Aug 23, 2008

Muda ni mali

Muda ni mali na heshima kwa watumia vizuri muda wao, hakika ukitumia muda wako vizuri utapata mafanikio na ukikata tamaa na kuaanza kulalamika hakika utabaki hivyohivyo tu yatupasa kuutumia muda wetu vizuri na hasa katika suala kujinasua katika umaskini sijalishi umaskini wa mtu mmoja pekee, hakuna bali ni umaskini wa Tanzania.

Tuijenge nchi yetu kwa kujituma kila sehemu kuhakikisha kunaijenga hata katika nyanja za kuhakikisha wanyonyaji tunawafutilia mbali, unyonyaji huu wa mabeberu yatupasa kuupinga kwa nguvu zote kwani hawa ndio chanzo cha umasikini wetu.

Sisi wazalendo tunabaki maskini huku wao wanatunyonya kila kona huku wakitutumikisha kwa malipo duni, sasa yatupasa kujikomboa kwa kudai Azimio la Arusha la baba wetu wa Taifa hayati Mwalimu J.K. Nyerere kwani hili lilikuwa mzingiti wa kukomesha unyonyaji wa mapepari na waliovunja hili Azimio yatupasa na wenyewe kuwazomea hadharani ili waone aibu ya kuvunja utawala bora wa kijamaa huku wakitupigilia kichwani mwetu bila huruma, misumari ya wapepari sijui walikuwa na ajenda gani na hawa mapepari au na wao ni mabepari?

No comments: