona na kutuona sisi kama Mungu hatupendi kumbe wanajidanganya wao wenyewe kwani Mungu wetu aliyembinguni anatupenda wote ndio maana akatupa kila kitu wote lakini wao kwa kumuuzi wakaamua kutunyang`anya na sisi haki yetu.

Watu hawa sasa wanafurahia katika dunia hii hawajui kuwa dunia hii ni ya kupita tu na makao yetu ya kudumu yako mbinguni kwa baba yetu Mungu, kule mbinguni ndio kutakuwa hakuna tena unyonyaji kama wanavyotufanyia sasa hivi huku wakitoa meno yote 36 nje kwa kujiona wao ndio wajaja kuzidi wote katika dunia hii.

No comments: