Aug 20, 2008

Tumechoka kudhulumiwa

Tanzania ina kila kitu Mungu kaijalia kuwa na kila kitu ina mito na maziwa wa maji nyenye kila aina ya samaki, madini ya kila aina almasi, tanzanite, dhahabu, ulanga, makaa ya mawe,shaba, rubi nk vilevile ina milima mingi kama vile mlima Kilimanjaro ambao ni mlima mrefu kupita milima yote Afrika, mbuga za wanyma nk, vyote hivi ni mali za watanzania lakini ninashindwa kujua umasikini wetu umetoka wapi? Nani mchawi wa umasikini wetu? kwangu mimi ninavyoona mchawi anayesababisha umasini ni wale viongozi wetu hawafuati misingi ya utawala bora wenye kulinda mali hya umma bali wanauza mali zetu na kusingizia uwekezaji. uwekezaji huku munaliingizia Taifa hasara kwa mikataba mibovu lakini tunawatahadhalisha ole wenu nyinyi wanafiki ipo siku Mungu atawaadhibu kwa niaba ya watanzania, hapo ndio mtakoma na kujuta kwanini mlizaliwa Tz, lakini sasa munachekelea huku mukiendesha magari yenu ya kifisadi na kutaka kutugonga huku mukitutukana iti sie washezi, washamba hatujui hata kukwepa magari.

No comments: