Aug 20, 2008

Dhambi ya ubaguzi

Rasilimali zetu wao wanaona kama Mungu aliwapa wenyewe na sio Watanzania wote. Wanajiamulia katika rasilimali zetu bila hata sisi kuwaruhusu wenyewe wanachukua huku wakituona sisi kama hatuna haki nazo, wakati Mungu alipotupaeia alitupa sote watanzania bila kubagua. Sasa wanaleta utawala wa kibaguzi kwa kutubagua wajili wao wakuu wakiwa na fikra za kuwa sisi ni wajinga hatujui haki zetu kumbe tunajua kila kitu, haya sasa Mungu ameshawalaani kwa kosa la kutubagua katika mali zetu, utawala wo umejaa fitna na unanuka ubaguzi kila sehemu.

Waonini sasa wamemukufuru hata Mwasisi wetu Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Watanzania kwa kushindwa kumuenzi kwa kila kitu, nakumbuka Mwalimu katika utawala wake alikuwa anapinga sana utawala wa kibaguzi, alimchukia kila mtu atakayeonekana mubaguzi kwani aliamini binadamu wote ni sawa,nakumbuka aliwahi kusema kuwa dhambi ya ubaguzi ni kubwa mno kwani ni sawa na mtu kula nyama ya mtu ambaye akiisha ila hataiacha katu.Hii ni kweli kabisa viongozi wetu mumezoea ubaguzi munatubagua sisi na hamtaacha kutubaguaa mpaka tujikomboe hapo ndio haki yetu itatimia

No comments: