Aug 22, 2008

Tanzania ya dhamani

Tanzania wewe ni wa dhamani sana hakika Mwenyezi Mungu alikujaria na kukubaliki tena kwa upendeleo, kwani kila kitu alikupatia, madini ya kila aina alikupa, mito na maziwa ya maji na zenyewe alikubariki, mbuga za wanyama kubwa zenye kuvutia kila aina ya watarii, ardhi yenye rutuba sanjari na milima mbalimbali ukiwemo mlima mrefu kupita yote Africa Kilimanjaro alikupa hakika wewe Tanzania umebarikiwa.

Lakini mimi ninakushangaa Tanzania pamoja na vitu vyote hivyo bado unaendelea kuisha na kubakia mashimo kila sehemu, huku madini wakikunyang`anya na kupeleka ughaibuni kama wewe huna watu wako!!?? hakika ninakusikitikia Tanzania wangu kwa jinsi unavyokaukia na kukonda huku ukibaki mifupa tupu!!!! samaki wako sangara wanakwapuliwa, pesa za walipa kodi wako zinafisadiwa na mafisadi wahujumu mali zako, ooooo!!!!! Ona sasa umebaki maskini huku ukiwayawaya huna pa kukimbilia!!

Ninazidi kushangaa sana wale waliokunyonya wanatembelea benzi, crusser,prado vx zenye mabillioni ya pesa zako ukiwasachi kwenye mabegi yao wanayotembea nayo yamejaa pesa zako huku wakiendelea tena kukutwisha mzigo kichwani wa makapuni yanayokufirisi, huku wewe ikibaki umekonda huna hata kitu cha kuwapa Watanzania!! Sasa yakupasa upambane na wanaokufirisi kwani watu wako watakufa kwa njaa. Haya jamani Watanzania simameni kuikomboa Tanzania Dr. Wilbroad Slaa simama, Zitto Kabwe inuka, Anne Kalango, Harisoni Mwakyembe, na wanaharati wenzanu simameni kupambana, Tanzania inaisha huku tunaiona mafisikoko wanaitafuna bila huruma kabisa.

No comments: