Aug 20, 2008

Hakika tunaweza

Ninaimani kubwa sana Watanzania tunaweza kujikomboa na kuwa huru kifikra, kimawzo, kiuchumi, kisansi, kijamii, kisaikoloa nk, ili tujikomboe yatupasa kufikria ni viongozi gani wanatufaa? ambao watasimama kutetea haki zetu na rasilimali zetu? hakika tukijua hilo hapo ndipo tutajikomboa na kuwa huru katika haki zetu, lakini tusipojua hilo daima tutaendelea kudhulumiwa haki zetu kwani viongozi wetu hawana na huruma nasisi pamoja na watoto wetu.

Lakini hawa wanyonyaji ninawaambia siku zao zinahesabika hazikawii ukombozi wetu unakuja mbio sana kwani hata wao wenyewe wanajua sehemu walivyotukosea sasa wanawayawaya hawana imani na sisi wameanza kutuhofia kuwa hueda tukafanya mapinduzi ya kura mwaka wa uchaguzi unaofuata.

No comments: