Aug 23, 2008

Wajibu wa kijana

Kwanini kijana unakaa vichochoroni, unalala mitaroni, unabeba zege na magunia, unasukuma matololi, unakimbizwa na migambo wa mji, unatembea kwa miguu bila kupanda daladala, unashinda kutwa nzima hujatia kitu tumboni huku tumbo linakuuma na huku nguvu zinakuishia taratibu unaelekea guanguka??? Yote haya ni mfumo mbaya ndio unaokutesa kijana wangu na sioni pa kijikomboa!!!!!!

Kijana wangu inaniuma sana ninapokuona unanyanyaswa na hawa fisikoko hawayani, wezi wakubwa wa raslimali zetu ambazo Mungu alitupatia wao wanazitumia bila kukuhurumia wewe kijana na wanataka wakumalize kwa njaa ili wajitwalie raslimali zetu bila kipingamizi, sasa tuwazomee haoooooooooo weziiiiiiii wakubwaaaaa tumewashutukiaaaa sasa hatutaki kuibiwa kwani hawa ni wabaya sana wanatudanganya kwa mikataba mibovu huku wakiendelea kutufirisi mali yetu, ukienda Buzwagi wanaiba, Bulwanhgulu wapo, Geita wanaendelea kusafirisha dhahabu zetu, Mlima Ngasamo na Mererani wamejaa huku sisi tunakufa na umaskini.


Sasa kijana simama imara uitetee haki yako, wote vijanawa kike na wakiume pambaneni na mafisadi na wizi wa madini yenu hapo ndio hadhi yenu itarudi na mtakula haki yenu, ninasema we kijana acha kusinzia, acha kudhurura, acha kukaa, acha kujiona huwezi kutetea haki yako daima pambana kwa nguvu zote kurudisha heshima na uhai wako hakika utajikomboa.

No comments: